Bunge lakumbwa na kashfa nzito

kanda2

JF-Expert Member
Apr 22, 2007
1,318
72
Bunge letu kama taasisi limetangaza nafasi za kazi mbali mbali hivi karibuni.

Kilichotokea nafasi hizo zilikuwa na watu maalum wameandaliwa. Moja ya masharti kama kuwa HANSARD REPOTER lazima uwe na na diploma au digrii ya mambo ya habari na uzoefu wa MIAKA MIWILI.

cha ajabu wahitimu zaidi ya 15 toka chuo kimoja,darasa moja, ST.AUGUSTINE UNIVERSITY ambao wamehitimu NOV 2008 walitakiwa wawe na uzoefu wa Miaka miwili, wote wamekuwa short listed na wameitwa kwenye interview.Wengi wenye sifa toka vyuo vingine kama UDSM hawakuitwa.

Watu wengi wamelalamikia utaratibu huo wa ajira na mimi nimebahatika kuona barua rasmi iliyotumwa kwa DR.Thomas Kashishillah katibu wa bunge, kumtuhumu kufanya mazingaombwe kwenye ajira hizo, nakala ya barua hiyo imekwenda Ikulu, waziri mkuu, Takukuru, Waziri wa kazi na ajira, Waziri wa utawala bora, Usalama wa Taifa nk.

Kama BUNGE linashindwa kufanya mambo yake kwa kanuni na Taratibu wapi wataweza kufuata kanuni?
 
Itabidi kabla ya malalamiko muangalie mtaala wa hicho chuo compare na vyuo vingine,pili reputation ya wahitimu wa hapo ni work area .Je UDSM wamefanya curriculum development mara ya mwisho lini?

Ok ,ukiajcha hayo hapa kinachoonekana wazi ni hawa walio kuwa short listed ni fresh from school nov,2008 let us worry about that,unless otherwise kulikuwa hakuna wenye uzoefu .
 
Kama BUNGE linashindwa kufanya mambo yake kwa kanuni na Taratibu wapi wataweza kufuata kanuni?

Nani kakwambia kuwa Bunge letu linafanya mambo yake kwa sheria na kanuni. Record zinaonyesha kuwa linafanya mambo yake kwa kujuana na kupendeleana.

Mifano:

1. Kesi ya Malima vs Mengi na kesi ya Karamagi vs Zitto. Wote walituhumiwa kusema uongo Bungeni. Mmoja (Malima) hakuchukuliwa hatua yeyote licha ya kumkashifu Speaker, wakati zitto alisimamishwa kwa muda.

2. Kesi ta IPTL vs Dowans. Wote wanauza mitambo chakavu. Mmoja (IPTL) Bunge linapiga chapuo inunuliwe, mwingine (Dowans) linakataza. Sheria ni ile ile moja. Huku inakataza na kwengine inaruhusu..
 
Kwa habari nilizonazo toka ndani ya Bunge, hizi kazi waliapply watu zaidi ya 2000. Inakuwaje wachaguliwe watu wa chuo kimoja, same intake tena wasio na uzoefu kama kweli hicho kilikuwa ni moja ya vigezo?
 
Mimi nadhani tatizo liko hapo HR department na katibu nae kuchi nehi che! na huyo ni katibu mpya... hiyo title imeshtua kidogo

Lakini pia tuache unafiki tuongee ukweli, huyo kashishila ni mtu wa wapi? maana kuna makabila humu bongo kwa kujuana yanakera
 
Mbona tanzania haya mambo si mageni? Serikalini ajira ziko kwa muundo huo. Kam humjui mtu uistegemee kupata ajira kirahisi.
 
Mara nyingi ujue kulikuwa na mtu mmoja ana mtu wake pale na akaona bora achukue darasa zima pamoja na marafiki za mtu anayemjua.

Hii inafanyika mara nyingi sana,mtu anaua soo kwa kuchukua watu wengi lakini kumbe nia yake ni mtu mmoja.

