HIZI NI BUSARA ZILIZOTUKUKA
Na Kilawa the Iron
Hekima na busara za viongozi wa CHADEMA zinafanana sana na zile za mfalme Suleiman ambazo tumejifunza katika vitabu vitakatifu .
Pamoja na serikali yetu kuwanyanyasa wapinzani hawa kwa kuwakamata,hata kuwapiga wafuasi na viongozi wa chadema pia kuwafungulia kesi mbalimbali zisizo na kichwa wala miguu lakini wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha haki za wananchi zinapatika kwa wakati. Demokrasia inarudi mahali pake
Viongozi wa chadema walitangaza kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kupinga udikteta September mosi 2016,
operation hii ilipewa jina maarufu sana UKUTA lililoshika kasi kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vyote vya habari.
Mjini na vijijini kote wananchi walijiandaa kushiriki maandamano haya kama ilivyopangwa.
UKUTA yenye maana ya UMOJA WA KUPINGA UDIKTETA TANZANIA imekuwa na mafanikio makubwa hata kabla ya Tr 1September ,na hii imejidhihirisha pale watawala walipoamua kulinoa jeshi la polisi kumbana na viongozi wa chama,wafuasi na wapenda demokrasia wote.,tumeona matamko mbalimbali kutoka kwa wakuu wa nchi,wakuu wa jeshi la polisi n.k
Jeshi la polisi mikoani kote wameonekana wakifanya mazoezi ya haki ya juu kuliko ilivyo kawaida ,tena kwenye viwanja vya wazi na kwenye makazi ya watu,ilikuwa ni kawaida kusikia milindimo ya mabomu na risasi mitaani mithili ya nchi yenye mapigano.
Lakini pia kumekuwa na matamko mbalimbali kutoka kwa wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya mbalimbali.
Mfano mzuri ni pale RC Makonda alipojitokeza hadharani na kuikanyaga katiba kwa vitisho ambavyo kama wapinzani nao wasingekuwa na busara hakika usalama wa wananchi ingekuwa hatarini.
Kwakuwa watu walijipanga na walikuwa tayari kwa lolote na serikali ilijiandaa kutumia dola kudhibiti maandamano hayo kwa namna yoyote ,hakika wengi wetu tungepoteza maisha na kuacha familia zikihangaika ,lakini yote haya yangetokea kwa faida ya kizazi kijacho.
Busara za viongozi wa CHADEMA zimeonekana baada ya viongozi wa dini kupitia jumuia zao,viongozi wakuu waliostaafu,vituo vya haki za binadamu na mashirika yasiyo ya serikali yanayotetea haki za binadam kuwaomba kusitishs maandamano hayo ili waweze kuutatua mgogoro huo kwa njia ya mazungumzo ,kwa weledi mkubwa ,kwa fikra pana viongozi wa CHADEMA wameonesha busara zao zilizotukuka na kuwatuliza wafuasi wao na hakika swala hili limepokelewa na wanachama vizuri kabisa.
Wajinga watasema CHADEMA imeiogopa serikali,Welevu wataalewa umuhimu wa busara za viongozi hawa wa CHADEMA katika kuutatua mgogoro huu wa kisiasa ambao unaweza kuiyumbisha nchi yetu kiuchumi.
Hakuna asiyejua madhara yanayoweza kujitokeza kwenye mgogoro wa kisiasa na katika hili kamati kuu ya CHADEMA,wanapaswa kupongezwa kwa maamuzi haya mazuri na ya busara.
Ikumbukwe tr 1 September 2016 ni siku ambayo jeshi letu linaazimisha siku yao ,na wataazimisha kwa kufanya usafi hivyo kwa busara za viongozi wa CHADEMA jeshi letu litapata fursa ya kufanya usafi na kuadhimisha siku yao bila bugudha na naamin watatumia pia siku hiyo kumshauri Mh Rais kusikiliza kilio cha watanzania ,wanaomtaka aongoze nchi hii kwa kufuata katiba.
Busara hizi za viongozi wa CHADEMA ni kete nzuri sana kuwafanya wananchi kuelewa kwa undani UKUTA,kuielewa serikali yao kwa mapana,na kupembua kwa kina kujua undani wa ni nani kati ya serikali na upinzani wanaopenda Amani? Au wanaovuruga Amani
Busara hizi zinawapa fursa waumin wote wanaoamini katika maridhiano kutafuta haki au kutatua mgogoro wa kisiasa kutafakari kwa kina.
Ikiwa serikali itashindwa kuumaliza mgogoro huu kwa kukaa meza moja na upinzani basi wafuasi wa maandano yatakapotangazwa tena watakuwa wengi sana Mara tatu zaidi ya sasa
Nawahakikishia huu ni mwanzo mzuri wa safari ya safari ya kuisaka haki
Viva CHADEMA, Viva viongozi wote
Na Kilawa the Iron
Hekima na busara za viongozi wa CHADEMA zinafanana sana na zile za mfalme Suleiman ambazo tumejifunza katika vitabu vitakatifu .
