Bus la Maning nice linanyanyasa abiria

bora mmesema humu sitapanda hili basi tena. Sio rafiki wa watoto na jamii kumbe. Unazuia godoro mwanafunzi akalale wapi? Na ametoka mbali na nyumbani sababu ya pesa kidogo? Hivi wangelrihusu aende si ingekuwa social corporate responsibility?
 
bora mmesema humu sitapanda hili basi tena. Sio rafiki wa watoto na jamii kumbe. Unazuia godoro mwanafunzi akalale wapi? Na ametoka mbali na nyumbani sababu ya pesa kidogo? Hivi wangelrihusu aende si ingekuwa social corporate responsibility?
Naunga mkono hoja, ikitokea nasafiri njia ambayo hilo basi linafanya safari zake silipandi
 
Na nyie abiria wengine (mleta uzi ukiwa mmoja wao) mlichukua hatua gani kuzuia unyanyasaji huo? Maamuzi ya kuikalia kimya dhuluma ni sehemu ya ushiriki wako. Ni wakati sasa watanzania tusimame na kujitetea/kuteteana, imagine binti mdogo wa shule anapambana na wanaume wanne halafu kuna mwanaume na misuli yake au mwanamke na nguvu zake amekaa tu anasubiri afike nyumbani awasimulie majirani wasikitike na kuhuzunika
 
Nadhani hao wajinga( Kondakta) wanajisahau kuwa huu ni utawala wa mama..utawala wa kunyanyasa watu na kuwaita wanyonge ulikwisha..
 
Na nyie abiria wengine (mleta uzi ukiwa mmoja wao) mlichukua hatua gani kuzuia unyanyasaji huo? Maamuzi ya kuikalia kimya dhuluma ni sehemu ya ushiriki wako. Ni wakati sasa watanzania tusimame na kujitetea/kuteteana, imagine binti mdogo wa shule anapambana na wanaume wanne halafu kuna mwanaume na misuli yake au mwanamke na nguvu zake amekaa tu anasubiri afike nyumbani awasimulie majirani wasikitike na kuhuzunika
Mimi kama mpita njia nilijaribu kupiga picha tiketi ya huyo mwanafunzi na kuituma kwa trafiki kibaha na pia kutoa taarifa kwa afisa wa LATRA Morogoro 0738 000 054

Sent from my SM-N920S using JamiiForums mobile app
 
Hapohapo Kibaha kuna Ofisi za chama cha Kutetea Abiria CHAKUA
amuone mtu mmoja anaitwa Hassan Mchanjama, hilo Bus la Manning litashughlikiwa na Godoro mwenye Kampuni atalipia Traffic au Mahakamani
Pole yake huyo Mwanangu, kwel tunasomesha kwa shida halafu wale waliotoroka darasani wanakuja kulipiza kisasi tena wanaume wa4?
Kwelikabisa wakatoe taarifa mapema atasaidiwa bila ya shida kabisa.
 
Hapohapo Kibaha kuna Ofisi za chama cha Kutetea Abiria CHAKUA
amuone mtu mmoja anaitwa Hassan Mchanjama, hilo Bus la Manning litashughlikiwa na Godoro mwenye Kampuni atalipia Traffic au Mahakamani
Pole yake huyo Mwanangu, kwel tunasomesha kwa shida halafu wale waliotoroka darasani wanakuja kulipiza kisasi tena wanaume wa4?
Statement yako ya mwisho imenichekesha na kunipa mawazo.
 
Bei ya elfu kumi kwa ilo godoro ni sahihi labda tu uyu mwanafunzi akuambiwa bei mapema.
Sitakaa nije nitetee mbwa hao, makondakta nimekumbana nao katika mazingira tofauti tofauti wakaninyanyasa sana

Tukio la huyo dada naliona kama copy and paste kasoro install tu na nilichofanyiwa mwaka jana kwenye gari ya mkulima.

