Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Wadau wa JF hebu mnisaidie hili, hivi hizi kamera za cctv zinaweza kweli kubaini mtu aliyeiba mtihani toka ofisi za Baraza la mitihani na kutoka nao nje?. Kwa sababu kunatakiwa awepo mtumishi ambaye atakuwa akifuatilia nyendo za watumishi kwenye komputa ambayo inaziongoza kamera hizo. Sasa kilichowashinda hawa watumishi kutoitunza mitihani wakati huu sizani kama Wizara ya Elimu au Baraza la Mitihani wamebaini sababu zake la sivyo mimi sioni kwa namna gani uthibitisho wa waziri unaweza kutimizwa.
Kinachotakiwa hapa ni maadili ya kusema hili jambo siyo sahihi na kwa maana hiyo Wizara ya Elimu pamoja na Baraza la Mitihani walitakiwa kubaini vitu vinavyowawezesha watumishi kuwa na hulka hiyo.
Kuna siku moja tulikuwa tunafanya kazi na Mtumishi mmoja wa Benki fulani. Baada ya kufanya ila kazi, Mnene wa Wizara fulani ambaye ndiye aliyekuwa anahusika na kazi hiyo akaamua kutulipa kifuta jasho. Lakini yule jamaa wa benki alikataa kupokea fedha ile kwa maelezo kuwa tayari Ofisi yake ilishamlipa kwa kazi ile. Nilifurahia na kutamani kama siku moja na watumishi wa serikali wangefikia hali hiyo naamini kusingelikuwa na wizi wa mitihani na mambo mengine yanayofanana na hayo katika utoaji wa huduma kwa umma
Kinachotakiwa hapa ni maadili ya kusema hili jambo siyo sahihi na kwa maana hiyo Wizara ya Elimu pamoja na Baraza la Mitihani walitakiwa kubaini vitu vinavyowawezesha watumishi kuwa na hulka hiyo.
Kuna siku moja tulikuwa tunafanya kazi na Mtumishi mmoja wa Benki fulani. Baada ya kufanya ila kazi, Mnene wa Wizara fulani ambaye ndiye aliyekuwa anahusika na kazi hiyo akaamua kutulipa kifuta jasho. Lakini yule jamaa wa benki alikataa kupokea fedha ile kwa maelezo kuwa tayari Ofisi yake ilishamlipa kwa kazi ile. Nilifurahia na kutamani kama siku moja na watumishi wa serikali wangefikia hali hiyo naamini kusingelikuwa na wizi wa mitihani na mambo mengine yanayofanana na hayo katika utoaji wa huduma kwa umma