Burudani kutoka kwa mlinzi wa W. Ruto

Burudani kutoka kwa mlinzi wa W. Ruto

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2017
Posts
10,687
Reaction score
19,444
Kwa wale waliopata fursa ya kuangalia utoaji zawadi baada ya mechi ya fainali ya CECAFA Senior Challenge Cup kati ya Kenya na Zanzibar ambapo mgeni rasmi alikua Makamu wa Rais wa Kenya Bwana W. Ruto watakua walimuona jamaa mmoja mwenye umbo la wastan, rangi ya kung`aa alieanza kwa kusimama jukwaa la kutolea zawadi sambamba na wageni wa waalikwa akiwa mtu wa tatu upande wa kulia wa Ruto. Jamaa alikua akiwasalimia kwa uchangamfu na bashasha sana wachezaji wa Kenya walipokua wakipita kuchukua medali zao huku wengine akiwakumbatia kwa kuwarukia

Kumbe jamaa alikua ni katika team ya ulinzi wa makamu wa Rais na alikua akionekana katika positions tofauti karibu na alipokua Ruto na kwa ujanja wa hali ya juu pale ambapo watu walimkaribia sana kiongozi huyo alikua anachukua jukumu la kuwasogeza pembeni kwa staili ya aina yake kana kwamba alikua katika washangiliaji ama kiongozi tu wa soka wa Kenya! pia alikua mara kwa mara akiwasiliana na wale walinzi waliovaa suti za kawaida za walinzi wa viongozi ambao walikua mbali kidogo na jukwaa huku yeye akionekana kuwapa instructions mbalimbali na nadhani ndie alikua kiongozi wa team ya ulinzi(sina hakika maana sina taaluma hiyo). Na hata Ruto alipokua anaondoka uwanjani yeye ndie alimcover very closely na wakaondoka in a very stylish way!

Ninachotaka kusema ambacho kilinifurahisha ni kwamba ulinzi ule ulikua kama an art. Ni sanaa flani ambapo pamoja nakuhakikisha ulinzi kwa kiongozi wa nchi lakini kazi hiyo ilifanyika bila kutisha watu kwa kukunja sura, kuwabugudhi na kuwasukasuka na pia kama vile wanatoa burudani flani hivi ikiwa utawashtukia kama ni walinzi! You will like them. Bahati mbaya sina ujuzi wa kuweka video clip humu ningefanya hivyo, kama kuna mtu anaweza anisaidie pls. Na natamani kama ningekua naangalia walinzi wa viongozi wetu hapa nchini nao wakifanya hivo lakini najua inawezekana kila nchi na taratibu zake
 
mie nilimuona wa mwisho kabisa alikuwa anawa hug kwa furaha sana (hug ya kihuni flani) nilifurahi sana

huyo mlinzi sikumuona, ungeweka video ingekuwa bora zaidi
 
Ni kweli mkuu usemalo jamaa alikuwa miongoni mwa Watu waliokuwa ndani ya Detail ya W.Ruto japo hakuwa leader, Unajua Swala la ulinzi haliko static wala huwezi kucopy style fulani mtu analindwa au kuwa closer na walinzi kutegemea Threat ya Eneo, Kuna kila namna Hawa VP Protecter Kuwapa Uhuru Fulani wanaowalinda protectees ili kutoharibu taswira ya audiences, marekani kutokana Tech wao hawako too close na Rais wao muda mwingi unamuona yuko kama alone ivi,japo Wanamfatilia tena wengi tu, Kwanini nimeandika haya Rais wetu Anakuwa attached na Walinzi wengi mpaka anapoteza mvuto mbele ya kamera sioni umuhimu wa ADC kuwa nyuma mkuu vile Adc ni mpambe pis jpm minimum ni walinzi watatu wanakuwa closer nae yani muda wote JPM hajawahi kuhang alone ivi na details yake Walau isionekane, Juzi Dodoma 9 Dec mpaka kwenye jukwaa kuu mpaka Gwaride alikagua akiwa na mlinzi wake wakati pale alipaswa awe na CDF tu
 
mie nilimuona wa mwisho kabisa alikuwa anawa hug kwa furaha sana (hug ya kihuni flani) nilifurahi sana

huyo mlinzi sikumuona, ungeweka video ingekuwa bora zaidi
Zipompa huyohuyo ndie mlinzi ninaemzungumzia, kama una access ya kuangalia tena video hiyo irudie na umfatilie huyo jamaa aliekua anawa hug wachezaji wa Kenya, utaona yoote aliyokua anafanya ...kuwasiliana na walinzi wenzie, kum cover Ruto kwa kuhakikisha watu hawamsogelei sana,kutoa instructions mabalimbali lakini bila kua noticed, angalia Ruto alipokua anatoka uwanjani utaona ile cover yake si ya kawaida. He was very professional
 
Ni kweli mkuu usemalo jamaa alikuwa miongoni mwa Watu waliokuwa ndani ya Detail ya W.Ruto japo hakuwa leader, Unajua Swala la ulinzi haliko static wala huwezi kucopy style fulani mtu analindwa au kuwa closer na walinzi kutegemea Threat ya Eneo, Kuna kila namna Hawa VP Protecter Kuwapa Uhuru Fulani wanaowalinda protectees ili kutoharibu taswira ya audiences, marekani kutokana Tech wao hawako too close na Rais wao muda mwingi unamuona yuko kama alone ivi,japo Wanamfatilia tena wengi tu, Kwanini nimeandika haya Rais wetu Anakuwa attached na Walinzi wengi mpaka anapoteza mvuto mbele ya kamera sioni umuhimu wa ADC kuwa nyuma mkuu vile Adc ni mpambe pis jpm minimum ni walinzi watatu wanakuwa closer nae yani muda wote JPM hajawahi kuhang alone ivi na details yake Walau isionekane, Juzi Dodoma 9 Dec mpaka kwenye jukwaa kuu
Thanks Mkuu, umenipa shule
 
Back
Top Bottom