CAF inakuwaje fainali ikawa mara 2?

CAF inakuwaje fainali ikawa mara 2?

Africa hatupo sawa kiuchumi na Ulaya, sasa fanal kwa mfano ifanyike South Africa ni wabongo wangapi wataakwenda? na ni wa south wangapi wataweza kukava mapenga kuingia uwanjani?
 
Mazingira ya Africa ndio yanasababisha waweke hivyo... Uliweka fainali moja Neutral venue, hautapata hata mashabiki... Hakutakuwa na usawa kabisa... Miundombinu na Usafiri kwa mashabiki kuhudhuria fainali tatizo pia... Mfano watanzania wangapi wanaweza kusafiri kwenda Morocco kusapoti timu?? Tusilinganishe Africa na Ulaya.
Yale yale ya mashabiki wangapi wanaweza enda Zanzibar toka Bara kuangalia marudiano!?
 
Final(Mwisho) au tamati hivi kwa Afrika neno Hili limegeuzwa nyuma mbele mbele nyuma Why?kila kitu kwetu ni tatizo?

Leo Mada ingelikuwa Moja tu,ila kwa upuuzi wa CAF tunasubirishwa untill next week.

Shame on you
Simba Bingwa....
 
Mapungufu ya federation sio hayo.
Ni pamoja na kukimbilia kupiga mikwaju ya penati baada ya dakika 90...

Hivi fikiria mechi kubwa yenye hadhi ya fainali ikitokea aggregate ya magoli ikifanana, inaamuriwa kwa matuta bila kwenda kwenye extra time.

Unakuta miundombinu ipo, lakini tunaishi maisha yaleyale.
 
Back
Top Bottom