Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,137
- 48,364
Ukiangalia na kuchunguza Kwa makini hali ya mvurugiko wa kisiasa nchini kwetu, utagundua ilianza mara baada tu ya CHADEMA kumchagua Tundu Lissu kuwa Mwenyekiti wao Taifa.
Mpaka leo ingawa CHADEMA imezuiliwa kufanya siasa na kuendelea kushambuliwa kila Kona, lakini unaona kabisa kuwa CCM bado hawajiamini kama wapo salama CHADEMA ikiendelea kuwepo.
Kuna watu wanayapenda Maigizo ya wana CCM hata kama wanajua ni UONGO.
Hebu fikiria zama zile za mazingaombwe, mfanya mazingaombwe ambao mara nyingi walikuwa wanajiita "Profesa" au "Dokta" anaweka kiingilio ili kuingia kwenye hayo mazingaombwe.
Lakini anapofanya michezo yake huonyesha jinsi anavyoweza kugeuza karatasi liwe pesa.
Sasa kama ana uwezo wa kugeuza karatasi kuwa pesa kwa nini mlangoni aliweka kiingilio?
CCM Kila siku inajionesha kuwa ina uwezo wa kufanya kila kitu na kujisifu chama Chao ni kikubwa na imara Afrika nzima.
Kama hizo sifa wanazosema CCM kweli wanazo, inakuwaje wanaigopa CHADEMA chama kisicho na dola?
CCM inayojisifu kwa uimara wake inaweweseshwaje na CHADEMA isiyo na Wenyeviti wa vitongoji, vijiji na mitaa wengi kuliko wao?
CCM inayojinasibu kwa mbwembwe kuwa wenyewe ni chama cha kihistoria kinakuwaje kinatumia dola kupambana na chama kilichoanzishwa mwaka 1993?
Mpaka leo ingawa CHADEMA imezuiliwa kufanya siasa na kuendelea kushambuliwa kila Kona, lakini unaona kabisa kuwa CCM bado hawajiamini kama wapo salama CHADEMA ikiendelea kuwepo.
Kuna watu wanayapenda Maigizo ya wana CCM hata kama wanajua ni UONGO.
Hebu fikiria zama zile za mazingaombwe, mfanya mazingaombwe ambao mara nyingi walikuwa wanajiita "Profesa" au "Dokta" anaweka kiingilio ili kuingia kwenye hayo mazingaombwe.
Lakini anapofanya michezo yake huonyesha jinsi anavyoweza kugeuza karatasi liwe pesa.
Sasa kama ana uwezo wa kugeuza karatasi kuwa pesa kwa nini mlangoni aliweka kiingilio?
CCM Kila siku inajionesha kuwa ina uwezo wa kufanya kila kitu na kujisifu chama Chao ni kikubwa na imara Afrika nzima.
Kama hizo sifa wanazosema CCM kweli wanazo, inakuwaje wanaigopa CHADEMA chama kisicho na dola?
CCM inayojisifu kwa uimara wake inaweweseshwaje na CHADEMA isiyo na Wenyeviti wa vitongoji, vijiji na mitaa wengi kuliko wao?
CCM inayojinasibu kwa mbwembwe kuwa wenyewe ni chama cha kihistoria kinakuwaje kinatumia dola kupambana na chama kilichoanzishwa mwaka 1993?