Bunge lakumbwa na kashfa nzito

Wakuu,

Hii hoja ina mambo mengi sana na ngumu kuchangia bila kujikanyaga. Kuna mambo mengi yamejadiliwa na mengi yanapingana.

Je ni lazima kuweka chuo ulichosoma kwenye kila CV? Hapana sio lazima ila ni muhimu. CV ni picha ambaye unampelekea dada anayetaka kuchagua mume wa kumuoa. Sifa za kuwa mume bora ziko nyingi sana na katu haziwezi kujulikana kwa kutumia hii picha moja. Lakini utakuwa kichaa kama utatuma picha ambayo unaonekana ni kituko. Inategemewa kwamba utajaribu kupeleka picha nzuri zaidi ili angalau uwe kwenye shortlist ya kuonana na huyu dada na hapo ndipo sifa zingine zitajulikana.

Chuo ulichosoma kinasaidia kuonyesha/kutoonyesha sifa uliyonayo. Kwa kutokuweka jina la chuo unaweza kuonekana umeficha makusudi, hivyo hufai, unaweza kumpa hamu huyo mtu atake kujua zaidi juu ya wewe na hivyo kukuingiza kwenye shortlist.

Kiujumla nitasema kwa kazi ambayo ni professional, nategemea kuona jina la chuo ulichosoma. Ukisema umemaliza form four lazima useme umemaliza wapi? Ukiandika umemaliza chuo kikuu, nitategemea useme ni chuo gani.

Kwa wengine chuo ulichosoma na kupasua kwako vinaishia kwenye shortlist. Ukija kwenye interview nitataka zaidi kujua unajua nini. Kila mtu ninayemwita kwenye interview ninakuwa na uwezo wa kumpa kazi. Ni kwamba katimiza minimum requirements ya kazi husika. Kwahiyo kuniambia umemaliza na A+ hainisaidii, ninataka kujua shuleni umefanya nini, umefanya projects zipi, mwisho wake ulikuwaje, ulipambana na matatizo gani, uliyatatua vipi nk. Mtu ninayempa kazi ni kwasababu amenionyesha anajua nini.

Je inawezekana kuchukua wanafunzi wa chuo kimoja tena darasa moja? Ningelikuwa mimi nisingelifanya hivyo hata siku moja hata kama hicho chuo kingelikuwa bora sana. Diversity ni jambo muhimu sana, kwa kuwa na interviewees toka vyuo mbalimbali unaweza kujifunza mengi na hivyo kufanya uchaguzi ambao ni wa maana zaidi. Hata probability inakataa kwamba katika vyuo 10, chuo kimoja tena watu wa mwaka mmoja wanaweza kuwa wazuri kuliko hawa wengine wote.

Haya mambo ya chuo kipi bora, nafikiri yapo toka miaka na miaka. Nakumbuka wakati wengine tupo mlimani, kulitokea vita kali kati ya UDSM na Mzumbe. Mwenyekiti wetu alitamka kwenye vyombo vya habari kwamba inakuwaje wanafunzi wa junior colleges kama Mzumbe wapate allowances kubwa kuliko sisi. Mzumbe walikuja juu sana.

Sidhani kama mijadala kama hii inasaidia sana jamii. Uzuri wa jambo unatokana na mambo mengi sana. Inawezekana UD ni brand kubwa na inapata wanafunzi wengi wazuri kwasababu ya jina lakini je output yake pia ni nzuri? Ni vizuri kumwangalia kila mtu individually na kumpima kama anafaa au la. Tukianza kuajiri watu kwa kufuata amesoma wapi, inaweza kutuletea matatizo mengi sana.

