VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Leo hapa Dodoma kilifanyika Kikao cha Kamati Kuu (CC) ya CCM. Kiliitishwa hasa kwa ajenda ya kujadili na kupitisha jina la Mgombea wa Ubunge katika Uchaguzi Mdogo katika Jimbo la Chalinze,mkoani Pwani.Kikao husika kiliongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Taarifa za kuaminika toka ndani ya kikao hicho zinaonesha kuwa hakukuwa na mjadala juu ya Mgombea wa Chalinze na badala yake CC ililipitisha tu jina la aliyeongoza katika kura za maoni Jimboni humo. Muda mwingi wa CC ulitumika kujadili mvutano unaoendelea katika Bunge la Katiba na CC imeandaa na kutoa maagizo kwa viongozi wa Wajumbe watokanao na CCM.
"Hakukuwa na majadiliano. Hata kwangu ni mara ya kwanza kuona mambo haya.Mwenyekiti alitupisha kwakuwa mmoja wa wagombea anamuhusu. Majina ya wagombea wa ndani ya chama yalisomwa pamoja na kura zao na Kaimu Mwenyekiti aliwataka Wajumbe waache matokeo kama yalivyo ili kuheshimu demokrasia ndani ya chama na Jimboni Chalinze. Wajumbe hawakuwa na ubishi. Jina lililoongoza la Ridhiwani Jakaya Kikwete lilipita kirahisi hivyo.Hakukuwa na ubishani wowote wala mjadala" kilidokeza chanzo hicho ambacho ni Mjumbe wa CC toka Zanzibar
"Tulitumia muda mwingi tulilijadili Bunge la Katiba.CC imetoa maelekezo kwa Wajumbe wote.Maagizo husika ni ultimutum kwa Wajumbe wote.Msimamo wa chama ni ule ule. Ni kura ya WAZI na Serikali mbili. Chama kubadilika ni ngumu sana hasa wakati huu ambapo panaonekana kama kuna ushindani. Hatutakubali kuonekana tumeshindwa" kiliongeza chanzo hicho
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
Taarifa za kuaminika toka ndani ya kikao hicho zinaonesha kuwa hakukuwa na mjadala juu ya Mgombea wa Chalinze na badala yake CC ililipitisha tu jina la aliyeongoza katika kura za maoni Jimboni humo. Muda mwingi wa CC ulitumika kujadili mvutano unaoendelea katika Bunge la Katiba na CC imeandaa na kutoa maagizo kwa viongozi wa Wajumbe watokanao na CCM.
"Hakukuwa na majadiliano. Hata kwangu ni mara ya kwanza kuona mambo haya.Mwenyekiti alitupisha kwakuwa mmoja wa wagombea anamuhusu. Majina ya wagombea wa ndani ya chama yalisomwa pamoja na kura zao na Kaimu Mwenyekiti aliwataka Wajumbe waache matokeo kama yalivyo ili kuheshimu demokrasia ndani ya chama na Jimboni Chalinze. Wajumbe hawakuwa na ubishi. Jina lililoongoza la Ridhiwani Jakaya Kikwete lilipita kirahisi hivyo.Hakukuwa na ubishani wowote wala mjadala" kilidokeza chanzo hicho ambacho ni Mjumbe wa CC toka Zanzibar
"Tulitumia muda mwingi tulilijadili Bunge la Katiba.CC imetoa maelekezo kwa Wajumbe wote.Maagizo husika ni ultimutum kwa Wajumbe wote.Msimamo wa chama ni ule ule. Ni kura ya WAZI na Serikali mbili. Chama kubadilika ni ngumu sana hasa wakati huu ambapo panaonekana kama kuna ushindani. Hatutakubali kuonekana tumeshindwa" kiliongeza chanzo hicho
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)