Msingi Mkubwa wa Chama chochote cha siasa kwenye ushindani wa vyama vingi, ni namna kinavyoweza kujenga hoja dhidi ya hoja zinazoibuiwa na upinzani, na hatimaye wananchi waweze kubaini kuwa walichoaminishwa na upinzani kumbe ni " fix" tupu!
Tokea serikali ya awamu ya 5 ya Chama kikongwe CCM iingie madarakani miaka takribani 2 iliyopita, wao wamekuwa na kazi moja ya kupambana na wapinzani huku wakiwa "assisted" na Jeshi la Polisi kuhakikisha kuwa vyama hivyo makini vya upinzani vinakufa!
Mbinu nyingine wanayotumia hao CCM ni kuwanunua wapinzani kwa fedha taslimu au kuwaahidi vyeo, wakiamini pia kuwa kwa njia hizo wataua upinzani nchini.
Nipende kuwaambia hao maccm wanaoamini kuwa wataua upinzani kwa njia hiyo kuwa wanajidanganya kupita kiasi, kwa kuwa wanazidi kuviimarisha vyama hivyo kwa kuwa wananchi walio wengi hivi sasa wamebaini mbinu hiyo ovu ya CCM na hivyo kuwajengea chuki zaidi chama hicho kikongwe kabisa hapa nchini.
Niwaambie CCM kuwa warudi kwenye misingi iliyokianzisha chama hicho ya kurejea kuimarisha idara ya uenezi wa Chama, katika kujibu makombora ya upinzani, na kamwe wasidhani kuwa kwa kutumia "pyupyu" ndiyo wataua upinzani.
Upinzani hapa nchini hautauwawa kwa mitutu ya bunduki na wala kwa kuwanunua wapinzani, watu waachiwe waone juhudi za maendeleo zinazofanywa na serikali yao ya CCM na hapo ndipo kwa hiyari yao kila mtanzania ataona umuhimu wa kujiunga na CCM.
Na kama CCM wataendelea na mtindo wao waliounzisha wa kutumia Jeshi la Polisi kuwatisha wananchi wasio na hatia na kuwabambikia kesi, hakika tutazihesabu siku za chama cha CCM kuendelea kubaki madarakani.
Na hakika zipo kila dalili za the last minutes of the dyeing horse.......
Kwa maneno mengine ni kuwa VERY SOON, CCM watalazimika kuachia madaraka, kama watapuuza ushauri huo muhimu wa wao kuendelea kusurvive.
Mungu ibariki Tanzania na uwabariki wananchi wake wabaini Sera nzuri wanazohubiriwa na wanasiasa, whether ni kutoka chama tawala au kutoka upinzani.