Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO)

Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO)

Mimi ingawa ni mtu wa Kyerwa lakini nimewahi kufanya kazi serikalini hapo Bukoba na najua siasa za hapo Bukoba ....kwanza kwa location ya Bukoba ina advantage nyingi kuliko Mwanza ....Kagera ndio mkoa unaopakana kwa ukaribu na nchi nyingi tena nchi hizo miji yao mikuu ikiwa mbali kulinganisha na distance ya kufika Bukoba ......lakini Bukoba imeshindwa kuvutia wafanyabiashara wengi kutoka nchi jirani kutokana na vitu vingi ....nikipata wasaa nitaviainisha hapa ili serikali isaidie kuimarisha miji mikubwa ya mipakani inayoweza kuvutia biashara nyingi ...

Ni kweli mkuu, unajua Tz ni nchi yetu sote kwa kila kitu. Tutakushukuru kwa michango yako
 
Mheshimiwa mimi siyo mkazi wa Bukoba lakini nafika mara kwa mara hapo mjini kwa shughuli zangu binafsi nikitokea mkoani kwangu. Nashauri kama mtanzania mpenda maendeleo mjaribu kujadiliana kuhusu suala la kuihamisha stendi ya mabasi iliyopo hapo katikati ya mji maana ni ndogo sana na imezidiwa na wingi wa magari. Hii pia itasaidia kuutanua mji na kuongeza fursa. Nakutakia shughuli njema katika kuwalete maendeleo wananchi wako.

Swali halikulengwa kwangu ila naweza kuchangia: Ujenzi wa stendi kila kitu kilikuwa tayari sema ilibaki sehemu kidogo ili ujenzi uanze, kilichokuja kuharibu ni baada ya wanasiasa kulifanya suala la ujenzi kuwa la kisiasa.

Mbunge aliyemaliza muda wake na meya aliyemaliza muda wake kila mmoja kwa wakati wake alitaka kutumia mradi ule kujipatia sifa za kisiasa. Baada ya ugomvi patashika kati ya Amani na Kagasheki ule mradi ukashindikana kuanza.
 
Matatizo makubwa ya Bukoba ni MAJUNGU na FITINA, huu mji una watu hawataki kubadilika!, kazi kubwa ambayo mbunge unaweza kuifanya ni kubadili mind set za watu!
mfano:

1-walipoingia Pride na Finca, walipata tatizo kubwa la marejesho, lakini kwa sasa watu wanaweza kukopa na kurejesha, Lakini kuna baadhi ya miradi ya Kaghasheki kiukweli kuna watu wamekula pesa ya mikopo, wangekuwa na akili ya kukopa na kurejesha wangekuwa mbali sana.

2- kuwa na uwelewa kwamba ni muhimu mfanyabiashara akasajili biashara yake, kuna faida kubwa watu kuwa na biashara rasmi kuliko kuwa na fikra ya kukwepa kusajili kampuni,

3-watu waelimishwe kuwa pesa ya bure sio nzuri, pesa ya kutegemea kupewa na wanasiasa sio mzruri kabisa

4- mambo ya uchamachama yafe kabisa, kusema hawa ni wa ccm, hawa ukawa yafutwe kabisa.

5-watu waandae mpango mkakati unaohusu matatizo yao, ampapo kama mbunge utahitaji kuyawakilisha pindi bunge litakapo anza.
 
Kwanza nianze kwa kusema mimi ni mwanachama wa Chama Tawala. Hata hivyo muungwana ni vitendo hivyo hongera kwa kura zako kutosha kuwakilisha Watanzania wa Bukoba Mjini.

Nimesoma uzi wako na umenivutia nikaona nichangie kidogo kwani ni mdau wa mkoa huo ingawa sitoki jimbo lako.

Hongera sana kwa idea nzuri ya kujaribu kuleta maendeleo katika jimbo lako ambalo nadiriki kusema ndiyo icon ya mkoa wetu.

Huwa nasononeka sana napoona mkoa unaosifika Tanzania kwa kutoa "wasomi" lakini kimaendeleo hai-reflect ukweli huo (wadau wengi wameshaainisha changamoto hizo sina haja ya kuzirudia).

Nataka nishauri yafuatayo kwani sitaweza kuwepo siku hiyo:

1. Katika term yako ya ubunge jitahidi sana kuwa mbuge wa "Bukoba Mjini" na usiwe mbunge wa "Tanzania" kwani bado tunachangamoto nyingi sana jimbo lako na mkoa kiujumla. Pls usiwe kama yule mbunge wa mkoa flani ambaye yeye anaongelea ukombozi sijui uhuru dhidi ya polisi. Usijikite kwa sasa kwenye kutumbua majipu ya Taifa bali kuwa "mbinafsi" kidogo shughulika na majipu ya jimboni kwako kwanza.

2. Weka u-chama pembeni hasa kwenye mambo ya maendeleo utaweza kuvuta watu wengi sana kwenye mambo ya maendeleo hata kama mimi ambaye si wa upande wako kwenye kuchangia. Nimeona umesema kongamano limeandaliwa na mbunge na madiwani, sijui kama ni madiwani wa pande zote au wa upande wako tu Mh?

3. Naomba ikiwezekana mojawapo ya outputs ya hilo Kongamano iwe platform (kama ni ya social media au yoyote) ambayo hata watu ambao wako mbali na huko waweze kuwa wanatoa mawazo yao ya jinsi ya kuendeleza constituency yako ila overall goal iwe ya mkoa mzima.

4. Halafu kwa position yako hebu jaribu ku-verify account yako basi hapa Jamiiforums ili uongeze credibility.

Kila la kheri!
 
Mzee tatzo sio sherehe, nisome vzuri! Ulipaswa kuweka mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wananchi km mbunge. Sijaongelea sherehe hzo. Hata madiwani wengi baada ya kushnda walifanya sherehe lakn hilo halikuwazuia kupita kwa wananchi kuwashukuru.
Mbunge wangu usipokuwa mtu wa kupokea maoni ya watu wako mbeleni kuna tabu. Kagasheki kilichomuangusha ni hayo hayo ya kuamini kila anachofanya yy ni sahihi na hakuna mtu wa kumshauri.

Ni kweli mkuu, mie niliyegemea kwa vile alipokuwa anaomba kura aliweza kufanya mikutano mingi basi nikatarajia alivyopewa hizo kura angerudi kuandaa mkutano wa kuwashukuru wananchi. Luna tatizo moja, hawa viongozi bado wanahisi mnawawazia sana, wanalinga na wao w?nachukulia kila kitu ni watanikima, mimi ndiye, n.k. Kusema ukweli mtu wa hivi hatambui hata kwanini yuko pale, ni kukosa maadiri pia, unawafundisha nini wenzio? Lakini niliwahi kusikia, kwamba huyu na yule wa CCM wao ni watu wa show tu, anataka tu amshinde mwenzie basi ( prestige).

Kwake akishamshinda mwenzie na akaweka mikogo basi mambo ya jimbo ni mengineyo, kama hilo lina ukweli basi wananchi kazi mmejipa wenyewe ( ekibi okizara ).
 
Ebu kwanza changamkenı wabunge wote wa Bukoba ipatıkane dawa ya ugonjwa wa MNYAUKO kwa migomba.Matatizo kama haya yakitokea Kilimanjaro haichukui round yanatatuliwa,BK sasa miaka karibia 10,migomba imeisha na ndızi hakuna.Alafu ya Bukoba nı ndızı na Kahawa.Achana mambo ya ubishıbishi,kuwenı wajanja,dawa lazima serikali inunue dawa!
 
Hakika mbunge wetu umeanza vizuri sana kwa kuitisha hili kongamano as a brainstorming forum. Tutajitahidi kuja na ni vema ikawa annual event. Ni vizuri pia tukasahau mabaya yaliyopita kwa kufungua ukurasa mpya kwenda mbele. Wish you all the best.
 
aisee ondoa kwanza mivumbi yote ya stand, viooo viwe safi, magari yawe kwenye mpangilio unaooeleweka.
 
Ebu kwanza changamkenı wabunge wote wa Bukoba ipatıkane dawa ya ugonjwa wa MNYAUKO kwa migomba.Matatizo kama haya yakitokea Kilimanjaro haichukui round yanatatuliwa,BK sasa miaka karibia 10,migomba imeisha na ndızi hakuna.Alafu ya Bukoba nı ndızı na Kahawa.Achana mambo ya ubishıbishi,kuwenı wajanja,dawa lazima serikali inunue dawa!

Jikite na Bukoba Yetu mkuu. Mie nawashauri kupitia mbunge na watendaji wa idara ya kilimo na wakufunzi kutoka kituo cha Maruku wakajifunze nchi Jirani Uganda ni vipi wao migomba inastawi kule. Hii haingii akirini kabisa, kutoka Bkb - Uganda ni 100km tu lakini hakuna safari za mafunzo juu ya kilimo bora cha migomba. Katika hili hata kiutamaduni na kijiografia kati ya mkoa wa Kagera na Uganda ni karibu sawa, sasa iweje jirani yenu ale ashibe na kwako ufe na njaa? Rai yangu, chini ya watendaji mbunge aandae safari ili watu wakajifunze pale Uganda, hili tatizo linatatulika.
 
JINSI BUKOBA ILIVYOULIWA UCHUMI MAKUSUDI

Bukoba kwa hakika iliuliwa na kukumbatia sana chama tawala, nakumbuka, Nikiwa nasoma Mugeza sekondari chama kikuu cha Kahawa KCU kilitengana na Karagwe coperative, ambapo Karagwe walikuwa wazalishaji wazuri wa kahawa, baada ya utengano kukatokea mambo ya kisiasa kuingia kwa vyama vingi 1992, baadhi ya wakurugenzi walikuwa makada watiifu wa chama tawala jambo ambalo waliikopesa ccm fedha za kufanya uchaguzi enzi zile mil. mia tano, chama kikayumba kweli, chama kikaanza kuuza magari yake , chama kikashindwa kuwa na rudhuku, kilishindwa kusuply madawa ya kuua wadudu kama vile ddt hivyo zao hilo likafa watu wakaanza kuing'oa mikahawa, hivyo uzalishaji ukapungua, KCU ikafunga shule zake zote baadhi ikaziuza, ndio ukawa mwanzo wa umaskini wa mkoa huu, shule za balimi ambazo zilikuwa zinaendeshwa kwa kutegemea mfuko wa chama zote zilikufa, kumbuka hizi shule zilikuwa zinahudumia wanafunzi elfu sita mpaka kumi, nakumbuka Shule ya Kishoju iliwahi kutoa wafunzi bora mwaka 1991 High Level mpaka ikapelekea Askofu Timanywa kuwakataza walimuMapadre) ambao walikuwa wanatoka rubya kwenda kufundisha Kishoju, mambo haya yalitokea kiwivu zaidi.

Bukoba sasa hivi ina majanga mengi ndio maana siku hizi haitoi wanafunzi bora wenye vipaji, kwa kuwa, kwanza mlo umekuwa wa shida, kulikuwepo maziwa mengi hadi majirani hawayauzi unapewa tu, leo hii ng'ombe hakuna, walikufa sana kutona na magonjwa nyemelezi baada ya serikali ya ccm kushindwa kuhudumia majosho, kushindwa kuwalipa bwana mifugo, huu mpango unaonekana kusukwa makusudi kupunguza akili za wahaya, sasa hivi kulipoingia biashara ya samaki, BK hakuna mboga tena zaidi ya kula mapanki, akili haiwezi kutokea kwa kula mlo wa kunusa mboga, dagaa zimekuwa kimbilio baada hata maharage ya mjunza kukosa , sasa hivi hakuna mbolea , migomba hipo hipo tu haina lishe, watu walitegemea (bushunga) mabaki ya kahawa baada ya kubanguliwa. Sasa hivi bukoba inabidi kujipanga upya kutokomeza roho mbaya(kutendelana) kwa watu wote, ukianzisha kitu kizuri unakwamisha makusudi ili usionekana una mawazo bora ya kimaendeleo.
 
Ni kweli mkuu, mie niliyegemea kwa vile alipokuwa anaomba kura aliweza kufanya mikutano mingi basi nikatarajia alivyopewa hizo kura angerudi kuandaa mkutano wa kuwashukuru wananchi. Luna tatizo moja, hawa viongozi bado wanahisi mnawawazia sana, wanalinga na wao w?nachukulia kila kitu ni watanikima, mimi ndiye, n.k. Kusema ukweli mtu wa hivi hatambui hata kwanini yuko pale, ni kukosa maadiri pia, unawafundisha nini wenzio? Lakini niliwahi kusikia, kwamba huyu na yule wa CCM wao ni watu wa show tu, anataka tu amshinde mwenzie basi ( prestige). Kwake akishamshinda mwenzie na akaweka mikogo basi mambo ya jimbo ni mengineyo, kama hilo lina ukweli basi wananchi kazi mmejipa wenyewe ( ekibi okizara ).

Nadhani ushauri kaupata. Km hatasikilza atajuta labda km atajitoq ktk siasa. Watu wanamchora tu. Ss tuliokuwa mashabiki wake ndo tuko tunapondwa. Swala la kuandaa mkutano wa hadhara kuwashukuru wananchi lilikuwa jambo la msngi xana ila yy baada ya kupata ubunge kasepa Dar. Swez kuandka mengi kwa heshima yake na ya Chama chetu.