Kuitwa kwenye interview ni hatua kubwa kuelekea kupata kazi. Ukisoma chuo ambacho brand yake inajulikana unakuwa umejirahisishia njia ya kwenda kwenye interviews nyingi na hivyo kupata kazi kirahisi. Chuo kikiwa na brand kama vile Oxford, Havard nk. kinakuwa kinapata wanafunzi wazuri zaidi, kinavutia walimu wazuri zaidi, research nyingi muhimu zinapelekwa kwao, ni rahisi kupata pesa nyingi zaidi, hivyo mara nyingi hata output yake inakuwa graduates wenye uwezo zaidi.

Umemaliza kila kitu,Thomas kashilillah na NOMBO ambaye ana kaimu ukurugenzi wa utawala na utumishi kwa upuuzi huu hahitajiki kukaimu atafutwe mtu mwingine, labda watajifunza.
 
cha ajabu wahitimu zaidi ya 15 toka chuo kimoja,darasa moja, ST.AUGUSTINE UNIVERSITY ambao wamehitimu NOV 2008 walitakiwa wawe na uzoefu wa Miaka miwili, wote wamekuwa short listed na wameitwa kwenye interview.Wengi wenye sifa toka vyuo vingine kama UDSM hawakuitwa.

It is hard to believe kanda2's posting, unless we are provided with more evidence.

Though everyone has the right to post anything, it'll be stupid for us to just jump affimatively into any postings, even if its validity is seemingly doubtful.

popcorn.jpg


P'se, don't just relax with your popcorn, do some thinking.
 
kwanza si vyema kutaja majina ya watu bila idhini japokuwa unahoja. Pili kuitwa interview watu wa darasa moja siyo ajabu, mimi nilifanya interview pale TBL DSM mwaka 2006 na alikuwa anatakiwa maintenance engineer tukakutana watu tisa wote darasa moja na mmoja wetu akachukuliwa. Nadhani acha vijana wenzetu wachape kazi cha msingi wasijiingize kwenye ufisadi.

Magezi...2006 Maintenance Engineer ungempata wapi zaid ya UDSM?...Kuna vyuo hadi sasa wana Kozi 2 au 3...the same kama wakati huo MD obvious wangekuwa kutoka Muhimbili....labda wengine waliosomo Nje ya Tanzania kama walikuwepo.....

Pia kutokea tukio 2006, kukawa hakuna mtu alielalamika, sio passport kuwa hatuwezi jadili ya leo hii 2009 ktk Taasis ya Public, wachache kuamua nani wamuajiri na nani wasimuajiri hilo haliwezekani...

Tunachotaka wahusika pale Bungeni waje PUBLIC kueleza umma vigezo gani vimetumika kuchukua wanafunzi kutoka chuo kimoja
.
 
It is hard to believe kanda2's posting, unless we are provided with more evidence.

Though everyone has the right to post anything, it'll be stupid for us to just jump affimatively into any postings, even if its validity is seemingly doubtful.

popcorn.jpg


P'se, don't just relax with your popcorn, do some thinking.

Kama unaona mimi ni muongo njoo na Facts kusema sio kweli majina hayapo na hayakuwa Nyegezi November 2008.Nimekuwekea majina yote na interview wamefanya kuanzia tarehe tatu hadi 13 mwezi huu,majina yao yakuitwa kwenye interview yalitoka kwenye Daily News na mwanachi kati ya feb 10 hadi 14.

Tangazo la kazi lilitangazwa tarehe 12 mwezi december 2008 kwenye Mwananchi na Daily News,wahitimu wa ST.Augustine wakiwa na wiki mbili tu toka wahitimu kwa maneno mengine bwana Nombo na DR.Kashililla walikuwa wanasubiri jamaa wamalize ndio watangaze kazi.

kama wewe unautaka ukweli kanusha habari yangu kwa kuwasiliana na DR.Thomas Kashilillah au Nombo namba zao ni Ofisi ya Dar-es-salaam ni +255 222 112065/7 na Dodoma ni +255 26 232315.

Game Theory amebahatika kuona document ya dhuluma ya DR.Thomas Kashilillah muulize kama unataka ukweli.
Kama Kashilillah au Nombo wamekutuma uje kutetea ujinga wao kwa mwendo huu wako utazidi kuwachafua.wameshikwa pabaya.
 
Eti niulize hakuna hata mzanzibar mmoja aliyeomba nafasi hizo ukizingatia bunge ni chombo cha muungano?
 
Eti niulize hakuna hata mzanzibar mmoja aliyeomba nafasi hizo ukizingatia bunge ni chombo cha muungano?

Wengi waliomba wamekatwa.kulikuwa na watu zaidi ya elfu mbili.kuna case nzito kuliko hao waZanzibar, kwa vile uchunguzi unaendelea sitoweza kuziweka wazi kwa sasa kuachia uchunguzi ufanye kazi yake.
 
Sasa kama nafasi say ni 14?? 20?? na maombi ni 2000 na ni Bunge la Muungano- kweli hakuna haja ya kuwa na quota ya nafasi hata 1 zu 2 toka visiwani kama kati ya waliiomba wanaqualify??

Hii ya kuchukua tu wanafunzi wa chuo kimoja kutakuwa kuna walakini!
 
Sasa kama nafasi say ni 14?? 20?? na maombi ni 2000 na ni Bunge la Muungano- kweli hakuna haja ya kuwa na quota ya nafasi hata 1 zu 2 toka visiwani kama kati ya waliiomba wanaqualify??

Hii ya kuchukua tu wanafunzi wa chuo kimoja kutakuwa kuna walakini!

sio chuo kimoja tu BALI DARASA MOJA Labda kuna faida kuwa kutakuwa hakuna haja ya introduction siku ya kuanza kazi kwani wote wanajuana.

ni bora kashilillah na Nombo wangeweka kuwa masharti ya kuomba uwe umesoma NYEGEZI-ST-AUGUSTINE au watuambie wazi kuwa CHUO CHA BUNGE NI NYEGEZI kama ILIVYOKUWA KWA CCM KUWA NA CHUO CHAO KIVUKONI.

Tujue kuwa chuo cha CCM ni kivukoni na chuo cha BUNGE NI ST.AUGUSTINE hakuna atakayelalamika kwani itakuwa wazi inajulikana na ikitangazwa kazi uspiteze wino na stempu yako kutuma barua ya maombi kama hutoki CHUO CHA BUNGE-ST AUGUSTINE.
 
Standards zetu ziko chini sana.Sikupenda walivyowavunjia privacy waomba kazi hapo.Kuna watu wengine wana mind business zao ziwe private, sasa kibongo bongo watu washawekwa mijina kwenye migazeti ya mtandaoni.
 
Eti niulize hakuna hata mzanzibar mmoja aliyeomba nafasi hizo ukizingatia bunge ni chombo cha muungano?

Si bora ungesema kuna udini hapo kama kule kwenye Axis of Mafisadi ,walokole watupu ,au uwongo ? eeti jamani naandika uwongo ? Si mumeona kule wanakowatafuta watu hamsini tu wanaojichukulia chao mapema.
 
Standards zetu ziko chini sana.Sikupenda walivyowavunjia privacy waomba kazi hapo.Kuna watu wengine wana mind business zao ziwe private, sasa kibongo bongo watu washawekwa mijina kwenye migazeti ya mtandaoni.

Nilipoanza sikuweka majina nikaambiwa muongo, nimeweka majina standards ziko chini, nimemsikilize nani?yako mengi ya private sijayaweka juu yao kama pass zao n.k kwenye kujenga au kurekebisha lazima maumivu yatokee ili turekebishe.
 
Nilipoanza sikuweka majina nikaambiwa muongo, nimeweka majina standards ziko chini, nimemsikilize nani?yako mengi ya private sijayaweka juu yao kama pass zao n.k kwenye kujenga au kurekebisha lazima maumivu yatokee ili turekebishe.

Wewe umeweza kuweka majina haya kutokana na system mbovu inayoruhusu kutoa majina haya katika files za HR.

What's next, watatoa mishahara yao pia?

Kama kuna ufisadi mtuhumiwa namba moja ni HR, kama kuna mtu wa kusakamwa na kutolewa jina ni hao watu wa HR.

Unless una ushahidi concrete kwamba hawa waomba kazi walitoa rushwa au kuhusika na ufisadi ili kupata kazi, kuwatoa majina ni kuwa expose unnecessarily.
 
Wewe umeweza kuweka majina haya kutokana na system mbovu inayoruhusu kutoa majina haya katika files za HR.

What's next, watatoa mishahara yao pia?

Kama kuna ufisadi mtuhumiwa namba moja ni HR, kama kuna mtu wa kusakamwa na kutolewa jina ni hao watu wa HR.

Unless una ushahidi concrete kwamba hawa waomba kazi walitoa rushwa au kuhusika na ufisadi ili kupata kazi, kuwatoa majina ni kuwa expose unnecessarily.

Nimeshamuweka muda mrefu mkuu wa HR ni Nombo soma maelezo yangu.majina ya hawa watu yako kwenye magazeti niliyokuwekea tarehe zake huko nyuma hakuna siri wala kuwa expose.magazeti yamesha wa expose.

kama wao Bunge wanaona wanaonewa wangefanya press conference kuelezea jambo hili wamekaa kimya kwa vile kuna ukweli kwenye shutuma hizi.
 
Kanda2

Unahangaika sana wala hakuna sehemu utakapofunga huyo jamaa ama hao jamaa unless uwe na kithibitisho cha kuwa walitoa na kupokea rushwa.

Hizo argument zako ni feki wala hazina afya ,sikatai jamaa kufanya manuva lakini kwa hoja zako hizi ni hoja zilizo na utapiamulo.Lete vithibitisho vya rushwa na sio darasa moja na experience.
 
Game Theory, Dar es salaam wamawazo kuwa waislam wamebaguliwa kwenye hii selection... Ndio maana unaona statement kama "...ohoo ngoja nipige simu kwa first lady" .. akitegemea JK na first lady i.e. waislam wenzao watawasaidia). OK?
MY TAKE: Tutetee haki bila kungalia kwanza dini ya "victim".
 
Mkamap.

Wamekuja watu wawili kukuelekeza jinsi ya kuandika CV.mimi nimekuwekea link ujifunze kuandika cv.
Nakuuliza ule mpango wako uliotutangazia kuwapeleka majuu wachezaji wetu umefikia wapi?umemuona Yusuph Bakhressa anayejua kuandika CV kijana Ngassa anakwenda west ham united.

wewe umeshindwa hayo utazijua hoja zangu? BUNGE sio jeshi walikojazwa wakurya watupu enzi za Mwalimu.

unajua kuwa shrika la Bima liliwahi kuundiwa Tume ya kuchunguza ajira za ubabaishaji kama hizi?ilikuwa kila atokae Mbeya anapata kazi, sawa na bunge kwa kila atokae Nyegezi.hakuna lisilo na mwisho za mwizi arobaini Nombo na kashilillah wako kikaangoni.
by the way vipi box ALCATEL leo?kule kwa michuzi blog kuna mjadala wa box tunaomba mchango wako.
 
Game Theory, Dar es salaam wamawazo kuwa waislam wamebaguliwa kwenye hii selection... Ndio maana unaona statement kama "...ohoo ngoja nipige simu kwa first lady" .. akitegemea JK na first lady i.e. waislam wenzao watawasaidia). OK?
MY TAKE: Tutetee haki bila kungalia kwanza dini ya "victim".

JK alipounda tume ya jaji kipenka Mussa kufuatilia mauaji ya wafanyabiashara ya madini katika orodha ya wafanyabiashara wale kulikuwa na muislam?na aliyekuwa akiwindwa ni Abdallah Zombe ambaye muislam mwenzake.

