Butiku aionya CCM kuelekea uchaguzi 2015

Butiku aionya CCM kuelekea uchaguzi 2015

Mbona unakosa heshima wewe?Hivi unawezaje kumdharau mzee kama Butiku kwa kumwambia akalale kisa ameongea busara na maoni yake kuhusu mwelekeo wa siasa za CCM.Kwanini mnalewa kiasi hicho?Butiku penngine ni baba yako,hata pengine babu yako,lakini kwa kulewa sifa na posho za kifisadi uko radhi hata kumtukana au kumdhihaki kama ulivyofanya.Lakini sishangai,kuna mmoja wenu aliwahi hata kumdhihaki waziri mkuu mstaafu mzee jaji Warioba kwa kumwita mpumbav, kwenye radio moja hapa jijiini kisa tu baba anamadaraka makubwa.

Ndugu hela ni shetani haimjui baba wala mama sembuse mtu wa pembeni. Mwenye hela haangalii nyuma anatumia pesa kujihakikishia maisha bora kwake hapa duniani!
 
Wengi wa mashabiki wa CCM ni wazee ambao wanahofia kupoteza nafasi zao na ambao kwa sasa hawawezi kumudu kasi ya vijana; na pia wako vijana ambao wazazi wao ndio vigogo wa CCM na hivyo wanatarajia kurithishwa madaraka.

Pia vijana wengi wasio na ajira hudanganywa na kushawishiwa na pesa ndogo ndogo pale inapoonekana kuwa watasaidia kwenye baadhi ya malengo kama vile kampeni, na malengo yao yakishatimia husahauliwa hadi msimu mwingine.
 
Dhamani ya wazee kama akina Butiku sio kwa sababu ya swala nyeti lililoko mbele ya Watanzania la uwandikishwaji wa Katibu mpya' sio kwa kuwa si wanachama wa CCM Au CHADEMA la ni kwa sababu ya unyeti wao walioonesha katika majukumu yao walioonwsha ni katika kusikiliza maonu ya wananchi katika kuandika katiba. Hivyo inavyotokea mtu wa chama chochote akamdharau kiss ni kukiuka matakwa ya chama anachokiamini na kulemwea kwa wananchu ni tu kubwa lisilofutika. Mzee butiku na wenzake waliamini tusi Kubwa ni kukiuka maoni ya watanzania wapatao 44mill na isitoshe waliapa kuilinda na kusema kweli mapendekezo yao maoni yao. Pia waliapa kuilinda katiba ya Jamhuri wa Muungano kwa namna yoyote inayoweza kutokea has a ktk mazingira haya yanayojitokeza sasa. Leo wanapotoa maoni yao kuhusiana na kile walichokiona ktk kazi ngumu mnawaona ni wasaliti na walioishiwa mawazo yao kusiasa hatumaye na kutukanwa.
 
ccm ya butiku ilijali watanzania ,ya,sasa ni wanyang' anyi ,si ya wazalendo ,ni wabinafsi sana.Huwezi shusha elimu,huwezi dumisha rushwa,fukuza wananchi kisa mpango mji,kuwanyima umeme,kuruhusu mauaji ya polisi kwa raia ambao wanajumuika na kuandamana kama haki yao ,wewe unasema intelijensia inasema alshaba - abu!!?. Chama cha aina hii hakifai,Butiku ananukuu ya Horace Korimba!! ,ccm hakika imepoteza mwelekeo
 
....KWANINI bUTIKU ANATOA SIRI HIYO?
 
....KWANINI bUTIKU ANATOA SIRI HIYO?
Kwa sababu sera za ccm hazisaidii sasa mwananchi wa kawaida,
Pili,chama badala ya kuleta maendeleo wanayoyahitaji watanzania ,ccm inakusanya fedha nyingi na kuanzisha vyama vingi kupambana na chama chenye kuungwa mkono na wananchi wengi mfano Act na ADC,
Usalama wa taifa wamesoma mchezo,ccm wanaingizwa mkenge ili watakapogundua,watz watawafurusha kiulaini,maana watachoka kutii polisiccm huku ajira hakuna,umeme,maji na elimu duni,hakutakuwa na msalia mtume!!!!
 
Subiri mvua ya matusi kwa Mzee Butiku kutoka lumumba fc
 
ccm wamechoka wahenga walisema"kiburi c maungwana" na kiburi na dharau zao ztawaangamiza.
 
butiku+clip.jpg

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku

Na Exuper Kachenje, Mwananchi

Posted Julai19 2014 saa 10:20 AM Kwa ufupi
Butiku ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema kuwa iwapo chama hicho kitasahau kuwa kinaiongoza nchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi ambayo sasa Watanzania wanataka iandikwe upya na kuendelea kukumbatia maovu kinaweza kuondolewa madarakani.

