CCM imejiandaaje kuuzima mpasuko huu?

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,894
Tabia ya uropokaji aliyo nayo Nape ni sawa CCM wameruka jivu na kukanyaga moto. Afadhali ya mzee makamba kadiri ya mizani yangu,
Kuna mambo kadhaa ambayo CCM inatakiwa kuwa macho sana kutokana na nyendo za Nape na kundi lake.
Katika mikutano sasa anaambatana na kundi lake la CCJ, kwa maana kwamba anakigawa chama.
Kuidhalilisha serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusiana na mwafaka na kudai kwamba Makamu wa Kwanza wa Rais Seif Shariff alikubali kwa sababu ya njaa na sasa anang'aa sababu ya whisk ya ikulu. Ni dalili dhahiri baadhi ya wanaccm Bara hawaridhiki kumwona Seif serikalini na kuingilia mambo ya Zanzibar yenye katiba yao.
Kumtuhumu mkuu wake Rais Kikwete kwamba ajivue gamba badala ya kukutana naye kumshauri badala ya kumwanika kwenye vyombo vya habari.
Kuwatukana na kuwadhalilisha viongozi wa upinzani si kwa hoja bali mashambulizi ya mtu binafsi.
Rostam aliongea maneno mazito ya siasa uchwara za Nape na Chillingati wanavyofanya kinyume cha makubaliano ya mikutano ya CCM.

Kwa jicho la upembuzi lile kundi la CCJ lililoasisiwa na Samweli Sitta, Nape na Mpendazone sasa linaanza kujitokeza zaidi na kufuatana pamoja kwenye mikutano kama ilivyotokea Mbeya.

Mwenye nacho haambiwi tazama na mwenye masikio haambiwi sikia.
 
.
Rostam aliongea maneno mazito ya siasa uchwara za Nape na Chillingati wanavyofanya kinyume cha makubaliano ya mikutano ya CCM.

Kwa jicho la upembuzi lile kundi la CCJ lililoasisiwa na Samweli Sitta, Nape na Mpendazone sasa linaanza kujitokeza zaidi na kufuatana pamoja kwenye mikutano kama ilivyotokea Mbeya. .

kumbe gamba rostam alikuwa sahihi sasa ameongoka jamaa wameamia kwa maalimu SEIF,
Hivi NAPE haoni tumbo lake hiyo kama mimba baada ya kuukwaa ukatibu itikadi anaongelea mng'alo wa huyo mzee wa watu.

anyway CUF wacha nao wakome uwezi kufanya ushirika na mwizi na hapo ndipo wanawawinda chadema huko ARUSHA
 
If there is ever a time when CCM as a party had a leader who is divisive and party killer it is this time and that leader is none other than Nnauye. He holds the key to door that takes CCM to heaven, he is a party liability, he is leadership liability and the price of having him in party leadership will be paid by the party itself and the chairman.
 
I don't give a da.mn about CCJ or CCM crap. Both parties must be dismantled and go down the toilet after 50 years of breeding poverty and corruption
 
CCM ikivua gamba inapatikana CCJ; sasa unalaum nini au wewe ni gamba
 
kumbe gamba rostam alikuwa sahihi sasa ameongoka jamaa wameamia kwa maalimu SEIF,
Hivi NAPE haoni tumbo lake hiyo kama mimba baada ya kuukwaa ukatibu itikadi anaongelea mng'alo wa huyo mzee wa watu.

anyway CUF wacha nao wakome uwezi kufanya ushirika na mwizi na hapo ndipo wanawawinda chadema huko ARUSHA

Kiongozi unapopanda jukwaani tumefundishwa na kusisitizwa kwamba andaa utakayosema, na hata kama utasoma kwenye karatasi ni bora kuwapa watu kitu ulichokiandaa na kukihakiki. Lakini hii ya kupagawa jukwaani na kuanza kutema matapishi kama mtu scrubu moja imelegea inahitaji kukazwa na wrench hapa kazi kweli kweli
 
Back
Top Bottom