Me naomba kama kuna mtu ana majina ya watu waliochukuliwa ayamwage hapa tufanye uchunguzi wa kina.
 
Ok kama kweli malalamiko tayari yalisha pelekwa kunako husika naona mpaka takukuru, ikulu etc ngoja tuone ni hatua gani itachukuliwa. Otherwise our nation is rotten.
 
One of the Mega problem katika nchi zetu maskini Tanzania ikiwa No1 ni kuwa still we value the Technical know who katika mambo mbalimbali. Na hili ni tatizo sugu sana. Maendeleo hayatafikiwa katu mpaka hako ka utamaduni kachafu kafutike. Transperency iwe juu Then Accountability ichukuwe mkondo. Kila kitu ni kujuana!!!!! everywhere!!! Kutoka Ikulu mpaka kwa mjumbe wa nyumba kumi kama unataka any official representation. Then mtakuja kushangaa watakoajiriwa katika kazi hiyo ikija who gets what then kujuana kutapita. HR katika Tanzania needs an overhaul.
 
popcorn.jpg


Ngoma itaja kuwa nzito hii..hebu ngojs nijichukulie popcorn mie



Hiii habari imekuwa inasemwa chini kwa chini na najua kuwa kuna uchunguzi ulikuwa unaendelea.

Mwanzilishi wa mada naona anazunguka mbuyu tuu

kuna tuhuma nzito za UDINI kwenye hii issue na binafsi nimeiona ile document iliyo kwenda mpaka Ikulu. Japo ilikuwa na mapungufu kadhaa lakini ni wazi kuwa tuhuma zilikuwa nzito sana. Waliokuwa wanafanya zoezi la usaili kwenye hili inasemekana walipitisha majina ya wasio na na sifa kwa sababu za dini zao na walioachwa nao inasemekana kuwa walikuwa na sifa zaidi ya hao waliopitishwa

Hii issue naona kadri muda unavyozidi kwenda itakuwa kama JINAMIZI linalokuja na kuondoka

By the way hii thread ikiachwa hapa watu wawili waliohusika na zoezi watakuja humu kujitetea kwani huibuka pale ambapo watu wao hutajwa kwenye kashfa kama hizi....kuna mengi yanaandaliwa na I am sure kuwa hii itakuja kublow out of proportion sasa sijui kama waheshimiwa washaliona hili au la
 
mimi sikatai watu wa darasa moja kuitwa kwenye interview haiwezekani,je wangekuwa wahitimu kutoka University of Dar-es-salaam ndio wameitwa kwenye hiyo interview pangekuwa na maneno?mimi naamini ST aguasyin University wako juu tuache majungu
 
Ngoma itaja kuwa nzito hii..hebu ngojs nijichukulie popcorn mie

Hiii habari imekuwa inasemwa chini kwa chini na najua kuwa kuna uchunguzi ulikuwa unaendelea.

Mwanzilishi wa mada naona anazunguka mbuyu tuu

kuna tuhuma nzito za UDINI kwenye hii issue na binafsi nimeiona ile document iliyo kwenda mpaka Ikulu. Japo ilikuwa na mapungufu kadhaa lakini ni wazi kuwa tuhuma zilikuwa nzito sana. Waliokuwa wanafanya zoezi la usaili kwenye hili inasemekana walipitisha majina ya wasio na na sifa kwa sababu za dini zao na walioachwa nao inasemekana kuwa walikuwa na sifa zaidi ya hao waliopitishwa

Hii issue naona kadri muda unavyozidi kwenda itakuwa kama JINAMIZI linalokuja na kuondoka

By the way hii thread ikiachwa hapa watu wawili waliohusika na zoezi watakuja humu kujitetea kwani huibuka pale ambapo watu wao hutajwa kwenye kashfa kama hizi....kuna mengi yanaandaliwa na I am sure kuwa hii itakuja kublow out of proportion sasa sijui kama waheshimiwa washaliona hili au la


