Bunge liombe radhi

Bunge liombe radhi

Najijua

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
1,040
Reaction score
182
Wadau nawasilisha hoja barazani la kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutuomba radhi walipa kodi wa nchi hii, wapiga kura wao na wenye maamuzi makubwa dhidi yao kabla hatuhatumia haki yetu ya kikatiba kuwataka wawajibike mbele yetu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo,

1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika

2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.

3. Staha ya kuvaa nayo imepungua na juzi naibu Spika amelalamikia uvaaji hususani waheshimiwa wa jinsia KE

Haya na mengine yote ambayo sija yataja hapa juu ni uthibitisho wa bunge kutukosea watanzania hivyo wanastahilli kutuomba radhi kabla hatujalazimisha kupewa heshima zetu
 
Wadau nawasilisha hoja barazani la kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutuomba radhi walipa kodi wa nchi hii, wapiga kura wao na wenye maamuzi makubwa dhidi yao kabla hatuhatumia haki yetu ya kikatiba kuwataka wawajibike mbele yetu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo,

1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika

2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.

Kwa haya nakuunga mkono Bruker. Nilisikitika sana jana, mpaka nikawa siamini macho na masikio yangu, kuwa hili ni bunge au kilabu cha kimpumu. Nadhani Spika inabidi atumie mamlaka yake vema kurudisha nidhamu ya bunge, lakini afanye hivyo baada ya kututaka radhi watanzania.
 
mmmh me nafikiri kuomba radhi sio suluhisho ukweli ni kwamba wamekosa adabu huwa najiuliza hao wanaozomea wana:watoto?,degree?,wake,?waume?, au ni wahuni tu walioingia bungeni kupitia migongo ya wahuni wenzao?manake hata makazini wale walioingia kwa migongo ya watu bila juhudi na sifa zinazotakiwa huwa hawana nidhamu ya kazi manake hawajui uchungu na thamani ya kazi husika nafikiri na bungeni ni hivyo hivyo da natamani Mungu angenyosha mkono wake akatoa fundisho flani,manake mamlaka imekosa adabu
 
Hakuna haja ya kusubiri ama kuwataka wao waombe radhi, nadhani ni wakati mzuri kwetu sisi wananchi kutathimin mwenendo wa matendo yao na kufanya maamuzi magumu. JAMANI WATANZANIA WENZANGU HEBU TUWE SERIOUS, NEXT TIME TUTUMIE HAKI YETU YA KIKATIBA KWA UFASAHA!
 
Acheni woga, ccm bila ligi ya man to man hayaendi haya mangumbaru. CDM MPs msilale mpk kieleweke.
 
mmmh me nafikiri kuomba radhi sio suluhisho ukweli ni kwamba wamekosa adabu huwa najiuliza hao wanaozomea wana:watoto?,degree?,wake,?waume?, au ni wahuni tu walioingia bungeni kupitia migongo ya wahuni wenzao?manake hata makazini wale walioingia kwa migongo ya watu bila juhudi na sifa zinazotakiwa huwa hawana nidhamu ya kazi manake hawajui uchungu na thamani ya kazi husika nafikiri na bungeni ni hivyo hivyo da natamani Mungu angenyosha mkono wake akatoa fundisho flani,manake mamlaka imekosa adabu

Hivi ninyi watu mna matatizo gani? Kuomba radhi kwa kosa gani, bungeni si mahala pa mchezo, watu wanakwidana mashati bungeni. Nani alikuambia part affiliation ndani ya bunge inatoweka, US kuna blue na red na hata wanavyokaa wanakaa kichama na hilo lipo kila kona. Kuzomea ni jambo la kawaida, Uk house of commons, wanazomea kila siku Hebu mfanye utafiti kuona mabunge yenye vyama vingi yanakuwaje, tatizo tz watu bado tumelala na inasikitisha. India wanazipiga kial siku, loh
 
Wadau nawasilisha hoja barazani la kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutuomba radhi walipa kodi wa nchi hii, wapiga kura wao na wenye maamuzi makubwa dhidi yao kabla hatuhatumia haki yetu ya kikatiba kuwataka wawajibike mbele yetu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo,

1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika

2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.

