Sina mahusiano makubwa na siasa za CCM ila nimehakikishiwa kipande hiki kweli kimetokea. Cha ajabu ni kwamba maslahi ya Wananchi na kuliweka Taifa kwanza zinaitwa ni sera za Upinzani... Hapo mishipa ya akili imesimama, sijui niseme nini kuhusiana na CCM..
Hapana ccm ni chama makini kama kilivyo chadema cuf nk Ila kuna watu ndani ya vyama hivyo kuna mifisadi tu .
Huwezi sema chadema ama SLAA ama ZITTO ndio kaanzisha hii move nenda nyuma kidogo uone nani alisababisha IDD SIMBA kujiuzulu,nani alisababisha Mbilinyi kama sikosei waziri wa fedha kujiuzulu na kwa sababu zipi?
Nakumbuka enzi hizo ilikuwa ni SKENDO akina Dr SLAA wao wameiita MAFISADI.Huwezi kabisa ku hadaa watu kwa kusema uvumbuzi wa uovu umeanzishwa na chadema .Sema kweli hili la EPA ndilo limeshkiliwa bango na SLAA.
Hizi juhudi ktk hili kuna jamaa wanalichukulia ili kupata umaarufu kisiasa kitu ambacho kipo tu enzi na enzi.
Hili la Tarime ccm kushindwa wala msilichukulie eti ndio mwanzo wa ukombonzi NEVER tumeona akina MREMA wakibebwa ,gari lao likisukumwa .tuambieni ukweli wakati wa MREMA na saizi CHADEMA ni wakati upi watanzania walipenda upinzani??
Pia tuambiane wakati Mrema ana wabwaga CCM temeke napo tutasema vipi?
Tatizo letu tunapenda kuzidaganya akili zetu kwa vitu vidogo kuwa vikubwa .
Ukombozi unahitajika LAkini si kwa viongozi wa vyma vilivyopo