Makondakta idadi hiyohiyo (midume kama mimi) yaling'ang'ania betri yangu ya sola eti yakaondoka nayo kisa yanadai nauli na mimi kwa hasira nikayaacha yakazunguka nayo siku tatu ndipo siku nipo kwenye mambo yangu nikaiona gari nikaifwata nikaichukua betri yangu bureeee.

Nilifurahi lakini nilichukia kidogo kwakuwa nilichokuwa nimedhamiria ni betri ipotee nikawashtaki niwasumbue kidogo

Basi mpaka leo siwapendi hao jamaa halafu nakutana nao bado japo wenyewe wamenisahau ila mimi nawakumbuka na nategea siku mmojawapo ajiingize kwenye anga zangu au ajilete ana shida fulani ndo atajua hajui

Mtu anaweza akasema mimi mgumu au sijui nini lakini sivyo ngoja nirewind hii stori utaelewa. Nilinunua vitu kadhaa wabebaji wakapakia kwenye keriya juu huko nikaongea na huyo mkuu wao nikamuorodheshea vitu nilivyonavyo akasema nilipe elfu 10 nikalipa

Kisha nikachukua kimzigo changu kingine na betri nikaingia nayo ndani sasa pale wakawa wananizuia wanasema ikapandishwe juu nikalazimisha nikaingia navyo. Wakasumbua sana mule ndani wanasema betri ni kitu hatari hivyo huwa wanashika hela kubwa nilipe elfu 15 nyingine kwajili ya betri tu ikabidi nimuite yule mkuu wao akawaambia waniache elfu kumi niliyolipa inatosha

Basi wakaambiana sawa, sawa kumbe vile wamekonyezana. Yule bwana akanipa namba yake akasema nimpigie kwa lolote (aliwaelewa mapema). Basi kufika nishuke sasa ndipo hapo utata ulipoanzia

Nilimpigia yule jamaa akaniambia hiyo betri wataacha ofisini nikachukue hawakuacha wakarudi nayo Dar ndipo nikaamua kuwaacha wazurure nayo. Sijui aliwachukulia hatua gani lakini alionesha kukasirika sana wale wajamaa kumdharau na akasema lazima awashughulikie
 
Mabasi ya kusini yana upumbavu mwingi sana.....yaani ukiweka hata kibox kwenye gari wanataka ulipie cha ajabu anayedai hiyo nauli ni kondakta lakini kwenye kukata tiketi huulizwi kuhusu mizigo.......hao ni MATAPELI.....

Hii niliishuhudia Tashrif bus na Maning nice
 
Hiyo njia bus langu ni Baraka classic huwezi nitoa wana mabasi mazuri siti nzuri na wasikivu kwa abiria
 
Hawa mabwana Ni wasumbufu Sana nilifikiri Ni Mimi kumbe Kuna wengi wametatizwa nao. Niliapa sitapanda Wala kutuma mzigo wangu kwao kwa usumbufu nilioupata. Hivi mmiliki Ni Mwenye asili ya Somali?
 
Leo nimeshuhudia mtafaruku kati ya watumishi wa BUS LA MANING NICE na abiria wa kike ambaye ni mwanafunzi aliyesafiri kutokea Lindi kuja Kibaha. Ameshuka na makondakta wakamshushia begi na godoro la futi 3, wakamdai alipie godoro elfu30. Mwanafunzi akapigwa butwaa kwani anadai godoro huwa analipia elfu3. Basi akaambiwa alipie elfu10, yeye akawa na elfu5. Kilichofuatia ni purukushani ya kumnyang'anya godoro huyo msichana na kuondoka nalo kuelekea morogoro ambako ndio kituo cha mwisho cha bus hilo la maning nice. Kilichotushangaza wengi ni bus hilo kuwa na wanaume 4 ambao wote wanajiita ni makondakta kunyang'nyana godoro na mwanafunzi wa shule. Nawasifu bodaboda waliingilia huo mgogoro kwa kuona wazi kuwa hiyo gharama haikuwa fair ila godoro lilishatupwa kwenye booth na booth kufungwa kwa hiyo haikuwezekana kupata godoro na bus likaondoka japo abiria waliokuwa ndani walipaza kelele kulaani kitendo hicho cha makondakta. Mwanafunzi alipohojiwa alibainisha kuwa alikata tiketi mapema sana tangu tarehe 8 Desemba na aliwapa taarifa kuwa ana begi moja na godoro, mkata tiketi akamshauri alete begi na godoro jana jioni tarehe 10 Desemba na hakuambiwa kuwa godoro atalipia kiasi gani hadi leo aliposhuka kwenye bus kibaha ndio akapewa hiyo "Suprize" ya kufunga mwaka. Mwanafunzi akaishia kulia na kufajiriwa na madereva wa bodaboda hadi ndugu yake alipofika kumpokea kama dk15 baadae.