Mstaafu Mkapa aliwahi kuivunja bodi ya Parole iliyoundwa na Sumaye kwa vile ilikuwa na dini moja yaani wakristu akasema iundwe upya kwa kujumuisha watu wa dini mbalimbali,jee yeye alikuwa muislam?

Nimesema kuwa waliokuwa wanafunzi wa Tumaini university chuo cha kikristu wameachwa kwenye ajira hizi hao si waislam,tunachopigania ni haki na usawa.mwenye uwezo hata kama ni Nyegezi apewe ila zisivunjwe taratibu kumpitisha mtu au watu kama wanalivyofanya kina Nombo.

Hili suala First lady linamuhusu vipi? waliofikishiwa kesi ni Phillip Malmo,Mizengo Pinda, Hossea wa Takukuru,Spika,waziri Kapuya,Ikulu kama taasisi n.k mimi sikuona nakala ya mama Salma.
 
Mkamap.

Wamekuja watu wawili kukuelekeza jinsi ya kuandika CV.mimi nimekuwekea link ujifunze kuandika cv.
Nakuuliza ule mpango wako uliotutangazia kuwapeleka majuu wachezaji wetu umefikia wapi?umemuona Yusuph Bakhressa anayejua kuandika CV kijana Ngassa anakwenda west ham united.

wewe umeshindwa hayo utazijua hoja zangu? BUNGE sio jeshi walikojazwa wakurya watupu enzi za Mwalimu.

unajua kuwa shrika la Bima liliwahi kuundiwa Tume ya kuchunguza ajira za ubabaishaji kama hizi?ilikuwa kila atokae Mbeya anapata kazi, sawa na bunge kwa kila atokae Nyegezi.hakuna lisilo na mwisho za mwizi arobaini Nombo na kashilillah wako kikaangoni.
by the way vipi box ALCATEL leo?kule kwa michuzi blog kuna mjadala wa box tunaomba mchango wako.

Rafiki wewe hoja zako zina utapiamulo kazipe dayati urudi zishibe zirudi tuzielewe vinginevyo utaishia kusema Bunge lakubwa na kashfa nzito.

Naona unashangaa kweli kuhusu alcatel nafahamu unachokoza ili upate kufahamu inakuwa je mwanafunzi kuomba kazi.Kifupi nitakwambia hivi hapa ukiwa mwanafunzi kuanzia mwaka wa nne hadi tano unapeleka timetable yako ya masomo unafanya kazi full time na ninaposema full time sio kama unavyoelewa bali ni hivi fanya vyovyote uwezavyo ila kwa wiki uwe umekamilisha masaa 40 yakazi.

Na kingine nikuwa yawezekana wewe una wikinesi fulani unapoona experience wameandika miaka mitatu wakati wewe huna,kama unajiamini na umeelimika omba hizo kazi usiogope hiyo experience wanayotaja,Lakini kama ulikuwa mpiga DESA mzuri bora ufunike kombe mwanaharamu apite.
 
Mkamap.

Kozi gani ya miaka mitano au medicine?Alcatel walikuchukua ukafanye Medicine kwao?hapa unakusudia wapi?
Sishangai kushindwa kuwapatia timu wachezaji kwani huna uwezo wa kujieleza au kuelewa topic inasema nini.

Hapa nimekuwekea kila kitu bado una bisha inawezekana hao waliopita ni jamaa zako au kashilillah una ujamaa nae.msome Mtanzania alivyokuweka sawa! msome Chuma ulivyomchanganya na maelezo yako.kama wana JF hawakuelewi wenye timu wangeweza kukuelewa? uko nchi gani Russia au Ukraine?

Nakusaidia kwa mara nyingine. soma kitabu Great Answers to Tough Interview Questions na Martin John Yate.
Mwambie Nombo na Kashilillah wapitie.
 
Back
Top Bottom