3. Staha ya kuvaa nayo imepungua na juzi naibu Spika amelalamikia uvaaji hususani waheshimiwa wa jinsia KE

Haya na mengine yote ambayo sija yataja hapa juu ni uthibitisho wa bunge kutukosea watanzania hivyo wanastahilli kutuomba radhi kabla hatujalazimisha kupewa heshima zetu

Kanuni na sheria rasmi ziko wazi tu. Makinda alipaswa kurejea kanuni zilizopo kuhusu dress code na mengineyo na kisha kutoa mwongozo. Kanuni ingeazuia kuzomea wasingezomea, ingewazuia kuvaa vimini wasingevaa. Watanzania wanayo haki ya kuhoji mpaka bunge letu liwe makini zaidi kwa kila hali. Katika mabunge mengi sana, hasa la uingereza ambalo nalifahamu vizuri, kuzomeana hilo ni jambo la kawaida. Nafikiri huko ndo tunakoelekea. La msingi ni kwamba inatupasa kwenda na wakati, katika muktadha wa utamaduni wetu.
 
Spika ameshindwa kumanage bunge.Anakua mkali kwenye hoja za msingi za kitaifa kwa kuzizima kibabe.Kama kweli spika anaweza basi wabunge wote wa mipasho wachukuliwe hatua za kinidhamu.Mi kwa maoni yangu bunge la safari hii ni la kihuni tu,na halina tofauti na kijiwe cha mashabiki wa Simba na Yanga au Man U, Arsenal na Chelsea, pumba tupu.
 
kweli we ichondi naona jina lako limekufiti kabisa mkioso kwa hiyo wabunge wa u.s wakianza kuingia uchi bungeni na wa huku waige?wazungu wana tamaduni fikra mtazamo na mienendo yao na siye yetu sio kila upupu tunaiga basi tuwaige kila kt uone
 
mmh egpytian ulishawhi kusikia mh waziri/mbunge kujibu au akichangia hoja utasikia.............mh spika........ktk bunge lako tukufu la......................


Hapo kweny red ni kweli tukufu? kama watu wanalala mle,wanapasha wenzao na kuzomea?
 
Mi nashimdwa kuelewa, huenda hawa wabunge wa CCM wote fani yao ni kuimba taarabu na pale sio mahali pao, na wapo pale kwa sababu wao ni wachakachuaji wa kura zetu siku zote vinginevyo wasingekuwapo mahali pale. Wanaudhi sana na siwapendi. Chadema kaza buti waonyesheni kuwa nyie ni vichwa hampelekwi pelekwi kama wao. Peopleeeeees power.
 
Mengine yote umesema kweli Bruker ila hili jingine la kusemeana mbovu wenyewe kwa wenyewe hapa spika mwenyewe alipalilia, ule Spika angeondoa ushabiki wa kisiasa akasimamia mwongozo yale yote yasingetokea, kama angekuwa calm kama alivyogundua pale mwishoni akajirudi kwa kuwakemea wote na kuwa wote wangetoka njee na kuahirisha bunge shida kama ile isingetokea. Kwa hili Spika mwenyewe aondoe ushabiki wa kichama na asimamie mwongozo wa bunge.

Aluta continue !
 
Wadau nawasilisha hoja barazani la kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutuomba radhi walipa kodi wa nchi hii, wapiga kura wao na wenye maamuzi makubwa dhidi yao kabla hatuhatumia haki yetu ya kikatiba kuwataka wawajibike mbele yetu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo,

1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika

2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.

3. Staha ya kuvaa nayo imepungua na juzi naibu Spika amelalamikia uvaaji hususani waheshimiwa wa jinsia KE

Haya na mengine yote ambayo sija yataja hapa juu ni uthibitisho wa bunge kutukosea watanzania hivyo wanastahilli kutuomba radhi kabla hatujalazimisha kupewa heshima zetu

Lawama zote ziende kwa mama Makinda ambaye anashindwa kuheshimu Kanuni, dharau kwa upinzani, jazba, nk!
 
