Naangalia bunge sasa hivi..Selukamba kasimama na kuomba radhi kwa maneno aliyotoa mchana.
Wenje nae kaomba muongozo kwa Ndugai..akirejea agizo la Makinda jana kwamba mbunge yoyote atakayetukana atatatolewa nje na polisi. Na anasema Selukamba katoa tusi kubwa kuliko matusi yote yaliyowahi kutolewa bungeni.
Ni matusi gani Selukamba katukana..mliosikia tafadhali mtujuze.
CCM wamejisahau sana kwa wingi wao Bungeni,lakini ikumbukwe,Daudi alimuua Goliati.Tuombe tu uzima haya yana mwisho.Leo ni moja ya siku ambazo nimekereka sana
mh bahati mbaya wapi mtu akishazoea matusi hutukana ovyoovyo
lakini ustaarabu ukiwa nao kamwe huwezi kutukana kwa bahati mbaya kwa sababu hata tusi kuelea kichwani kwako haiwezekani.
Tatizo la kulala Chako ni Chako kula bia na kuku ambao hawajaiva!! Mkiamka asubuhi bado mmevimbiwa kuku na pombe kichwani halafu badala ya kujadili mambo ya kitaifa mnaporomosha matusi. Aibu hii haitawatoka hawa wabunge!! Mtu mzima hovyo sana.
Ukizowea kujamba ukiwa pekee yako, huja siku ukasahau ukajamba mbele ya kadamnasi. Fundisho ni kuwa private na public lives zina tabia ya kuambukizana.
Bongo mtu anaiba mapesa ya epa akishakiri aliiba anaambiwa tulia hutotangazwa na hakuna hukumu we rudisha tu chini chini na taifa zima likakubaliana na hali hiyo. Je uzito wa tusi unaweza piku hii mpaka waadhibiwe? labda serikali nyingine sio hiii tunayoiona.