Ina maana hakuna Mama Ntilie kwenye Kitimoto? Kwani nani anachinja Kitimoto? Mbona huko hamji juu?
Huu ni UPUUZI wa Pande zote mbili na Wassira kwa kushindwa ku-solve hili swala, nimemdharau mno na kusema kweli hafai hata kupelekwa Gombe maana hata huko ataharibu. Hili ni swala dogo na linaongeleka sana tu. Hakuna kutumia mabavu na kama kwenye Kitimoto hatulalamikiani kwa nini kwenye nyama tulalamikiane?
Pia inakuwaje kwamba Bucha za Waislaam zilianza kudoda? Si tunaambiwa kuwa nchi hii Waislaam ni wengi?
Narudia tena, WOTE NI WAPUUZI tu na vidini vyenu vya kuletwa na MELI.
ha ha haa sijui nikwambiaje kwanza nikuulize unajua maana ya islam chunguza kwanza ujue maana yake ndio ulinganishe na huo mwaka ulioandika kwanza Yesu (issa) hakuleta ukristo nitafutie andiko lolote kwenye biblia kwamba yesu ameleta ukristo
ha ha haa sijui nikwambiaje kwanza nikuulize unajua maana ya islam chunguza kwanza ujue maana yake ndio ulinganishe na huo mwaka ulioandika kwanza Yesu (issa) hakuleta ukristo nitafutie andiko lolote kwenye biblia kwamba yesu ameleta ukristo
Sawa sawa mkuu
naona baada ya kukatazwa ng'ombe wameamua kumchinja mchungaji hahaha
waislam bana ndio maana marekani na nchi za magharibi hawataki kusikia
kabisa hii kitu, waislam wa huko ulaya ni majina tuu ila hawana
itikadi.
jamani nimesema kati ya walioenda kununua nyama pale wengine wachoma mishikaki na mama ntilie ambao wanahudumia public,sasa hapa wapi huelewi?
Ni kama ambavyo waislamu wangenunua nyama ya ibada yao wakaenda kuchoma mishikaki na kuuza mahotelini.
MKUU
aha sasa nimewaza maana hapa wenzetu wanajifanya ushabiki wa imani ambayo ukichunguza sana hupati mantiki.
sasa kama swala ni imani ya kula kilichosaliwa na lazima awe muislamu ndio kachinja je hii ni kwa ng'ombe na mbuzi na kuku na kondoo na kanga tu au kwa kila chenye uhai? maana ndege na senene na pweza ,na samaki wanaovuliwa na wakristo na vinginevyo?
mimi nafikiri wakikaa sana na kujiuliza wanaweza wakabadili mitazamo yao
kwahiyo leo ndo mmejua mlikua mkila nyama kinyume na mafundisho yenu?.
Anyway,hulazimishwi ila ukitaka kufanya biashara ya nyamafu hakikisha hata kwenye mahoteli inapoenda unaweka tangazo ili wasiokula nyamafu wasije kununua sawa.maana usipofanya hivo na wakagundua umewalisha nyamafu lazima pataleta shida
Inabidi tuwe makini sana na hizi Redio na Televisheni za madhehebu ya dini kwani nazo zinachochea sana vurugu hii.
maandiko yako mengi lakini hata nikikuwekea hautaamini, utaanza kuleta sababu nyingine nyingi tu. hadi msahafu unautambua ukristo sembuse biblia? si zaidi sasa? jitahidi ufaham maana ya ukristo mkubwa.
kabla hujapewa aya toka kwenye biblia, soma kwanza hii
SURA 2. SURA AL- BAQARA 62. Hakika Walio amini, na Mayahudi na Wakristo, na Wasabai; yeyote atakaye
muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akatenda mema basi watapata malipwa
yao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
TAARIFA kutoka kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) zilizotumwa katika mitandao ya Kijamii na Bi Hellen Kijo bisimba mchana huu zinapasha kuwa kuzuka vurugu na kusababisha majeruhi huko Wilayani Chato.
Tumepokea taarifa za masikitiko kuhusu vurugu zilizotokea huko Buselele Chato kuhusu uchinjaji wa nyama unaobishaniwa na Waislam na Wakristo.
Chanzo cha Habari hizi kimetueleza kuwa baada ya mivutano kuhusu uchinjaji wa nyama.
Baaadhi ya Wakristo waliamua kuanzisha bucha ya ili wachinje na kununua hapo ili wasishiriki kula nyama zilizochinjwa kama sehemu ya ibada ya Kiislamu kwa vile uchinjaji kwa Waislam ni ibada.
Baada ya kufungua Bucha hiyo leo asubuhi taarifa inasema watu wanaosadikiwa kuwa waislam walifika kutaka kuifunga hiyo Bucha na baadaye Polisi nao walifika na walitaka wamchukue mwenye bucha hiyi.
Suala hili likazua tafrani na pakatokea mapigano kati ya pande mbili yaani waislam na wakristo na kuna watu wameumizwa.
Taarifa imezidi kueleza kuwa pia mali za aliyehamasisha ufungwaji wa bucha nazo zimeharibiwa.
Baada ya kupokea taarifa hii tumewatuma waangalizi wetu wa haki za binadamu kwenda kutuletea kwa kina hali halisi kama watakavyoweza.
Tunahabari kuwa kikosi cha kuzuia fujo kilifika na kutuliza hizo vurugu.Jambo tunaloliona kwa haraka ni kuwa kunaelekea kukosekana kwa uongozi wa kuyatazama masuala kama haya na kuyawekea msimamo na maelekezo kabla vurugu kama hizi kutokea.
Pili tunaona kuwa hali ya kukosa stahamala za kidini inajengeka nchini jambo ambalo ni hatari sana kwa usalama na amani hapa nchini.Wakati tunasubiri taarifa zaidi tunapenda kutoa angalizo kwa viongozi wetu maana tumesikia mkuu wa wilaya tayari ameshafika katika eneo la tukio.
Masuala kama haya yatazamwe kwa mujibu wa sheria na sheria zifuatwe lakini pia kwa kuzingatia haki za binadamu na hususani haki za kiraia na kiutamaduni ambazo zinatoa uhuru wa ibada na kila mtu asiingiliwe katika haki hizi.
Lakini pia njia za utatuzi wa migogoro ya aina hii isifanywe kijuujuuu bali pawe na nafasi yamaongezi ya kina ya uchambuzi wa kiini cha mgogoro.
Tutaweza kutoa taarifa zaidi tutakapopokea taarifa kutoka kwa waangalizi wetu wa kiini na matokeo ya mgogoro au vurugu hizi
Chanzo Juma Mtanda Blog
Kwani lazima ukale kwa huyo mama ntilie? Embu waislam tuache UJINGA, Kwa hili tunazidi kutia Aibu na tunaendelea kuonekana wa ajabu.