Kama unavyosema, huu utaratibu wa kofia mbili unafaa kwa nchi zilizoendelea. Kumbuka Tanzania ni moja ya nchi ya dunia ya tatu.
Tanzania haijafikia kwenye kiwango cha siasa za nchi zilizoendelea na kulazimisha itakuwa kama kumlazimisha mtoto kuanza kukimbia wakati hata kukaa hajaweza.
Mazingira ya Siasa za Tanzania hayaruhusu kofia ya Rais wa Nchi na Mwenyekiti wa Chama Taifa kushikwa na watu wawili tofauti. Hii inasababishwa na Katiba ya Tanzania.
Katiba ya Tanzania imejenga mazingira ambayo kama kofia mbili zitatenganishwa, basi kuna hatari ya kuwepo mvurugano ndani ya chama ambao pia utaathiri moja kwa moja utendaji wa serikali.
Mbaya zaidi, hii CCM ya sasa inahitaji kusafishwa kabla hata ya kuanza kufikiria kutenganisha kofia mbili.