Katika hali isiyo ya kawaida Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam John Guninita amemshambulia vikali waziri wa ushirikiano Afrika Mashariki Samwel Sitta kwamba anataka kuua chama.
Guninita alitoa shutuma hizo jana kwenye mikutano ya CCM.
Ifuatayo ni sehemu ya hotuba yake kama ilivyonukuliwa na gazeti la majira la leo:
''Viongozi wa namna hii tusiwavumilie hata kidogo mtu kama Waziri Sitta hawezi kukaa kwenye mkutano kama ule na kusema maneno ya namna hiyo ikizingatiwa yeye alikuwa waziri tangu enzi za hayati Mwalimu Julius Nyerere, lakini pia utaratibu wetu ni kwamba mtu akikerwa na jambo fulani anakaa kwenye vikao na kuzungumza hivyo kuzungumza maneno hayo ndiko kunakusababisha chama kishindwe kwenye chaguzi.
"Isiwe kuwa ni hasira ya kuondolewa uspika ndiyo inayo mpelekea kusema hivyo kwani kilichofanyika bungeni ni kutaka 50 kwa 50 kwamba kipindi hiki aongoze mwanamke ambaye ni Mheshimiwa Anne Makinda, hivyo aache kuleta nongwa kwenye chama, ninawaomba ndugu zangu wana CCM mpuuze Waziri Sitta kwani inaonekana ana mipango yake mingine anayoijua mwenyewe," alisema Mwenyekiti huyo.
Alisema kuwa maneno ya Waziri huyo ni ya kukibomoa chama kwani hajatumwa na Katibu Mkuu Taifa, Bw. Wilson Mukama wala Rais Kikwete na kwamba viongozi hao hawawezi kumtuma maneno ya kubomoa serikali yao na kuuyumbisha umma kama alivyofanya''
Mwisho wa kunukuu......
Guninita alitoa shutuma hizo jana kwenye mikutano ya CCM.
Ifuatayo ni sehemu ya hotuba yake kama ilivyonukuliwa na gazeti la majira la leo:
''Viongozi wa namna hii tusiwavumilie hata kidogo mtu kama Waziri Sitta hawezi kukaa kwenye mkutano kama ule na kusema maneno ya namna hiyo ikizingatiwa yeye alikuwa waziri tangu enzi za hayati Mwalimu Julius Nyerere, lakini pia utaratibu wetu ni kwamba mtu akikerwa na jambo fulani anakaa kwenye vikao na kuzungumza hivyo kuzungumza maneno hayo ndiko kunakusababisha chama kishindwe kwenye chaguzi.
"Isiwe kuwa ni hasira ya kuondolewa uspika ndiyo inayo mpelekea kusema hivyo kwani kilichofanyika bungeni ni kutaka 50 kwa 50 kwamba kipindi hiki aongoze mwanamke ambaye ni Mheshimiwa Anne Makinda, hivyo aache kuleta nongwa kwenye chama, ninawaomba ndugu zangu wana CCM mpuuze Waziri Sitta kwani inaonekana ana mipango yake mingine anayoijua mwenyewe," alisema Mwenyekiti huyo.
Alisema kuwa maneno ya Waziri huyo ni ya kukibomoa chama kwani hajatumwa na Katibu Mkuu Taifa, Bw. Wilson Mukama wala Rais Kikwete na kwamba viongozi hao hawawezi kumtuma maneno ya kubomoa serikali yao na kuuyumbisha umma kama alivyofanya''
Mwisho wa kunukuu......