Ndiyo mkuu, maswali yajibiwe, tusisahau kuwa siasa na uwanaharakati sio sawa!! mtu akiamua kuwa mwanaharakati siku akigeuka kuwa mwanasiasa, ni sawa na kugeuka misingi uliyojiwekea!! MMMKJJ anageuka misingi aliyojiwekea, sasa moja na moja inakuwa 11 na anaona ni sawa tu!!
Naona napata swali lingine. CCM awamu ya nne wamefanya nini kustahili kuendelea na dhamana ya uongozi wa taifa? Is there anything they can show to intelligent men kuwa walifanya na watafanya nini wakipewa tena 2010.
Mwanakijiji unaweza kutuma ka-inzi kako kwenye ofisi ya CUF, maana kwa uzoefu wangu wa siku za nyuma inaonekana kuwa mchezo unakuwa wa kawaida. CUF inashinda CCM itawala, CUF wanacharazwa bakora unaitishwa mwafaka, life goes on. Naona this time around kumekuwa kimya kiasi au ndio kuwa viongozi wachache wa CUF wamelambishwa asali, wanakaa kimya, halafu wataanza kulalama baada ya Oktoba? Huko Zanzibar nako kula swali kama hilo wamefanya nini kustahili tena dhama ya uongozi??
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.