Tunakutegemea Mkuu! Tujuze yanayojiri. Updates Pls!
Werema na Wasira ni vilaza.Wanabodi wenye access na TBC, angalieni TBC Live kipindi cha Jambo Tanzania. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Warema na Waziri Stephen Wasira, wanahojiwa live kuhusu kuwasilishwa Muswada wa Sheria wa Kuundwa Tume ya Kukusanya Maoni ya Kubadilisha Katiba.
Kinachoendelea ni utumbo mkuu, tusubiri mchana kwenye mjadala wa mswaada wa katiba tutajuzana kila hatua. Ila kwasasa nitakuwa na weka maji kwenye gunia kama alivyosema member mmoja hapo juu kuwa maswali ni yale yale na majibu yale yale.
Huyu ni Mwanasheria Mkuu wa ajabu sana. Yaani hawa wote wanaopinga ni wajinga isipokuwa wao tu ndio wapo sahihi? Shivji, Kanywanyi, TLS, Jukwaa la Katiba, na wananchi wengine wote hawajui wanachokipinga?
Mimi nafikiri hatua iliyobaki ni moja, nayo ni wanaharakati wote na vyama vya upinzani kuibuka na mchakato sambamba na ule wa serikali ambao hawa bwana wamekamia kuupitisha wiki hii. Kisha kukusanya maoni sambamba na hiyo tume ya kwao na kuibuka na rasimu ya katiba mbadala. Itakapofika wakati wa kura ya maoni, ifanyike kampeni ya kura ya 'HAPANA' dhidi ya kura ya 'NDIYO' ya serikali.
Mkuu Avatar yako nimeipenda. Huenda.Hivi kweli Prof. Shivji na Kanywanyi hawajui muswada huu unahusu nini? au Werema na huyo Tayson wameamua kuwaponda hadharani wanataaluma hao?
Hadi sasa huu muswada ni wa kurekebisha katiba na sio kwa kutunga katiba mpya. Kwa Werema kuutetea ni sawa kabisa maana tangu hapo awali alisema waziwazi kuwa katiba ya sasa haina shida kama kuna jambo la kurekebisha basi watu waseme na litarekebishwa. Maneno haya ya Werema pia yalisemwa na Celina Kombani.
Kwa hiyo Serikali ya ccm haina nia ya kuandika katiba mpya - that's very obvious. Kama walikuwa na nia ya kuandika katiba mpya kwa nini hawataki kusikiliza maoni ya wananchi? Ni kitu gani kinawafanya watake kusoma huu muswada kwa mara ya pili? Ni ni lini muswada wa KUTUNGA katiba mpya uliwahi kupelekwa bungeni? Ule mwingine ulipelekwa tena kwa lugha ya kiingereza ulikuwa wa KUREKEBISHA katiba.
Naye Steven Wasira na utaalam gani kwenye mambo ya katiba kiasi kwamba ccm wanamtumia kuhubiri huu muswada uliojaa matatizo? Kwa nini watu kama Wasira na Werema wanajiona wanajua mambo ya katiba kuliko Prof Shivji? Shida kubwa ninayoona ni kwamba kuna gap kubwa sana kati ya ccm na wananchi. Wakishapata Ubunge hawa ccm ni kama wanajigeuza baraza la mawaziri tena mawaziri wasiosikiliza wale wanaowaongoza. Huu muswada unaweza kuipeleka kuzima ccm mapema kuliko ilivyokuwa iwe.
Ningeomba kuuliza, Spika wa bunge ana uwezo/nguvu gani katika hali kama hii ambapo serikali inaonekana waziwazi kwenda kinyume na public interest?
Huyu ni Mwanasheria Mkuu wa ajabu sana. Yaani hawa wote wanaopinga ni wajinga isipokuwa wao tu ndio wapo sahihi? Shivji, Kanywanyi, TLS, Jukwaa la Katiba, na wananchi wengine wote hawajui wanachokipinga?
Mimi nafikiri hatua iliyobaki ni moja, nayo ni wanaharakati wote na vyama vya upinzani kuibuka na mchakato sambamba na ule wa serikali ambao hawa bwana wamekamia kuupitisha wiki hii. Kisha kukusanya maoni sambamba na hiyo tume ya kwao na kuibuka na rasimu ya katiba mbadala. Itakapofika wakati wa kura ya maoni, ifanyike kampeni ya kura ya 'HAPANA' dhidi ya kura ya 'NDIYO' ya serikali.
Jamani naomba mnisaidie, mswada ukisomwa kwa mara ya kwanza au ya pili, what are the effects
Jamani naomba mnisaidie, mswada ukisomwa kwa mara ya kwanza au ya pili, what are the effects
tupe link yakucheki hiyo tbc via internetnenda sikiliza bunge live kupitia TBC Taifa kwenye internet live bila chenga