Umewahi kujaza form yeyote kwenye tovuti? Wengi watasema ndiyo maana ata ku-login hapa JF lazima ujaze form yenye username na password.. Pale unapofanya hivi browser(Chrome, Edge, Opera) itakuomba ruhusa ya kukumbuka password na username, baadae utakapofungua ile website utaona username na password yako ziko pale kwenye form zikiwa highlighted kwa rangi ya njano.
Hivyo basi cookies hutumika na tovuti kukumbuka taarifa muhimu za watembeleaji wa tovuti husika iwe ni majina, passwords, shopping cart customization.