Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 104
Mchezo wa michuano ya Klabu bingwa barani Afrika umepigwa hii leo katika Dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam ambapo Wekundu wa Msimbazi Simba alikua nyumbani akiikaribisha FC Platinum ya Zimbabwe ikiwa ni mchezo wa pili kati ya michezo miwili ya hatua ya mtoano.
Mechi hiyo ambayo ilipewa jina la kingereza ‘’WAR IN DAR’’ na wenyeji Simba imetoa maamuzi ya klabu ya Simba kuendelea kusonga mbele kwenye hatua ya makundi baada ya kuitandika Platinum bao 4 - 0.
Goli la kwanza la Simba limefungwa na E. Nyoni kunako dakika ya 39' kwa mkwaju wa penati na goli la pili likifungwa na S .Kapombe dakika ya 62' na goli la tatu likifungwa na J .Bocco dakika ya 90+1' na goli la kutamatisha likifungwa na C.Chama dk ya 90+5'.
Wachimba Platinum wa Zimbabwe waliingia katika mchezo huo wakiwa na faida ya goli 1-0 walilolipata katika mchezo wa kwanza uliopigwa katika Dimba la Taifa huko Zimbabwe majuma mawili yaliyopita.