Bunge la 11 kuandika historia

Bunge la 11 kuandika historia

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,148
Reaction score
56,424
Rais Magufuli ametangaza tatehe 17/11 kuwa siku rasmi ya bunge la 11 kuanza kazi, bunge linalojumuisha pande mbili za muungano yaani Bara na Tanzania Zanzibar.

Lakini jambo la kushangaza bunge limeitishwa bila kufikia mwafaka wa wabunge wa JMT toka Zanzibar.

Endapo itatokea wabunge toka Zanzibar watakanyaga kapeti jekundu na kuapa bila kuchaguliwa ama kuteuliwa kwa maana uchaguzi wote wa Zanzibar umefutwa, basi bunge la Tanzania litakuwa limeandika historia mpya na pengine inaweza kuwa ajabu ya dunia kwa bunge kuapisha wabunge ambao uteuzi wao umetenguliwa na tume halali ya uchaguzi.

Jambo la msingi kabla ya rais kulihutubia bunge, atumie muda huu uliobaki hadi tarehe 17 kutatua tatizo lililopo.

Nawasilisha.
 
Jaji Lubuva alielezea kwamba uchaguzi wa Rais wa JMT na wabunge wa JMT kwa upande wa Zanzibar haujafutwa.
 
Jaji Lubuva alielezea kwamba uchaguzi wa Rais wa JMT na wabunge wa JMT kwa upande wa Zanzibar haujafutwa.
ZEC walisema haukuwa huru na haki idadi ya majina ilizidi, kwani kulikuwa na daftari mbili tofauti na wasimamizi tofauti na vituo tofauti?
 
Haya ni maajabu ya karne ase, yaani sijui dunia itatuonaje, yetu masikio na macho.
 
ZEC walisema haukuwa huru na haki idadi ya majina ilizidi, kwani kulikuwa na daftari mbili tofauti na wasimamizi tofauti na vituo tofauti?

ujifunze basi kufatilia mambo usiwe unakurupuka maana hiyo issue ishajadiliwa sana
 
Jaji Lubuva alielezea kwamba uchaguzi wa Rais wa JMT na wabunge wa JMT kwa upande wa Zanzibar haujafutwa.

hiii jamani sasa feki haihitaji kuwa na cheti tu cha sheria, mtu yule yule wakti ule ule, apige kura kwa wakti mmoja, muungano sawa zanzobar mbaya!! upiuuzi jaji , Jaji historia itakutsuta one day
 
ZEC walisema haukuwa huru na haki idadi ya majina ilizidi, kwani kulikuwa na daftari mbili tofauti na wasimamizi tofauti na vituo tofauti?

mkuu hao wamejitia upofu kwa makusudi hawawezi kukuelewa , aliyefuta amesema amefuta matokeo ya uchaguzi wa zanzibar .
 
Rais Magufuli ametangaza tatehe 17/11 kuwa siku rasmi ya bunge la 11 kuanza kazi, bunge linalojumuisha pande mbili za muungano yaani Bara na Tanzania Zanzibar.

Lakini jambo la kushangaza bunge limeitishwa bila kufikia mwafaka wa wabunge wa JMT toka Zanzibar.

Endapo itatokea wabunge toka Zanzibar watakanyaga kapeti jekundu na kuapa bila kuchaguliwa ama kuteuliwa kwa maana uchaguzi wote wa Zanzibar umefutwa, basi bunge la Tanzania litakuwa limeandika historia mpya na pengine inaweza kuwa ajabu ya dunia kwa bunge kuapisha wabunge ambao uteuzi wao umetenguliwa na tume halali ya uchaguzi.

Jambo la msingi kabla ya rais kulihutubia bunge, atumie muda huu uliobaki hadi tarehe 17 kutatua tatizo lililopo.

Nawasilisha.

Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unasimamiwa na NEC (Lubuva), Uchaguzi wa Raisi wa Zanzibar, Baraza la wawakilishi na Mashekha unasimamiwa na ZEC hivo tu Zec wamefuta uchaguzi wa sehemu inayowahusu yaani wa Baraza la wawakilishi, Rais na Mashekha tu.

Mwananchi wa Zanzibar hupiga kura 5 yaani (Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais wa Zanzibar, Wabunge wa JMT, Baraza la wawakilishi na Mashekha) wakati sisi tunapiga kura 3 nafikiri wazijua?

Tanzania Bara tukipiga kura tunapaka kidole kimoja ule wino lumaanisha tayari ushamaliza kazi ya kupiga kura, wakati Zanzibar wanapaka vidole viwili yaani ukipoga ya JMT Rais na wabunge unapaka kidole chake na Ukipiga Rais SMZ, Mashekha na Wawakilishi unapaka kidole chake ivo taratibu tofauti.


NB: NEC inaingia mpaka Zanzibar kusimamia uchaguzi wake wa wabunge wa JMT na RAIS wa JMT ndio ukomowake hapa, ZEC inaanza kwa Rais wa SMZ, Wawakilishi na Mashekha.

Wawakikishi wa Zanzibar hawaingii kwenye bunge la JMT
 
Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unasimamiwa na NEC (Lubuva), Uchaguzi wa Raisi wa Zanzibar, Baraza la wawakilishi na Mashekha unasimamiwa na ZEC hivo tu Zec wamefuta uchaguzi wa sehemu inayowahusu yaani wa Baraza la wawakilishi, Rais na Mashekha tu.

