CAF inakuwaje fainali ikawa mara 2?

CAF inakuwaje fainali ikawa mara 2?

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,652
Reaction score
5,133
Final(Mwisho) au tamati hivi kwa Afrika neno Hili limegeuzwa nyuma mbele mbele nyuma Why?kila kitu kwetu ni tatizo?

Leo Mada ingelikuwa Moja tu,ila kwa upuuzi wa CAF tunasubirishwa untill next week.

Shame on you
 
Mazingira ya Africa ndio yanasababisha waweke hivyo... Uliweka fainali moja Neutral venue, hautapata hata mashabiki... Hakutakuwa na usawa kabisa... Miundombinu na Usafiri kwa mashabiki kuhudhuria fainali tatizo pia... Mfano watanzania wangapi wanaweza kusafiri kwenda Morocco kusapoti timu?? Tusilinganishe Africa na Ulaya.
 
Mazingira ya Africa ndio yanasababisha waweke hivyo... Uliweka fainali moja Neutral venue, hautapata hata mashabiki... Hakutakuwa na usawa kabisa... Miundombinu na Usafiri kwa mashabiki kuhudhuria fainali tatizo pia... Mfano watanzania wangapi wanaweza kusafiri kwenda Morocco kusapoti timu?? Tusilinganishe Africa na Ulaya.
hilo haliwezi kuwa tatizo.
 
Wamefanya ivyo kwa sababu za kiuchumi, mapatato ya CAF yanaongezeka, Pia Kuna baadhi ya Timu hazitakua na mashabiki wengi kwenye fainal itakayo chezwa (neutral ground)
Inaweza tokea Fainal ikawa na mashabiki wengi wa upande mmoja kwasababu za ki uchumi.

Chukulia bila Ndege ya mama Simba ingeweza kusafiri na mashabiki wangapi kwenda Berkane wenye uwezo wa kujitegemea kwa Kila kitu?
 
Hata kama ni roho mbaya hii yako ni extraordinary mkuu🙌🏽

Mpira ni kwa ajili ya mashabiki mkuu. Bila mashabiki mpira ni useless. Afrika bado hatujafikia uchumi wa watu kusafiri kuzifuata tim zao popote zitakapocheza. Mfano fainali ipigwe neutral ground tufanye South Africa, hapo ni mashabi wachache wataweza kuhudhuria kuishuhudia tim yao, sababu kubwa ikiwa uwezo kiuchumi. Ndio maana fainali inapigwa home and away, yote kuwapa mashabiki wanachostahili.

Acha roho mbaya kiongozi.
 
Mi nilishichanga kufuatili mipira ya afrika kutokana na mambo yao
Tatizo mnataka kila kitu mfanane na wazungu na amuwezi.

Ebu assume fainali inafanyika south africa kati ya simba na Barkane.
Huoni km itakosa mvuto kabisa, ni mashabiki wangapi wataweza kusafiri kwenda kuzishangilia timu zao? Au unataka fainali ya club bingwa ionekane km ndondo cup
 
Hata kama ni roho mbaya hii yako ni extraordinary mkuu🙌🏽

Mpira ni kwa ajili ya mashabiki mkuu. Bila mashabiki mpira ni useless. Afrika bado hatujafikia uchumi wa watu kusafiri kuzifuata tim zao popote zitakapocheza. Mfano fainali ipigwe neutral ground tufanye South Africa, hapo ni mashabi wachache wataweza kuhudhuria kuishuhudia tim yao, sababu kubwa ikiwa uwezo kiuchumi. Ndio maana fainali inapigwa home and away, yote kuwapa mashabiki wanachostahili.

Acha roho mbaya kiongozi.
hapana,inapunguza vibe la Ubingwa.

Leo tungekuwa tunaamka na habari moja tu.
 
hapana,inapunguza vibe la Ubingwa.

Leo tungekuwa tunaamka na habari moja tu.
Upo sahihi kabisa. Kuna mtu nilimwambia vibe la tim yako kushinda UCL ni kubwa kuliko ikishinda EPL, sababu ubingwa wa EPL ni unauona kabisa ulee unakuja hivyo kuna kuzoea flani, ila UCL, ni dk90 boom. Hata hili ni hivyo hivyo, ila sababu kubwa ni hio, mpira ni kwa ajili ya mashabiki na uchumi wetu africa bado haurusu mashabiki wengi kusafiri kifuata tim zao
 
Africa ni bara maskini mashabiki hatuna hela za kusafiri kama ulaya. Pia miundombinu ya kuunganisha nchi za africa kama treni za umeme na ma trams hakuna

Caf walijaribu kuweka fainali mechi moja katika neutral ground wakajikuta viwanja wazi mashabiki hakuna
 
Mazingira ya Africa ndio yanasababisha waweke hivyo... Uliweka fainali moja Neutral venue, hautapata hata mashabiki... Hakutakuwa na usawa kabisa... Miundombinu na Usafiri kwa mashabiki kuhudhuria fainali tatizo pia... Mfano watanzania wangapi wanaweza kusafiri kwenda Morocco kusapoti timu?? Tusilinganishe Africa na Ulaya.
Umesema vyema ndugu. Wakati mwingine lazima tuhusishe uhalisia wetu. Na pia game 2 kuna namna zina ladha yake tofauti na game moja.

Ila, walimwengu walivyo wa ajabu Ulaya wangekuwa wanacheza game 2 na Afrika game moja bado wangerudi hapa kusema tucheze game 2.
 
Final(Mwisho) au tamati hivi kwa Afrika neno Hili limegeuzwa nyuma mbele mbele nyuma Why?kila kitu kwetu ni tatizo?

Leo Mada ingelikuwa Moja tu,ila kwa upuuzi wa CAF tunasubirishwa untill next week.

Shame on you
Mkuu team za uarabuni ndio hawataki mechi ya final iwe moja kwasababu ya advantage ya mechi ya nyumbani al ahly walikataa na walijaribu mara moja ilikuwa al ahly na esperence de Tunis walifanya vurugu baada ya kufungwa ikabidi mechi ichezwe home and away.
 
Final(Mwisho) au tamati hivi kwa Afrika neno Hili limegeuzwa nyuma mbele mbele nyuma Why?kila kitu kwetu ni tatizo?

Leo Mada ingelikuwa Moja tu,ila kwa upuuzi wa CAF tunasubirishwa untill next week.

Shame on you
Sio Africa tuu hata kule south America mechi ni mbili

Pili iliwahi kuwa mechi moja ila waarabu wakaona haifai tukarudi kwenye mbili


NB: kila sehemu kuna kanuni zake sio lazima zifanane na ulaya

Mfano ubelgiji anayemaliza top kwenye ligi hawi bingwa moja kwa moja bali wanacheza mini tournament wale top 4 kupata bingwa

Sasa siku kina karia wakileta hiyo kanuni hapo si mtawatukana
 
Back
Top Bottom