MKUU HII MAMBO UNAIJUA ZAIDI YA 'MRUSHA THREAD'..........fanya kuirusha upya in a 'detailed format'
 
mimi sikatai watu wa darasa moja kuitwa kwenye interview haiwezekani,je wangekuwa wahitimu kutoka University of Dar-es-salaam ndio wameitwa kwenye hiyo interview pangekuwa na maneno?mimi naamini ST aguasyin University wako juu tuache majungu

ST.Augustine hawako juu kuwashinda UDSM au Tumaini University.waliochukuliwa wana kiwango kidogo cha kufaulu.nimebahatika kuona vyeti vya walioachwa na waliopita kwenye interview,wameachwa wengi wenye uzoefu na uwezo.mfano sharti la kazi lazima uwe una uzoefu wa miaka miwili hao wa ST.AUGUSTINE hata mmoja hana sifa hiyo.huwezi kuchukua watu wa darasa moja Hansard Repoter wameitwa watu 15 kwenye interview na wa ST.AUGUSTINE wako 14. nafasi zinazotakiwa ni saba.ST.Augustine hawawezi kuwa juu ya UDSM hata kwa nini.inaonekana wewe ni mmoja ya hao walioitwa kwenye Interview wakiwa wahitimu wa ST.Augustine utasema vipi majungu wakati Hard Facts zipo na unapewa.
 
Mara nyingi ujue kulikuwa na mtu mmoja ana mtu wake pale na akaona bora achukue darasa zima pamoja na marafiki za mtu anayemjua.

Hii inafanyika mara nyingi sana,mtu anaua soo kwa kuchukua watu wengi lakini kumbe nia yake ni mtu mmoja.

Me naomba kama kuna mtu ana majina ya watu waliochukuliwa ayamwage hapa tufanye uchunguzi wa kina.

Kwa mujibu wa barua ya malalamiko kwa DR.Kashishilah Thomas majina ya waliomaliza NOV 2008 na hawana uzoefu hata wa miezi sita baadhi yao ni TUSAJINGWE,MUNGILE,CATHERINE MWIHULU,SALVATORY MKUDE,JOSEPHAT QORRO,MTAKI,EVARIST,JASMINI BABLIA,MORORO,WAMBURA,CATHELINE,IRINE,MWIHULA hao wote ni darasa moja wamehitimu NOV 2008.

UNAPOCHUKUA WATU WA DARASA MOJA KAMA WANA WEAKNESS BASI NI WOTE ILA UKIWEKA MCHANGANYIKO WANAWEZA KUJIFUNZA KWA WENZAO AU WAKAWAFUNZA WENZAO.

CHANZO CHENYEWE KUNA DADA MHITIMU WA ST.AUGUSTINE AMBAYE YUKO HR BUNGENI, AKISHIRIKIANA NA DAP NOMBO KWA BARAKA ZA DR.KASHISHILAH WAMEKUWA WAKIFANYA MAZINGAOMBWE HAYA KWA MUDA MREFU.
 
Kwa mujibu wa barua ya malalamiko kwa DR.Kashishilah Thomas majina ya waliomaliza NOV 2008 na hawana uzoefu hata wa miezi sita baadhi yao ni TUSAJINGWE,MUNGILE,CATHERINE MWIHULU,SALVATORY MKUDE,JOSEPHAT QORRO,MTAKI,EVARIST,JASMINI BABLIA,MORORO,WAMBURA,CATHELINE,IRINE,MWIHULA hao wote ni darasa moja wamehitimu NOV 2008.

UNAPOCHUKUA WATU WA DARASA MOJA KAMA WANA WEAKNESS BASI NI WOTE ILA UKIWEKA MCHANGANYIKO WANAWEZA KUJIFUNZA KWA WENZAO AU WAKAWAFUNZA WENZAO.

CHANZO CHENYEWE KUNA DADA MHITIMU WA ST.AUGUSTINE AMBAYE YUKO HR BUNGENI, AKISHIRIKIANA NA DAP NOMBO KWA BARAKA ZA DR.KASHISHILAH WAMEKUWA WAKIFANYA MAZINGAOMBWE HAYA KWA MUDA MREFU.

