Nashukuru nimempata mdada kupitia jukwaa hili wa kuniuzia kiduka changu cha nguo na mambo yanaenda vizuri. Karibuni kijitonyama mumuchangie,
leo nina wazo hili.
Kulingana na kuwa na majukumu binafisi,
Nitatoa million mbili kwa kijana yeyote wa kitamzania ambaye atakuwa tayari kubuni biashara au kutafuta fursa au office ya aina yeyote harali.
Hiyo biashara itakuwa yangu yeye atakuwa kama nimemwajiri japo atakuwa amebuni na kuanzisha biashara hiyo.
Leseni nitamchukulia mimi TRA,
Location au eneo au frem ya biashara atatafuta mwenyewe ila nitaiilipia mimi na mumiliki wa nyumba au Frem hizo atanitambua mimi kama mkodishiwa,
Biashara isiwe mobile (easy to be moved).
Bizaa tutaenda kununua wote hadi hapo tutakapoaminiana,
Mauzo ya kila siku yatawasilishwa kwa namna tukavyopatana,
Eneo la biashara ni sehem yeyote mkoa wa Dsm au mkoa wa Pwani.
Awe na umri unaotakiwa kisheria kuajiriwa,
Awe tayari kunipeleka kwa kwa ndugu au mtu anaetambulika.
Atatakiwa kwenda naye mahakamani kwa ajili ya kuapa akiwa na vizibitisho (dhamana) inaweza ikawa barua, vyeti na picha n.k... Hii itasaidia siku akikimbia nikimkamata niweze kumuadhibu kisheria na kihaki.
Jinsia yeyote na Elimu yeyote,
Asiwe mkubwa saana hadi nikawa namuogopa kusaidiana katika kukuza biashara yetu. (umri wa kati tu).
Sihitaji business plan nahitaji wazo lako tu, mfano sema nitafungua Grocery sehem flan au nitafungua stationary sehem flan nk. Na mimi nitapima wazo lako nikilikubali ndo tutaanzia hapo.
awe mwaminifu.