Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,894
Tabia ya uropokaji aliyo nayo Nape ni sawa CCM wameruka jivu na kukanyaga moto. Afadhali ya mzee makamba kadiri ya mizani yangu,
Kuna mambo kadhaa ambayo CCM inatakiwa kuwa macho sana kutokana na nyendo za Nape na kundi lake.
Katika mikutano sasa anaambatana na kundi lake la CCJ, kwa maana kwamba anakigawa chama.
Kuidhalilisha serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusiana na mwafaka na kudai kwamba Makamu wa Kwanza wa Rais Seif Shariff alikubali kwa sababu ya njaa na sasa anang'aa sababu ya whisk ya ikulu. Ni dalili dhahiri baadhi ya wanaccm Bara hawaridhiki kumwona Seif serikalini na kuingilia mambo ya Zanzibar yenye katiba yao.
Kumtuhumu mkuu wake Rais Kikwete kwamba ajivue gamba badala ya kukutana naye kumshauri badala ya kumwanika kwenye vyombo vya habari.
Kuwatukana na kuwadhalilisha viongozi wa upinzani si kwa hoja bali mashambulizi ya mtu binafsi.
Rostam aliongea maneno mazito ya siasa uchwara za Nape na Chillingati wanavyofanya kinyume cha makubaliano ya mikutano ya CCM.
Kwa jicho la upembuzi lile kundi la CCJ lililoasisiwa na Samweli Sitta, Nape na Mpendazone sasa linaanza kujitokeza zaidi na kufuatana pamoja kwenye mikutano kama ilivyotokea Mbeya.
Mwenye nacho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia.
Kuna mambo kadhaa ambayo CCM inatakiwa kuwa macho sana kutokana na nyendo za Nape na kundi lake.
Katika mikutano sasa anaambatana na kundi lake la CCJ, kwa maana kwamba anakigawa chama.
Kuidhalilisha serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusiana na mwafaka na kudai kwamba Makamu wa Kwanza wa Rais Seif Shariff alikubali kwa sababu ya njaa na sasa anang'aa sababu ya whisk ya ikulu. Ni dalili dhahiri baadhi ya wanaccm Bara hawaridhiki kumwona Seif serikalini na kuingilia mambo ya Zanzibar yenye katiba yao.
Kumtuhumu mkuu wake Rais Kikwete kwamba ajivue gamba badala ya kukutana naye kumshauri badala ya kumwanika kwenye vyombo vya habari.
Kuwatukana na kuwadhalilisha viongozi wa upinzani si kwa hoja bali mashambulizi ya mtu binafsi.
Rostam aliongea maneno mazito ya siasa uchwara za Nape na Chillingati wanavyofanya kinyume cha makubaliano ya mikutano ya CCM.
Kwa jicho la upembuzi lile kundi la CCJ lililoasisiwa na Samweli Sitta, Nape na Mpendazone sasa linaanza kujitokeza zaidi na kufuatana pamoja kwenye mikutano kama ilivyotokea Mbeya.
Mwenye nacho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia.