Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 31,139
- 88,799
Wakuu, kwema?
Wengi tunabadirisha engine oil kila mara, lakini tunasahau fluids zingine muhimu sana, mfano coolants na brake fluids.
Leo kwenye muendelezo wetu wa service, tuzungumzie coolant na brake fluid ambazo zikipuuzwa zinaweza kuharibu engine au system ya breki au zikakupa majanga makubwa.
Coolant na Kazi zake:
Hii ni fluid inayowekwa kwenye gari kwa madhumuni ya kupooza engine (na components zake), kuzuia kutu kwenye radiator na block.
Interval:
Badilisha kila baada ya miaka 2 au km 40,000–60,000 kutegemea na mazingira.
Unavyobadirosha usichanganye rangi tofauti, mfano nyekundu na green. Kwahiyo ni vema kujua gari lako linatumia coolant ya rangi gani.
Kutegemea na gari lako, magari mengi yanapokea lita 4-6 ila pia yapo makubwa kama Harrier au Prado yanameza lita 7-9.
Ukienda kununua lazima ujue unapewa concentrate coolant (ambayo utachanganya na distilled water 50/50) au ready to use coolant ambayo wameshachanganya wewe unamimina tu.
Bei zake mara nyingi ni 20,000 hadi 35,000 kwa lita na vitup vingi vya mafuta utazipata.
Ukienda garage hakikisha wamefanya flush (kusafisha system kabla ya kujaza mpya), na pia hakikisha air bubbles zimeisha baada ya kujaza na please usimix colors.
Brake Fluid na Kazi yake:
Hii fluid inawekwa kwenye system ya breki kwa malengo ya kupeleka pressure kutoka kwa pedal hadi brakes pindi unapokanyaha. Mara nyingi unyevu (humidity) inapelekea ipoteze uwezo wake wa kufanya kazi na kuathiri perfomance ya breki.
Interval:
Unashauriwa kubadirisha kila baada ya miaka 2 au km 40,000. Kutegemea na maelezo ya gari yako, utatumia DOT 3 au DOT 4 tu, usichanganye.
Magari mengi yanapokea lita 1 kushuka chini, na bei zake haizidi elfu 20 kwa lita moja.
Hii ukienda garage hakikisha amefanya bleeding asifanye topup na ikibaki usirudi nayo home kama una watoto.
Me naona niishie hapa. Kama kuna mtu ana cha kuongeza karibu.
Wengi tunabadirisha engine oil kila mara, lakini tunasahau fluids zingine muhimu sana, mfano coolants na brake fluids.
Leo kwenye muendelezo wetu wa service, tuzungumzie coolant na brake fluid ambazo zikipuuzwa zinaweza kuharibu engine au system ya breki au zikakupa majanga makubwa.
Coolant na Kazi zake:
Hii ni fluid inayowekwa kwenye gari kwa madhumuni ya kupooza engine (na components zake), kuzuia kutu kwenye radiator na block.
Interval:
Badilisha kila baada ya miaka 2 au km 40,000–60,000 kutegemea na mazingira.
Unavyobadirosha usichanganye rangi tofauti, mfano nyekundu na green. Kwahiyo ni vema kujua gari lako linatumia coolant ya rangi gani.
Kutegemea na gari lako, magari mengi yanapokea lita 4-6 ila pia yapo makubwa kama Harrier au Prado yanameza lita 7-9.
Ukienda kununua lazima ujue unapewa concentrate coolant (ambayo utachanganya na distilled water 50/50) au ready to use coolant ambayo wameshachanganya wewe unamimina tu.
Bei zake mara nyingi ni 20,000 hadi 35,000 kwa lita na vitup vingi vya mafuta utazipata.
Ukienda garage hakikisha wamefanya flush (kusafisha system kabla ya kujaza mpya), na pia hakikisha air bubbles zimeisha baada ya kujaza na please usimix colors.
Brake Fluid na Kazi yake:
Hii fluid inawekwa kwenye system ya breki kwa malengo ya kupeleka pressure kutoka kwa pedal hadi brakes pindi unapokanyaha. Mara nyingi unyevu (humidity) inapelekea ipoteze uwezo wake wa kufanya kazi na kuathiri perfomance ya breki.
Interval:
Unashauriwa kubadirisha kila baada ya miaka 2 au km 40,000. Kutegemea na maelezo ya gari yako, utatumia DOT 3 au DOT 4 tu, usichanganye.
Magari mengi yanapokea lita 1 kushuka chini, na bei zake haizidi elfu 20 kwa lita moja.
Hii ukienda garage hakikisha amefanya bleeding asifanye topup na ikibaki usirudi nayo home kama una watoto.
Me naona niishie hapa. Kama kuna mtu ana cha kuongeza karibu.