CAF yafuta michuano ya Afcon U-17

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Sep 11, 2020
69
104
IMG_20210309_003335_486.jpg

Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limefuta mashindano ya fainali za Afcon kwa vijana chini ya umri wa miaka 17

Mashindano hayo ambayo yalikuwa yafanyikie Morocco yalitarajiwa kuanza Machi 13

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania vijana chini ya miaka 17 tayari kipo Morocco na mchezo wao wa kwanza ulipangwa kuchezwa Machi 14 dhidi ya Nigeria

Kamati ya Dharura ya CAF ilikutana Jumatatu, Machi 08, 2021 huko Rabat, Morocco ili kuamua juu ya kufanyika kwa michuano ya Afcon U-17 2021

Kamati ilifahamishwa juu ya vizuizi vinavyokabiliwa na baadhi ya washiriki pamoja na nchi mwenyeji wa michuano hiyo ikiwa ni pamoja na uwepo wa janga la Korona .

Aidha kwa kuzingatia kuwa FIFA ilifuta Kombe la Dunia la Vijana chini ya miaka 17 kwahiyo hata Afcon U-17 ingeendelea wasingeweza kufuzu kombe la dunia

Kuibuka tena kwa janga la Covid19 na kuongezeka kwa vizuizi katika safari za kimataifa na kutokuwa na uhakika juu ya mabadiliko ya hali hiyo Kwa sababu hizi zote, Kamati iliamua kughairisha mashindano hayo
 
Dah! Hao CAF wana akili sana. Vijana warudi tu waje walisukume gurudumu la maisha. Itawasaidia pia vijana kujipanga kwa ajili ya mashindano yajayo.
 
Bora tu yameahirishwa. Tumechoka kuona kila siku timu zetu za Taifa zikienda tu kushiriki badala ya kwenda kushindana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom