Bunge kuanzisha studio yake ya Matangazo

Bunge kuanzisha studio yake ya Matangazo

Wizara ya habari, utamaduni, wasanii na michezo ndio wizara ambayo kwa kushirikiana na wizara zingine (ajira, kazi na elimu) ingeweza kuweka mikakati ya kuongeza ajira na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo wa nje na ndani, ingewezekana kwa kiasi fulani kuweka mifumo ya kitaifa na kimataifa itakayowatoa vijana wa kitanzania kutoka katika upofu na umasikini wa fikra walio nao.

Lakini cha kusikitisha, waziri wa wizara hii, Nape Nnuye amejikita kwenye juhudi za kufungia vyombo vya habari vyenye mlengo tofauti na chama chake, kudhibiti uhuru wa habari na sasa anataka kutuletea kituko kingine. Kwamba kutakuwa na studio ya bunge itakayokuwa inarusha matangazo ya bunge, na vyombo vingine vya habari vitaruhusiwa tu kuchukua matangazo kutokea huko. Yaani hakutakuwa na uhuru wa kuchukua habari moja kwa moja kutoka bungeni isipokuwa kutokea kwenye studio ya bunge.
Hii yote inaashiria juhudi za Nape Nnauye kuwanyima watanzania taarifa halisi kutoka kwa wawakilishi wao waliowachagua.
Nape hataki watanzanua waone akina Tundu Lissu wanavyomfundisha sheria mwanasheria wa serikali anapojaribu kupindisha kanuni kwa ushabiki wa kichama ili kitumbua chake kisiingie mchanga. Anataka kuweka studio itakayoedit na kufuta baadhi ya matukio kwa faida anazojua yeye.

Kitu ambacho Nape Nnauye hajui au amesahau ni kwamba kwa kiwango cha teknolojia kilichopo sasa hivi, vifaa kama saa za mkononi, pete, kalamu, vifungo vya shati, bangili, hereni, na of-course simu za mkononi zinaweza kutumika kurekodi matukio na kuyarusha mitandaoni.
Anachokifanya Nape ni kuongeza matumizi ya internet na kunufaisha makampuni ya simu, kwa sababu wananchi wakishajua kwamba habari za bunge zinatengenezwa, na baadhi kufutwa, hawataamini vyombo vya habari, watahamia kwenye mitandao kuangalia uhalisia kama itakavyokuwa imerekodiwa na waliomo bungeni.

Kwa hiyo wazo la Nape, kama ni kutaka kuficha ushirikina wa bunge, limeshindwa kabla halijaanza kutekelezeka. Na vyombo vya habari vikitaka kupoteza 'credibility' kwa wananchi, vikitaka kukimbiwa na watazamaji viunge mkono akili hii ndogo ya Nape Nauye.

'Akili za kupambana na vikundi vya kisiasa wakati mtu ni waziri anayetakiwa kutumikia umma wote, haziwezi kusogeza mbele taifa hili'.

Nape aache, kupambana na vyombo vya habari vinavyoiweka serikali ya chama chake uchi. Apambane na tatizo la ajira kwa vijana, wizara yake ina jukumu hilo. Hapo ndipo anaweza kujenga 'legacy' yake kiuongozi. Other wise, ataendelea kuwa 'Nape Nauye'.
 
Just to remind you this. Adolf Hitler once said this 'If I can control the media, then I can control the State'. Ni wakati sasa serekali kufuatilia kwa makini hawa propagandists wanatumia media to tarnish the image or the positive actions taken by the current leadership to reshape the economic base of our motherland Tz.God bless Tz.
 
Wizara ya habari, utamaduni, wasanii na michezo ndio wizara ambayo kwa kushirikiana na wizara zingine (ajira, kazi na elimu) ingeweza kuweka mikakati ya kuongeza ajira na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo wa nje na ndani, ingewezekana kwa kiasi fulani kuweka mifumo ya kitaifa na kimataifa itakayowatoa vijana wa kitanzania kutoka katika upofu na umasikini wa fikra walio nao.

Lakini cha kusikitisha, waziri wa wizara hii, Nape Nnuye amejikita kwenye juhudi za kufungia vyombo vya habari vyenye mlengo tofauti na chama chake, kudhibiti uhuru wa habari na sasa anataka kutuletea kituko kingine. Kwamba kutakuwa na studio ya bunge itakayokuwa inarusha matangazo ya bunge, na vyombo vingine vya habari vitaruhusiwa tu kuchukua matangazo kutokea huko. Yaani hakutakuwa na uhuru wa kuchukua habari moja kwa moja kutoka bungeni isipokuwa kutokea kwenye studio ya bunge.
Hii yote inaashiria juhudi za Nape Nnauye kuwanyima watanzania taarifa halisi kutoka kwa wawakilishi wao waliowachagua.
Nape hataki watanzanua waone akina Tundu Lissu wanavyomfundisha sheria mwanasheria wa serikali anapojaribu kupindisha kanuni kwa ushabiki wa kichama ili kitumbua chake kisiingie mchanga. Anataka kuweka studio itakayoedit na kufuta baadhi ya matukio kwa faida anazojua yeye.

