Najijua
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 1,040
- 182
Wadau nawasilisha hoja barazani la kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutuomba radhi walipa kodi wa nchi hii, wapiga kura wao na wenye maamuzi makubwa dhidi yao kabla hatuhatumia haki yetu ya kikatiba kuwataka wawajibike mbele yetu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo,
1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika
2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.
3. Staha ya kuvaa nayo imepungua na juzi naibu Spika amelalamikia uvaaji hususani waheshimiwa wa jinsia KE
Haya na mengine yote ambayo sija yataja hapa juu ni uthibitisho wa bunge kutukosea watanzania hivyo wanastahilli kutuomba radhi kabla hatujalazimisha kupewa heshima zetu
1. Kushindwa kutumia hekima na busara kwa kuendesha mijadala wa wapo mjengoni, hii tabia imekithiri na imeanza kuota mizizi, siku hizi ni kawaida sana kusika bungeni wabunge wakizomea, dhihaki michango ya wenzao na hata kuropoka pasipo mpangilio, wanakwenda mbali zaidi hata kupingana na muongozo wa spika
2. Wabunge siku hizi wanajadili hoja na miswada kwa kufuata ushabiki wa kisiasa wa itikadi wa vyama vyao na si maslahi ya taifa letu, wanaweka maslahi ya chama mbele ya nchi nyuma.
3. Staha ya kuvaa nayo imepungua na juzi naibu Spika amelalamikia uvaaji hususani waheshimiwa wa jinsia KE
Haya na mengine yote ambayo sija yataja hapa juu ni uthibitisho wa bunge kutukosea watanzania hivyo wanastahilli kutuomba radhi kabla hatujalazimisha kupewa heshima zetu