Pamoja na serikali yetu kuwanyanyasa wapinzani hawa kwa kuwakamata,hata kuwapiga wafuasi na viongozi wa chadema pia kuwafungulia kesi mbalimbali zisizo na kichwa wala miguu lakini wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha haki za wananchi zinapatika kwa wakati. Demokrasia inarudi mahali pake
Viongozi wa chadema walitangaza kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kupinga udikteta September mosi 2016,
operation hii ilipewa jina maarufu sana UKUTA lililoshika kasi kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vyote vya habari.
Mjini na vijijini kote wananchi walijiandaa kushiriki maandamano haya kama ilivyopangwa.
UKUTA yenye maana ya UMOJA WA KUPINGA UDIKTETA TANZANIA imekuwa na mafanikio makubwa hata kabla ya Tr 1September ,na hii imejidhihirisha pale watawala walipoamua kulinoa jeshi la polisi kumbana na viongozi wa chama,wafuasi na wapenda demokrasia wote.,tumeona matamko mbalimbali kutoka kwa wakuu wa nchi,wakuu wa jeshi la polisi n.k
Jeshi la polisi mikoani kote wameonekana wakifanya mazoezi ya haki ya juu kuliko ilivyo kawaida ,tena kwenye viwanja vya wazi na kwenye makazi ya watu,ilikuwa ni kawaida kusikia milindimo ya mabomu na risasi mitaani mithili ya nchi yenye mapigano.
Lakini pia kumekuwa na matamko mbalimbali kutoka kwa wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya mbalimbali.
Mfano mzuri ni pale RC Makonda alipojitokeza hadharani na kuikanyaga katiba kwa vitisho ambavyo kama wapinzani nao wasingekuwa na busara hakika usalama wa wananchi ingekuwa hatarini.
Kwakuwa watu walijipanga na walikuwa tayari kwa lolote na serikali ilijiandaa kutumia dola kudhibiti maandamano hayo kwa namna yoyote ,hakika wengi wetu tungepoteza maisha na kuacha familia zikihangaika ,lakini yote haya yangetokea kwa faida ya kizazi kijacho.
Busara za viongozi wa CHADEMA zimeonekana baada ya viongozi wa dini kupitia jumuia zao,viongozi wakuu waliostaafu,vituo vya haki za binadamu na mashirika yasiyo ya serikali yanayotetea haki za binadam kuwaomba kusitishs maandamano hayo ili waweze kuutatua mgogoro huo kwa njia ya mazungumzo ,kwa weledi mkubwa ,kwa fikra pana viongozi wa CHADEMA wameonesha busara zao zilizotukuka na kuwatuliza wafuasi wao na hakika swala hili limepokelewa na wanachama vizuri kabisa.
Wajinga watasema CHADEMA imeiogopa serikali,Welevu wataalewa umuhimu wa busara za viongozi hawa wa CHADEMA katika kuutatua mgogoro huu wa kisiasa ambao unaweza kuiyumbisha nchi yetu kiuchumi.
Hakuna asiyejua madhara yanayoweza kujitokeza kwenye mgogoro wa kisiasa na katika hili kamati kuu ya CHADEMA,wanapaswa kupongezwa kwa maamuzi haya mazuri na ya busara.
Ikumbukwe tr 1 September 2016 ni siku ambayo jeshi letu linaazimisha siku yao ,na wataazimisha kwa kufanya usafi hivyo kwa busara za viongozi wa CHADEMA jeshi letu litapata fursa ya kufanya usafi na kuadhimisha siku yao bila bugudha na naamin watatumia pia siku hiyo kumshauri Mh Rais kusikiliza kilio cha watanzania ,wanaomtaka aongoze nchi hii kwa kufuata katiba.
Busara hizi za viongozi wa CHADEMA ni kete nzuri sana kuwafanya wananchi kuelewa kwa undani UKUTA,kuielewa serikali yao kwa mapana,na kupembua kwa kina kujua undani wa ni nani kati ya serikali na upinzani wanaopenda Amani? Au wanaovuruga Amani
Busara hizi zinawapa fursa waumin wote wanaoamini katika maridhiano kutafuta haki au kutatua mgogoro wa kisiasa kutafakari kwa kina.
Ikiwa serikali itashindwa kuumaliza mgogoro huu kwa kukaa meza moja na upinzani basi wafuasi wa maandano yatakapotangazwa tena watakuwa wengi sana Mara tatu zaidi ya sasa
Nawahakikishia huu ni mwanzo mzuri wa safari ya safari ya kuisaka haki
Viva CHADEMA, Viva viongozi wote