Bunge la Kenya lamuidhinisha Mchungaji wa Kanisa kuwa Mkuu wa Kitengo cha kupambana na kuzuia rushwa

shige2

JF-Expert Member
Oct 11, 2016
8,106
3,966
Katika tukio lisilo la kawaida Afrika Mashariki, Wabunge wa bunge la Kenya WAMEMUDHINISHA Mchungaji mstaafu Eliudi Wabukala kuwa ndiye Mkuu mpya wa kitengo cha kuzuia na kupambana na rushwa.

Hii inatokana baada ya MWANASHERIA Phillip Kinisu kuondolewa katika wadhifa huo kutokana na wizi wa shilingi 721 million za Kenya.

Rais alikuwa amepokea majina tatu ya walioibuka bora baada ya mahojiano. Rais wa Kenya akalichagua jina la huyo mchungaji lijadiliwe bungeni. Bunge likubali ama likatae uteuzi wake.

Lakini jambo la kushangaza wabunge wote kwa kauli moja wamekubaliana leo katika kikao rasmi cha bunge kuwa ni mtu atakayeweza kupambana na RUSHWA.
Inasemekana Huyu ni mtu wa pili wa DINI kushikilia Idara nyeti.
Mwingine ni GAVANA mkuu wa BENKI KUU ya Kenya ambaye ni Padri wa shirika la OPUS DEI.
Aliyeweza kufanya kazi nzuri sana
Swali Je watu wa DINI wanaweza kuwa msaada kwa serikali zetu za Afrika?
 
Kwani kwenye hizo teuzi dini ilikuwa mojawapo ya vigezo au walipendekezwa na hatimaye kupitishwa kutokana kufaulu michujo?
 
Hii inadhihirisha na inaonesha kuwa makanisa ni nyumba ya siasa na Ujasusi. Kwa maana no way stranger akaingizwa katika system kama hiyo from no where.

Ni lazima alikuwa one of them.
 
Back
Top Bottom