CCM ingemsimamisha Lowassa ingeanguka vibaya

CCM ingemsimamisha Lowassa ingeanguka vibaya

TeamCCM-2015

Senior Member
Joined
Aug 19, 2015
Posts
112
Reaction score
44
Matokeo yaliyopo sasa yanaonyesha wazi kuwa CCM ingemsimamisha Lowasa ingepigwa mwereka mbaya sana.

Hongera CCM kwa kuliona hili mapema na pia hongera sana mwana wa kitanzania na mzalendo John Pombe Magufuli.
 
Matokeo yaliyopo sasa yanaonyesha wazi kuwa CCM ingemsimamisha Lowasa ingepigwa mwereka mbaya sana.

Hongera CCM kwa kuliona hili mapema na pia hongera sana mwana wa kitanzania na mzalendo John Pombe Magufuli.
Na mbaya zaidi ingekuwa kama Magufuli anangegombea UKAWA na Lowassa CCM. CCM wangeambulia 10 % tu.
 
Heheheh...

CCM hata ikisimamisha jiwe kwa tume hii ya uchaguzi lazima jiwe lishinde...

Matokeo yaliyopo sasa yanaonyesha wazi kuwa CCM ingemsimamisha Lowasa ingepigwa mwereka mbaya sana.

Hongera CCM kwa kuliona hili mapema na pia hongera sana mwana wa kitanzania na mzalendo John Pombe Magufuli.
 
Jamaa kiburi na kujiamini kote kumbe ni kwenye uhalifu wa Mtandao. Baada ya kudakwa wale vijana ndo akaanza kulia lia mwanzo alisema uchaguzi ulikuwa huru
 
Tulisema tangu mwanzo kuwa Lowasa anaweza kuongoza mafisadi tu siyo kuongoza watanzania.
 
Jamaa kiburi na kujiamini kote kumbe ni kwenye uhalifu wa Mtandao. Baada ya kudakwa wale vijana ndo akaanza kulia lia mwanzo alisema uchaguzi ulikuwa huru
Huyu fisadi anamambo ya kihuni sana kila kitu anafanya sanaa tu.
 
Matokeo yaliyopo sasa yanaonyesha wazi kuwa CCM ingemsimamisha Lowasa ingepigwa mwereka mbaya sana.

Hongera CCM kwa kuliona hili mapema na pia hongera sana mwana wa kitanzania na mzalendo John Pombe Magufuli.

Ni kweli kabisa.CHADEMA wangemsimamisha Slaa.Halafu wakomalie hoja za ufisadi kwenye kampeni washambulie Lowasa kulia na kushoto kuwa CCM imeweka Fisadi.CCM ingeshindwa mapema asubuhi wala sio siri.Watu walijiandaa kupiga kura za hasira kuionyesha CCM kuwa hawataki fisadi Lowasa.CCM ingeondoka na kufilia mbali Lowasa angechaguliwa mgombea wa CCM.

Na CHADEMA walikuwa wanavizia iwe hivyo.Lakini Lowasa alipotimkia CHADEMA baada ya kukatwa watu wakaanza kurudisha imani kwa CCM kuwa ni chama kisichopenda mafisadi wakakipa kura.Na CHADEMA wananchi wakakiona chama cha Wakumbatia mafisadi wakakinyima kura sehemu nyingi.

CHADEMA itawachukua miaka mingi kurudisha hadhi kilichokuwa nayo mbele za wananchi na yawezekana kabisa kikafutika kwenye ramani ya Siasa nafasi yake ikachukuliwa na ACT wazalendo.Sababu generally watu hawana imani na CHADEMA tena baada ya kumkaribisha Lowasa.
 
Ccm ingefutika kwenye ramani ya siasa
 
Matokeo yaliyopo sasa yanaonyesha wazi kuwa CCM ingemsimamisha Lowasa ingepigwa mwereka mbaya sana.

Hongera CCM kwa kuliona hili mapema na pia hongera sana mwana wa kitanzania na mzalendo John Pombe Magufuli.

Kwani EL angepiga marufuku kutumika kwa zile zilizopigwa kabisa, nakusambazwa nchi nzima kama mahindi?
 
kweli kabisaaa... maana CDM walikuwa na silaha zote za ufisadi wa lowassa
 
Kama CCM ingemsimamisha Lowassa, nakuapia asingeanguka. Kumbuka katika kila uchaguzi kwa kila ngazi kuna kitu kinaitwa CCM Factor. Hiki ndicho kinawezesha wagombea kushinda kama wamesimamishwa na CCM hata kama wananchi hawawapendi.
 
Ila jamani tuseme ukweli,CCM Ingemsimamisha LOWASSA Ingekuwa na hali ngumu zaidi kuliko ilivyo sasa.
 
Mwisho wa siku kila mtu ataendelea na shughuli zake. Kama ni hali ngumu, kama ni kukosekana kwa maji, kama ni barabara mbovu, kama ni kukosekana dawa hospitalini ni mimi, wewe, ndugu zako, na watanzania wote tutaumia bila kujali nani alimchagua nani.
 
Ila jamani tuseme ukweli,CCM Ingemsimamisha LOWASSA Ingekuwa na hali ngumu zaidi kuliko ilivyo sasa.Mtu mwenyewe ukimuangalia ANATIA HURUMA SANA.CCM Kumsimamisha ingekuwa ni maajabu ya DUNIA.CDM Wanapaswa kujua CCM Siyo DP HUWEZI KUITOA KWA UJANJAUJANJA NA SHORTCUTS.Unapaswa kuwa RASLIMALI WATU MAKINI,MIPANGO NA MIKAKATI SIYO KINA MBOWE.
 
baada ya kura watu ; wangekuwa wanashangilia................. na hii slogani ndo wangetumia<br><br>mabadiliko ----ukawa<br>ukawa ...........mabadiliko<br><br>na ziito wangemkaribisha kama alivyoomba mwanzo;<br><br>jeshi lingechukua nchi
 
CCM ingemsimamisha lowassa angeshinda kwa 70% percent. Naamini hvyo, watu wangempigia kura sana kuliko ilivosasa kwa magufuli
 
Tanzania Hakuna Uchaguzi kuna CCM na tume.... Hata angewekwa Lusinde Kibajaji CCm wanabeba tena Asubuhi kabla hakujapambazuka.

mi nadhani turudi kwenye siasa za chama kimoja tu
 
Jamaa kiburi na kujiamini kote kumbe ni kwenye uhalifu wa Mtandao. Baada ya kudakwa wale vijana ndo akaanza kulia lia mwanzo alisema uchaguzi ulikuwa huru

Alidhani shetani ndiye anatawala. Alisahau Mungu naye yupo hanunuliwi kwa pesa.Na hawa vijana wasingekamatwa mapema ingekuwa hatari tupu kwa sababu wangetoa kwenye mitandao matokeo potofu yakionyesha ushindi kwa fisadi na Lowasa angeshupalia hayo kwamba ndio halisi. Hapo tungefika wapi?
 
Back
Top Bottom