Picha ya wanaume 4 wanamnyang'anya godoro mtoto wa shule imenisikitisha sana ila bahati mbaya mfukoni nilikuwa na elfu2 tu na hao makondakta kwa lugha waliyokuwa wanatumia nilishindwa kuwaomba wapokee elfu2 ili wampe huyo mtoto kagodoro kake. Na lugha waliyokuwa wanatumia ilikuwa sio ya kistaarabu na matusi ya nguoni. Kiukweli imeniuma sana kushuhudia unyama huu ulivyofanyika na napata wasiwasi kuwa mwenye kampuni anaweza kujua haya mambo ambayo yanaweza kuharibu sifa za kampuni ya wakati huu ambao ushindani ni muhimu na customer care ndio dira. Kama anayoelezea huyu mtoto ni sahihi basi nilitegemea mteja alipie mizigo inayotakiwa kulipia anapopakia mizigo na kupewa risiti halali ya malipo ya mizigo labda na luggage tag ambayo kopi yake inaambatanishwa kwenye tiketi ya abiria kwa ajili ya utambulisho. Kwa namna wanavyoendesha mambo walikuwa na uwezo wa kumdai mwanafunzi huyu hata laki1 kwa godoro la elfu50!! Hii ni kama blackmail kwa kweli. Labda hainihusu, ila bus moja linakuwaje na makondakta 4, wanalipwaje mishahara? Nadhani hii inasababisha "wajiongeze" jinsi ya kupata mshahara!!

Nini maoni yako kuhusu kitendo kilichofanywa na watumishi wa bus la kampuni hii kwa mtoto huyu? Huyu mwanafunzi angeweza kusaidiwa "customer watchdog" ipi kama ipo??
Nilichoweza kumsaidia mwanafunzi huyu ni kupiga picha ya ticket hii na kumpa elfu2 niliyokuwa nayo imsaidie kwenye ngwe ya safari iliyobakia kufika nyumbani kwao.
Lakini pia nadhani taarifa hii itawasaidia abiria wengine kujihadhari na kutumia usafiri wa kampuni hii ya MANING NICE kwani uthubutu wa matendo ya hao makondakta ni ushahidi kuwa management ya kampuni ni mbovu sana, haya ni mawazo yangu. Kama taarifa hii itawaokoa wahanga "watarajiwa" nitajisikia nimeutendea haki umma. Ila pia naomba mamlaka husika wafuatilie huduma za kampuni hii ili kupunguza adha wanazopata abiria. Lakini pia iwe taratibu kumtaarifu abiria gharama ya mizigo kabla ya safari ili abiria awe na uhuru wa maamuzi. Hapa hapa pia naomba mamlaka husika iweke rasmi muda wa buses kusimama kwa ajili ya kula. Hivi karibuni nilishuhudia abiria wa bus la Arusha wakipewa dk 10 kwa huduma ya chakula. Hadi mtu wa mwisho anashuka kutoka kwenye bus zilishaisha dk4, niliona kama haikuwa fair kwa huyu abiria wa mwisho aliyekuwa na watoto mapacha, daaah!! God bless Tanzania.View attachment 2040736
Poleni.

Login • Instagram
 
Back
Top Bottom