Source :Gazeti la mwanachi |
Tuesday, 14 June 2011 21:43 |
Neville Meena, Dodoma HOJA ya kutaka kufutwa kwa posho za vikao za wabunge na watumishi wengine wa umma wa imechukua sura mpya baada ya jana Mbunge wa Bumbuli (CCM), Januari Makamba kuliambia Bunge mjini hapa kuwa suala la kufutwa kwa posho ni la kitaifa na ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano uliowasilishwa na serikali.Kauli hiyo yab Makamba ambaye pia ni Katibu wa Mambo ya Nje wa Sekretarieti ya CCM imekuja huku kukiwa na malumbano makali baina ya Spika wa Bunge, Anne Makinda na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe kuhusu suala hilo la posho za vikao vya wabunge. |
Hivi Hawa CCM akili zao zipo kichwani? hayo maneno ya Makamba ( niliyokoleza Red..) ni kweli yametoka serikalini au ni Chadema ilikuja na huo mpango?? mbona serikali inapenda sana kucopy na kupaste bila hata kuedit?
Si wangesema tu wazo la Chadema ni zuri kufuatwa????