Je nuliza . Ushahidi wa PM kudanganya bunge kuhusu yaliyotokea Arusha ni lini utasomwa? Je Kuhusu Msukuma Ngereja ni lini atasasambuliwa na lisi
 
Spika anawalea wabunge wa CCM wakifanya mambo ya kihuni...wanazomea hovyo, wanaongea hovyo hovyo bila kuruhusiwa n.k....kwake hiyo haoni ni ukosefu wa adabu! Mbunge wa CDM akiongea ghafla anakuwa mkali na kuanza kufoka kama anaongea na wanae nyumbani....\

Huu ni unafiki mkubwawa Spika kwa sababu amekuwa anawalea CCM ndio maana hali imefika hapa...na bado mpaka wachapane ngumi labda ndio wataanza kuheshimiana!
 
Mnajua Wabunge wa CCM na spika wao wanadhani walichotumwa na wananchi Bungeni ni kwenda kupambana na Chadema. Hata hoja iwe ya msingi na manufaa kwa taifa madamu imetolewa na Mbunge wa Chadema basi itapingwa na kuzomewa kijinga jinga. Huu ni upumbavu ambao wabunge wa Chadema sasa unaanza kuwachosha na kufikia kusema "funga milango zipigwe"
Makinda angesimamia haki na kuacha ushabiki wake safari hii kungekuwa na Bunge zuri sana kuliko yote yaliyopita kwa kuangalia uwiano kati ya wabunge kivyama,damu mpya,uelewa mpana nk. Fikiri Bunge hili lingekuwa chini ya Sita ingekuwaje kwa Mawaziri? lazima blabla zingeisha.
Wananchi tumewaona wabunge wetu wa CCM na tumejua wamo mle wakiwakilisha nini badala ya kutuwakilisha sisi. Huwezi kukubali ulipanga foleni masaa kadhaa kumchagua mtu anayeleta mizaha na kuzomea wengine wenye kutoa hoja zenye mishiko. Huyo hafai na lazima nasi wakirudi majimboni tuwaambie hatukuwatuma hayo na ujinga hatutaki maana ndio unaotufanya tushindwe kutengana na umasikini.
 
Yaani bunge linaendeshwa kiushabiki zaidi, kilichotokea jana ni kama kwenye kilabu cha pombe.
 
Hii ni wazi Spika Bunge limemshinda haliwezi kabisa Bunge la mwaka huu! yuko kichama zaidi kuliko maslahi ya Taifa anajisahau kuwa kile ni chombo cha Taifa na sio chao cha Magamba! iko siku ngumi zitalika kule bungeni, kama jana jioni nilikuwa naangalia taarifa ya habari kupitia mlimani tv nilijionea vituko hasa nikajiuliza bunge letu limekuwa nila vijembe kama waimbaji taarab au....!

Makinda asipojiangalia vizuri nae atavuliwa magamba!
 
Mimi naona bunge liende hivi hivi mpaka pale kanuni zitakavoanza kufuatwa na yule mama lasivyo ccm wanaona kama bunge ni mali yao. Siku hizi waziri akidanganya anaambiwa hapo hapo kwa sababu amna haja ya kuwa na bunge la makondoo linalopitisha miswada kwa maslahi ya chama..Peoples power mpk kielewekeee
 
Hivi ninyi watu mna matatizo gani? Kuomba radhi kwa kosa gani, bungeni si mahala pa mchezo, watu wanakwidana mashati bungeni. Nani alikuambia part affiliation ndani ya bunge inatoweka, US kuna blue na red na hata wanavyokaa wanakaa kichama na hilo lipo kila kona. Kuzomea ni jambo la kawaida, Uk house of commons, wanazomea kila siku Hebu mfanye utafiti kuona mabunge yenye vyama vingi yanakuwaje, tatizo tz watu bado tumelala na inasikitisha. India wanazipiga kial siku, loh

Letu ni bunge la watanzania kwahiyo kunaumuhimu wa kuheshimu kanuni zilizowekwa za kuliendesha bunge letu; kusema kuwa kwa vile wabunge wa uingereza wanazomeana na sisi pia tuige tabia hiyo si sahihi kwani uzomeaji ni ukosefu wa adabu na hufanywa na wale wasio kuwa na hoja za nguvu. Ni vizuri tukaiga yale tu mazuri yanayofanywa na mabunge ya nchi nyingine pasipo kuiga hovyo hovyo tu ilimradi mabunge mengine yanafanya hivyo!!
 
Back
Top Bottom