Kitu ambacho Nape Nnauye hajui au amesahau ni kwamba kwa kiwango cha teknolojia kilichopo sasa hivi, vifaa kama saa za mkononi, pete, kalamu, vifungo vya shati, bangili, hereni, na of-course simu za mkononi zinaweza kutumika kurekodi matukio na kuyarusha mitandaoni.
Anachokifanya Nape ni kuongeza matumizi ya internet na kunufaisha makampuni ya simu, kwa sababu wananchi wakishajua kwamba habari za bunge zinatengenezwa, na baadhi kufutwa, hawataamini vyombo vya habari, watahamia kwenye mitandao kuangalia uhalisia kama itakavyokuwa imerekodiwa na waliomo bungeni.

Kwa hiyo wazo la Nape, kama ni kutaka kuficha ushirikina wa bunge, limeshindwa kabla halijaanza kutekelezeka. Na vyombo vya habari vikitaka kupoteza 'credibility' kwa wananchi, vikitaka kukimbiwa na watazamaji viunge mkono akili hii ndogo ya Nape Nauye.

'Akili za kupambana na vikundi vya kisiasa wakati mtu ni waziri anayetakiwa kutumikia umma wote, haziwezi kusogeza mbele taifa hili'.

Nape aache, kupambana na vyombo vya habari vinavyoiweka serikali ya chama chake uchi. Apambane na tatizo la ajira kwa vijana, wizara yake ina jukumu hilo. Hapo ndipo anaweza kujenga 'legacy' yake kiuongozi. Other wise, ataendelea kuwa 'Nape Nauye'.
duuh waliona hata tbc ikiacha basi wengine watatangaza....sasa hii studio ya bunge yenyew itakuwa haicost ela nyng kam tbc?
 
Huu ujinga wa kuendelea kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari kwani STARTV wakirusha live hizo pesa za kurusha matangazo zinawahusu nini CCM? Hatuwezi kukubali huo ujinga
 
Naona MCC imeanza kuwaingia. Uhuru wa kupata habari na demokrasia nchini.

Msumari uki ingia mnakuja na GIA mpya eti Oohh gharama ''studio mtaendesha bure? Je mitambo ya studio?''
 
Tumefika hapa tulipo kwa upuuzi wa ccm,tumefika hapa tulipo kwa udhaifu wa bunge
Jonh mnyika
 
Mkuu christopher umeongea nilichokua nafikiri big up mkuu...kula tano..shida za Watanzania ni studio ya Bunge akili ndogo sana huyu Waziri baada ya kutengeneza ajira kwa vijana yupo busy tuu bunge lichakachuliwe kuoneshwa anauzi sana..
 
Kuna kitu bado sijaelewa hapo alipodai kuwa kuna vigezo vitakavyotolewa na mamlaka hiyo vya kuzingatia.
Hapo kuna kitu kinatafutwa kuminywa
Huyu nape ni bonge la jipu kubwa kwenye utendaji wa shughuli za umma,yeye kazoea u vuvuzela wa ccm
 
Wakuu, sijui kama ni sahihi sana, lakini hata Bunge la Kenya lina kitengo cha Broadcasting....Parliamentary Broadcasting Unit. TV stations hurusha matangazo ya Bunge yanayoratibiwa na kitengo hiki..
 
Huyu nape ni bonge la jipu kubwa kwenye utendaji wa shughuli za umma,yeye kazoea u vuvuzela wa ccm
Anabebwa na mfumo huyu mkuu.
Wenyewe wanasema wanalipa fadhila kwa aliyoyafanya baba yake Mzee Nnauye wakati wa vita vya Kagera
 
Anabebwa na mfumo huyu mkuu.
Wenyewe wanasema wanalipa fadhila kwa aliyoyafanya baba yake Mzee Nnauye wakati wa vita vya Kagera
Daaaa,mbona nasikia nape asili yake ni kule mbeya?
 
Nimeshagundua. Hapa kinachotafutwa ni jinsi ya kuzidhibiti televisheni binafsi zilizojitolea kuonyesha live vikao vya bunge.

Ndiyo maana Nape anasema vituo binafsi vitachukua matangazo kutoka studio hiyo ya bunge. Yale yale ya kuonyeshwa vitu nusu nusu.
 
Anzisheni mtuoe ajira, sio muekane huko tena
 
Back
Top Bottom