Bunge live 'limeanza'!

Bunge live 'limeanza'!

Jamaa umeona umetoa bonge hoja mwenyewe...
 
Serikali haijakataza bunge kuoneshwa live huu ni upotoshaji tu.

Serikali imejitoa kuonesha bunge live kupitia shirika lake la utangazaji TBC kwa sababu ilizozitoa.

Aliyezuia vikao vya bunge kuoneshwa live kwa vyombo binafsi ni bunge lenyewe baada ya TBC kujitoa kurusha matangazo hayo.

Kwa hiyo kulaumu serikali hasa rais kwa maamuzi ya mhimili mwingine ni upumbavu tu,rais alaumiwe kwa kujitoa kwa TBC basi lakini hata akiamua TBC irudishe utaratibu wa zamani wakuonesha live,uongozi wa bunge tayari umezuia kamera yoyote kuingizwa kwenye ukumbi wa bunge kwa ajili ya kurusha live.

Haya yote yanatokea sababu hatuna upinzani imara nchi hii.
 
Kichwa cha habari na yaliyomo tofauti kabisa.ccm bwana ni shida.sasa kijana kama huyu usikute kule ccm ndo msomi kuliko wengine.
 
Watanzania watu wa ajabu sana! Humu JF zinapigwa kelele nyingi kuhusu uamuzi wa Serikali kusitisha kuonyesha Bunge live. Watu wanadai wananyinwa haki yao ya kupata habari toka Bungeni. Cha kushangaza ni kwamba wanaolalamikia kupata yanayojiri Bungeni ndio hao wanatuletea habarI 'motomoto' za Bungeni.

Kwa maana nyingine Serikali iko sahihi si lazima Bunge lionyeshwe live ili watu wapate habari muhimu! Wapo wanaoshupaa kabisa na kudai kwamba Watanzania wengi wanataka kuona Bunge live kwahiyo 'wengi wape'.

Ni wengi wapi hao? Tanzania imejaa maskini ambao hats mlo mmoja kwa siku kuupata niv shida. Hivi ni kweli wengi hawa, maskini wa Tanzania wanataka Serikali yao ionyeshe tv live badala kuwakwamua kwenye umaskini wao?

Ifike mahali 'sisi' Watanzania wachache wenye uwezo tuwafikirie na Watanzania wenzetu walio wengi ambao wanaihitaji sana hiyo fedha ambayo Serikali inadhamiria kuokoa kutoka matangazo live. Na wao wana haki pia!

Pengine Serikali ya HAPA KAZI TU ingetutangazia kwamba hakuna kuonyesha Bunge live ili waangaliaji wote wachape KAZI maana ni muda wa kazi kwa Watanzania wote Wakulima na Wafanyakazi!
Yaan ilibidi watanzania wote tuwepo pale bungeni, tushiriki moja kwa moja, tuulize maswali, tusikilize hoja na kupitisha baadhi ya mambo sasa kwa kuwa hilo haliwezekani ndio maana tumechagua wawakilishi wakawasilishe matakwa yetu. Sasa kama kushiriki moja kwa moja imeshindikana basi tuna haki ya angalau kuona uwakilishwaji wetu huko bungeni. Tuone live bila kuchuja chochote kama hilo limeshindikana basi waongeze ukubwa wa bunge ili watanzania wote zaidi ya milion 45 tukutane pale bungeni
 
Back
Top Bottom