Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Nimefuatilia,nimesikia na kujua kinachoendelea Bunge Maalum la Katiba. Pamoja na kujua kwangu,bado nina swali kwa watanzania wenzangu: Bunge hilo linajadili Rasimu ipi? Iko wazi kuwa Rasimu ya Tume ya Katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Sinde Warioba inabeba mapendekezo ya Serikali tatu.
Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zinazoliongoza Bunge hilo, Bunge Maalum linapaswa kujadili na kuipitisha Rasimu ya Tume ya Warioba. Hakuna la zaidi. Ilidhaniwa kuwa Wajumbe wangejadili serikali tatu tu na kuona uimara na udhaifu wa mapendekezo hayo. Halafu,kura zingepigwa.Kama mapendekezo yangepita;yangebaki kama yalivyo.Yangekataliwa,pangefunguliwa milango ya mapendekezo mengineyo katika kuirekebisha na kuiboresha Rasimu husika.Na kura ingefuatia.
Lakini,mambo yamekuwa kinyume.Tangu mwanzo,Rasimu inajadiliwa kana kwamba kuwa mapendekezo-chaguo ya serikali tatu au serikali mbili. Kuchanganya hoja za serikali tatu na mbili pamoja hakuwezi kutupa Katiba. Kufanya hivi kutakwamisha namna ya kupiga kura za kupitisha mapendekezo. Wajumbe wataulizwaje?
Ifike mahali,Bunge Maalum litumie Sheria zake na hekima katika jambo hili. Kama limeshindwa,liseme na kila mmoja arudi kwao. Mchafukoge uliopo juu ya Bunge Maalum kwasasa si mzuri na ni wa hatari. Wananchi wanaweza kuandika Katiba yao nje ya utaratibu na kuifuata.Yaweza kuwa hata mioyoni mwao tu.Ikitokea hivyo,Katiba inayoandikwa Bungeni haitafuatwa na kuheshimiwa.Nchi itakuwa kwenye hali gani?
cc Mchambuzi Yericko Nyerere Ngekewa FaizaFoxy Mamndenyi Chris Lukosi zumbemkuu Dingswayo Ben Saanane na wengineo karibuni tujadili
Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zinazoliongoza Bunge hilo, Bunge Maalum linapaswa kujadili na kuipitisha Rasimu ya Tume ya Warioba. Hakuna la zaidi. Ilidhaniwa kuwa Wajumbe wangejadili serikali tatu tu na kuona uimara na udhaifu wa mapendekezo hayo. Halafu,kura zingepigwa.Kama mapendekezo yangepita;yangebaki kama yalivyo.Yangekataliwa,pangefunguliwa milango ya mapendekezo mengineyo katika kuirekebisha na kuiboresha Rasimu husika.Na kura ingefuatia.
Lakini,mambo yamekuwa kinyume.Tangu mwanzo,Rasimu inajadiliwa kana kwamba kuwa mapendekezo-chaguo ya serikali tatu au serikali mbili. Kuchanganya hoja za serikali tatu na mbili pamoja hakuwezi kutupa Katiba. Kufanya hivi kutakwamisha namna ya kupiga kura za kupitisha mapendekezo. Wajumbe wataulizwaje?
Ifike mahali,Bunge Maalum litumie Sheria zake na hekima katika jambo hili. Kama limeshindwa,liseme na kila mmoja arudi kwao. Mchafukoge uliopo juu ya Bunge Maalum kwasasa si mzuri na ni wa hatari. Wananchi wanaweza kuandika Katiba yao nje ya utaratibu na kuifuata.Yaweza kuwa hata mioyoni mwao tu.Ikitokea hivyo,Katiba inayoandikwa Bungeni haitafuatwa na kuheshimiwa.Nchi itakuwa kwenye hali gani?
cc Mchambuzi Yericko Nyerere Ngekewa FaizaFoxy Mamndenyi Chris Lukosi zumbemkuu Dingswayo Ben Saanane na wengineo karibuni tujadili