Mwananchi wa Zanzibar hupiga kura 5 yaani (Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais wa Zanzibar, Wabunge wa JMT, Baraza la wawakilishi na Mashekha) wakati sisi tunapiga kura 3 nafikiri wazijua?

Tanzania Bara tukipiga kura tunapaka kidole kimoja ule wino lumaanisha tayari ushamaliza kazi ya kupiga kura, wakati Zanzibar wanapaka vidole viwili yaani ukipoga ya JMT Rais na wabunge unapaka kidole chake na Ukipiga Rais SMZ, Mashekha na Wawakilishi unapaka kidole chake ivo taratibu tofauti.


NB: NEC inaingia mpaka Zanzibar kusimamia uchaguzi wake wa wabunge wa JMT na RAIS wa JMT ndio ukomowake hapa, ZEC inaanza kwa Rais wa SMZ, Wawakilishi na Mashekha.

Wawakikishi wa Zanzibar hawaingii kwenye bunge la JMT
Mkuu hayo yote nayajua na yanajulikana, mimi najaribu kujiongeza alipoishia Lubuva.

Inakuwaje mfano kwenye kituo kimoja idadi ya majina ya kumchagua mbunge yawe sahihi ila ya kumchagua mwakilishi yazidi wakati ni msimamizi huyo huyo na daftari lile lile limetumika?

Jamani tusiwe wepesi wa kukubali kila tunachoambiwa tuchanganye na zetu.
 
Bunge linaanza nadhani wakati mgumu sana yule mwanasheria wa serikali Masaju .
 
Mkuu hayo yote nayajua na yanajulikana, mimi najaribu kujiongeza alipoishia Lubuva.

Inakuwaje mfano kwenye kituo kimoja idadi ya majina ya kumchagua mbunge yawe sahihi ila ya kumchagua mwakilishi yazidi wakati ni msimamizi huyo huyo na daftari lile lile limetumika?

Jamani tusiwe wepesi wa kukubali kila tunachoambiwa tuchanganye na zetu.

Si hakika kama wanatumia daftari moja ila si kila anaweza kupiga kura za Rais wa SMZ na Baraza la wawakilishi na Mashekha anaweza kupiga za JMT
 
Si hakika kama wanatumia daftari moja ila si kila anaweza kupiga kura za Rais wa SMZ na Baraza la wawakilishi na Mashekha anaweza kupiga za JMT
Fahamu ZEC ni mawakala wa NEC kwa kura za wabunge na za rais wa JMT, Lubuva au NEC hawakwenda Zanzibar kuandikisha wapiga kura waliandikishwa na ZEC, daftari ni moja na wapigakura ni wale wale wasimamizi ni wale wale na vituo ni vile vile.
 
Rais Magufuli ametangaza tatehe 17/11 kuwa siku rasmi ya bunge la 11 kuanza kazi, bunge linalojumuisha pande mbili za muungano yaani Bara na Tanzania Zanzibar.

Lakini jambo la kushangaza bunge limeitishwa bila kufikia mwafaka wa wabunge wa JMT toka Zanzibar.

Endapo itatokea wabunge toka Zanzibar watakanyaga kapeti jekundu na kuapa bila kuchaguliwa ama kuteuliwa kwa maana uchaguzi wote wa Zanzibar umefutwa, basi bunge la Tanzania litakuwa limeandika historia mpya na pengine inaweza kuwa ajabu ya dunia kwa bunge kuapisha wabunge ambao uteuzi wao umetenguliwa na tume halali ya uchaguzi.

Jambo la msingi kabla ya rais kulihutubia bunge, atumie pmuda huu uliobaki hadi tarehe 17 kutatua tatizo lililopo.

Nawasilisha.

Wakati mwingine inabidi uulize badala ya kupotosha.uchaguzi uliofutwa ni wa Rais,,wawakishi na madiwani toka zanzibar.ule wa rais na bunge la muungano upo safi ndio mana wabunge wa cuf wa pemba wamo.watakao kosekana ni wabunge kama watano toka baraza la wawakilishi na hilo halitaharibu akidi
 
Si hakika kama wanatumia daftari moja ila si kila anaweza kupiga kura za Rais wa SMZ na Baraza la wawakilishi na Mashekha anaweza kupiga za JMT

Licha ya nani anasimamia uchaguzi, wapiga kura si walewale? Kila Mzanzibari anapiga kura ya JMT na SMZ lakini asiyemzanzibari akiwa Zanzibar anapiga tu ya JMT. Kwa mantiki hiyo, kama serikali imekubali kwamba uchaguzi ulikua na kasoro, chujio gani limetumika kujua na kujiridhisha kwamba huo uvunjwaji wa taratibu uliathiri tu SMZ?
 
Wakati mwingine inabidi uulize badala ya kupotosha.uchaguzi uliofutwa ni wa Rais,,wawakishi na madiwani toka zanzibar.ule wa rais na bunge la muungano upo safi ndio mana wabunge wa cuf wa pemba wamo.watakao kosekana ni wabunge kama watano toka baraza la wawakilishi na hilo halitaharibu akidi
Sawa ila swali langu dogo sana uchaguzi wa Zanzibar ulisimamiwa na vyombo viwili tofauti?

Mbona mnakwepa swali?
 
Back
Top Bottom