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku amekionya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa kipo hatarini kupoteza madaraka katika uchaguzi mkuu ujao, iwapo kitafanya makosa na kuendekeza ubinafsi na utawala wa kiimla unaotokana na utamaduni wa rushwa na matumizi mabaya ya mali za umma.

Butiku ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema kuwa iwapo chama hicho kitasahau kuwa kinaiongoza nchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi ambayo sasa Watanzania wanataka iandikwe upya na kuendelea kukumbatia maovu kinaweza kuondolewa madarakani.

Alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam, Jumatano wiki hii katika mahojiano maalumu na gazeti hili ambapo alizungumzia mambo mbalimbali.

“…Kosa moja la msingi ni CCM kusahau misingi ya Katiba ya chama chao na Katiba ya nchi. Watanzania wengi wanaikubali Katiba ya CCM na Katiba ya nchi, lakini ambayo wanasema itazamwe upya, iandikwe Katiba Mpya,” alisema Butiku.

Huku akisisitiza, Butiku alisema:


Alifafanua kuwa hali hiyo itaikumba CCM kwa kuwa ndiyo kanuni ya maisha ya binadamu akisema:


“Vyama vyote tawala vilivyosahau masilahi ya wananchi wake, demokrasia, uhuru na haki, vikakumbatia uovu vinaanguka. Huo siyo utabiri wangu binafsi, bali historia itawahukumu.”

Butiku alitoa mfano akieleza: “Mfumo wa kibabe zaidi wa makaburu wa Afrika Kusini, uliangushwa na wasio na viatu. Nani anaweza kujenga ubabe wa sura kama ule wa makaburu, nani ataruhusu? Ni muhimu CCM nayo ijitazame.”


Rushwa

Alisema kuwa alipoondoka madarakani, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema taifa linanuka rushwa hali ambayo imeota mizizi hata sasa.

“…Leo rushwa ni kawaida, ni mfumo wa kuuza na kununua uongozi, kama taifa mkifika hapo ni hatari. Mkishanunua uongozi basi mmekwisha. Mkijenga mfumo huo, mnaondoa haki.

Ikiwa kura yako imekuwa biashara umekwisha, hakuna ushirikiano tena kati ya kiongozi aliyenunua nafasi na mwananchi. Hapo mnajenga kundi la viongozi la wafanyabiashara wa kura katika uchaguzi, mnajenga mfumo wa raia kuwa maskini.”

“Raia wakiuza haki yao na kununua hakutakuwa na taifa lenye utulivu. Wanunua kura wajue ni vita, siku moja wauza kura wataamua kuwaondoa nao watagoma kwa kuwa walinunua uongozi, hapo damu itamwagika, watu watauana.

Wanyonge hawapotezi haki ya unyonge wao, unaweza kuiangusha CCM…

 
hawa kina Butiku, Warioba, Salim, Nyerere Family etc si ndo walipaswa kutoka kabisa CCM ili kuonesha wako serious na wamechoka na kusema bila kusikilizwa???
 
Mbona unakosa heshima wewe?Hivi unawezaje kumdharau mzee kama Butiku kwa kumwambia akalale kisa ameongea busara na maoni yake kuhusu mwelekeo wa siasa za CCM.Kwanini mnalewa kiasi hicho?Butiku penngine ni baba yako,hata pengine babu yako,lakini kwa kulewa sifa na posho za kifisadi uko radhi hata kumtukana au kumdhihaki kama ulivyofanya.Lakini sishangai,kuna mmoja wenu aliwahi hata kumdhihaki waziri mkuu mstaafu mzee jaji Warioba kwa kumwita mpumbav, kwenye radio moja hapa jijiini kisa tu baba anamadaraka makubwa.

chezea buku 7 wewe wako tayari kuongea lolote mradi waingize siku pale lumumba
 
Utamaduni wa mwafrika hata siku 1,mtu mkubwa anaheshimiwa na kupewa hadhi take,
malezi yamekuwa ya hovyo Sana.Siku hizi mtoto anaweza hata kumkunjia Baba ngumi,hii nchi ina laana
 
Hawa ndo wanajua CCM ilipotoka sio kina nape
 
Mzungu yupo duniani kwa ajili ya kuongoza wajinga WAAFRIKA TU. Waafrika hatuwezi kujitawala wala hatuna akili hiyo.
 
Back
Top Bottom