Violation of effin privacy.
 
Tunawasihi Watz kupiga filimbi mapema kuzuia upendeleo kama huu!

This will be one case of Preventive Mitigation Strategy kupunguza corruption ktk ajira!

Tz ajira nyingi ni Technical Know 'who' !!!

Ila filimbi ya faulu ikipigwa mapema basi hii yaweza kupunguzwa na kuwa objective and fair to recruit according to technical 'know how'!!

Aluta Continue!!
 
Na hili ndilo tatizo la wahitimu wa Tanzania, wote wanataka kufanya kazi za kuajiriwa... ona sasa vyuo vingine vinavyonyanyapaliwa!

Elimu ya kujitegemea iko wapi?

Mnakumbulka shairi hili?

Tumeizika elimu, elimu ya kizamani
Elimu ile haramu, maana ya kikoloni
Imetuishia hamu, kuiga ya ugenini
Elimu yetu ya sasa, yawafaa wananchi

Kama ni kweli elimu yetu ya sasa yatufaa wananchi, kilio cha kuajiriwa kinatoka wapi?
 
ST.Augustine hawako juu kuwashinda UDSM au Tumaini University.waliochukuliwa wana kiwango kidogo cha kufaulu.nimebahatika kuona vyeti vya walioachwa na waliopita kwenye interview,wameachwa wengi wenye uzoefu na uwezo.mfano sharti la kazi lazima uwe una uzoefu wa miaka miwili hao wa ST.AUGUSTINE hata mmoja hana sifa hiyo.huwezi kuchukua watu wa darasa moja Hansard Repoter wameitwa watu 15 kwenye interview na wa ST.AUGUSTINE wako 14. nafasi zinazotakiwa ni saba.ST.Augustine hawawezi kuwa juu ya UDSM hata kwa nini.inaonekana wewe ni mmoja ya hao walioitwa kwenye Interview wakiwa wahitimu wa ST.Augustine utasema vipi majungu wakati Hard Facts zipo na unapewa.

Hapa sioni tatizo kabisa.
Mimi mwenyewe nime apply kwenye kazi ambayo requirement ikisema experience miaka mitano ,tena nikiwa mwanafunzi na nimeitwa na makapuni makubwa na nikiwa short listed baadhi ya makapuni hayo ni ALCATEL-LUCENT,Atos origin n.k.

Na kiwango cha kufaulu wajili wajanja hawaangalii sana wanachoangalia je nini unakifahamu kuhusiana na kazi waliyokuitia.Pia experience mwajuwa je? hawo jamaa hawana experience?? kumaliza shule 2008 si kigezo kabisa.

Mtu iga first class yako andika CV yako shagharabala nenda kwenye interview ushindwe kuwakilisha uone jinsi utakavyopigwa bao na watu wa third class.

Hapa kwa kweli mimi sioni hoja mpaka hapo baadae mtakapotumwagia data za uhakika
 
Violation of effin privacy.
Hakuna violation ya privacy kwani vyombo vyote vya habari vinazo copy ya malalamiko haya. mimi nimefanikiwa kupata kopi kwani niko kwenye chombo cha habari.
 
mimi sikatai watu wa darasa moja kuitwa kwenye interview haiwezekani,je wangekuwa wahitimu kutoka University of Dar-es-salaam ndio wameitwa kwenye hiyo interview pangekuwa na maneno?mimi naamini ST aguasyin University wako juu tuache majungu

Sipingi darasa zima kuitwa kwenye interview ila kama wana MERITS au sifa husika cha ajabu creteria zilizowekwa za kuomba kazi hiyo hawana kama uzoefu wa miaka miwili.Nyegezi haiwezi kuifikia UDsm HATA iwe vipi?fuatilia UNIVERSITY LEAGUE TABLE kwa Africa utaona Udsm ina nafasi gani na Nyegezi hakuna anayeijua.
NYEGEZI haiwezi kupambana na Tumaini acha Udsm.labda ijipime na Kairuki au Bukoba University.
 
Back
Top Bottom