Mbulula + kiaziWatanzania watu wa ajabu sana! Humu JF zinapigwa kelele nyingi kuhusu uamuzi wa Serikali kusitisha kuonyesha Bunge live. Watu wanadai wananyinwa haki yao ya kupata habari toka Bungeni. Cha kushangaza ni kwamba wanaolalamikia kupata yanayojiri Bungeni ndio hao wanatuletea habarI 'motomoto' za Bungeni.
Kwa maana nyingine Serikali iko sahihi si lazima Bunge lionyeshwe live ili watu wapate habari muhimu! Wapo wanaoshupaa kabisa na kudai kwamba Watanzania wengi wanataka kuona Bunge live kwahiyo 'wengi wape'.
Ni wengi wapi hao? Tanzania imejaa maskini ambao hats mlo mmoja kwa siku kuupata niv shida. Hivi ni kweli wengi hawa, maskini wa Tanzania wanataka Serikali yao ionyeshe tv live badala kuwakwamua kwenye umaskini wao?
Ifike mahali 'sisi' Watanzania wachache wenye uwezo tuwafikirie na Watanzania wenzetu walio wengi ambao wanaihitaji sana hiyo fedha ambayo Serikali inadhamiria kuokoa kutoka matangazo live. Na wao wana haki pia!
Pengine Serikali ya HAPA KAZI TU ingetutangazia kwamba hakuna kuonyesha Bunge live ili waangaliaji wote wachape KAZI maana ni muda wa kazi kwa Watanzania wote Wakulima na Wafanyakazi!
Pengine Serikali ya HAPA KAZI TU ingetutangazia kwamba hakuna kuonyesha Bunge live ili waangaliaji wote wachape KAZI maana ni muda wa kazi kwa Watanzania wote Wakulima na Wafanyakazi!
Sijui kama kuna kituo cha redio kinatangaza safari hii tumeipata.Hata walio masikini hujikusanya mahali wakaona.
Mmewawezesha?Miaka 50 baada ya Uhuru umaskini unatisha kwa kufungia matangazo ya Bunge wafanye kazi umaskini utawatoka what a joke,tena tubhu kuita watu maskini hili hali awakujitakia kuwa hivyo.Tuwe wakweli, hao maskini unaowasema ndio wale wanaofuata drama za bungeni si lolote la maana. Katika awamu hii maskini wanatakiwa wafanye kazi kwa bidii ili wajikwamue kutoka kwenye umaskini wao.
Fikiria zaidi mkuu. .bado! Democracy ina gharama zake! !unapoelekea utataka hata mishahara isilipwe tununue madawatiMimi bana silipwi na yeyote. Mie ni Mtanzania maskini na mzalendo niliyejipa kazi ya uanaharakati wa kutetea maslahi ya maskini wenzangu. Sisi maskini waTanzania tunawaomba Azam na vituo vilivyojitolea waunge mkono juhudi Rais Magufuli waelekeze fedha hizo kwenye madawati, vitanda mahospitalini nk. Nawashangaa sana nyie ambao mko radhi watoto wa Watanzania wenzenu wasome wameketi mchangani, akina mama wajawazito walale chini ninyi wkt ninyi mnastarehe kuangalia Bunge live!
Ndiyo, hasa hasa likiwa lime anzia ccm, mashabiki wapo kibwena hadi wale wa kulazimishwaHivi akitokea mtu na kushauri bunge lifutwe kukaa kama bunge na kubakia kamati nasi wananchi tusijulishwe chochote kwa kuwa hayo ni garama kubwa, hilo nalo litapata washabiki?
Kiuchumi na kinadharia "your statement is unjustifiable " mpaka unieleze mbinu za kumwezesha mtu kuchapa kazi.Wakati wa bunge live, masaa 8 au 9 yanapotea kwa siku. Elimu ndogo tu ya uchumi utajua thamani ya masaa kazi wanayopoteza Watz kwa kukodoa mimacho kuangalia bunge live badala ya kuchapa kazi. Hao Azam na Star Tv waruhusiwe ku-record na warushe usiku. Uangalie masaa hayo yote usiku shauri yako, kesho yake tunataka uchape kazi tu.
Kwani ww shambani unabeba tv yako na kulima nayo ! acha uvivu fanya kazi , wanaotetea jambo hili ni wavivu hawana kaziTunachotaka mtuambie ni sababu gani zilizosabisha serikali ya matingatinga kuzuia bunge kuoneshwa live. Hakuna hata anayethubutu kueleza sababu japo moja tu zaidi ya kutembea na fisi kwenye mikutano ya hadhara.
Shambani wanabeba radio.Kwani ww shambani unabeba tv yako na kulima nayo ! acha uvivu fanya kazi , wanaotete jambo hili ni wavivu hawana kazi
Sisi Magufuri anatosha mengine hatuna habari nayo hata kama hatuna bunge sawa tu , watu wanakaa kupiga porojo eti nipoteze muda kuwaangalia , ukiangalia bunge live ndio unaletewa mkate wa kula , acha uvivu hapa kazi tuHivi akitokea mtu na kushauri bunge lifutwe kukaa kama bunge na kubakia kamati nasi wananchi tusijulishwe chochote kwa kuwa hayo ni garama kubwa, hilo nalo litapata washabiki?