Tushirikiane kuijenga Bukoba yetu. Aache "kwebona" ili tuondoe makundi ya uchama. Bukoba ni yetu sote. Nina imani manispaa itapga hatua kubwa kimaendeleo maana meya na mbunge ni kutoka Ukawa. Tusije kuleta vsngzio baada ya manispaa kudorora.

Tuanze na stendi ya Bukoba maana ni aibu.

Elimu imedorora xana.

Tuna imani mbunge atafanya kazi kubwa na kwa weledi na kushirikiana na wananchi kuleta maendeleo Bukoba.
 
Mheshimwa Mbunge tunashukuru kwa kitu bomba ulichokuja nacho umeangalia mbali na mapema bila kupoteza mda...kwani whatever the case mkoa wa kagera ni wetu woote mwisho wa siku tukiondoka tutarudishwa uko no matter where we are , what we are doing right away. Wewe ulikuwa kama mmoja wa wabunge machachari katika bunge la 2005 na watanzania wengi wanakukumbuka tunaomba motto ule ule kwa stahili ile ile ulisaidie taifa letu hasa mkoa wetu wa kagera.Tayari umepewa Mr. Mwijage waziri nakusihi kwa kupitia wanakagera mfanye kazi kwa pamoja kama wafanyavyo wenzetu wa kilimanajaro kama ni tofauti ziwe kwenye makaratasi ya vyama tu...mwisho naomba uaagalie ni jinsi gani unaweza ukatushirikisha sisi wahayabongodar es salaam kusudi na sisi tuweze kuchangia katika huo mjadala I can tell u pamoja na kuwa mbali na mko wetu ila kwa wingi wetu na ukijitahidi kuwashirikisha wenzako wa ccm mkatukusanya hapa dar utashangaa utakachokipata...Hongera saana jembe
 
Safi Sana Mh.Mbunge,
Nashauri wale wiliopo mbali wapate fursa ya kuangalia na kusikiliza kwa kushiri online.
Tupo Pamoja
 
Sasa na wewe ndugu umekosa cha kumwambia mbunge wako? yeye kakutaarifu juu ya conference itakayojadiri namna ya kuiendeleza Bk, halafu wewe umebakia kusisitiza eti afanye mkutano kuwashukru wapiga kula wake; hiyo ni sawa lakini jambo la maana kuliko yote ni yeye mbunge kutimiza ahadi alizoahidi kwenye kampein zake; huduma bora na rahisi kwa wanabukoba mfano: maji ya kutosha na salama ya kunywa; huduma bora za afya zenye garama nafuu ikiwemo kuweka ambulance zenye kukikidhi mahitaji; mazingira bora ya elimu, barabara bora za lami mjini Bk, mazibgira bora ya upatikanaji wa ajira kwa wanabukoba.Nadhani hayo akiwafanyia wanabukoba watafurahi na kumuenzi kwa kazi nzuri yaani hata asipoandaa mkutano wa kuwashukuru lakini akitimiza ahadi zake kwa wanabukoba bado watamchagua tu hata uchaguzi ujao; kinachotakiwa ni kuwatumikia wanachi kwa kutumiza yale ulowaahidi.
 
Ebu kwanza changamkenı wabunge wote wa Bukoba ipatıkane dawa ya ugonjwa wa MNYAUKO kwa migomba.Matatizo kama haya yakitokea Kilimanjaro haichukui round yanatatuliwa,BK sasa miaka karibia 10,migomba imeisha na ndızi hakuna.Alafu ya Bukoba nı ndızı na Kahawa.Achana mambo ya ubishıbishi,kuwenı wajanja,dawa lazima serikali inunue dawa!

Usijifanye hayawani, suala la mnyauko ni la kitaifa kupitia wizara ya kilimo na sio mbunge ndio anapaswa kutolea ufumbuzi.Tatifi zishafanywa kuhusu huo ugonjwa sasa hivi tunasubiria mrejesho na tiba.
 
Nadhani ushauri kaupata. Km hatasikilza atajuta labda km atajitoq ktk siasa. Watu wanamchora tu. Ss tuliokuwa mashabiki wake ndo tuko tunapondwa. Swala la kuandaa mkutano wa hadhara kuwashukuru wananchi lilikuwa jambo la msngi xana ila yy baada ya kupata ubunge kasepa Dar. Swez kuandka mengi kwa heshima yake na ya Chama chetu.

Tushirikiane kuijenga Bukoba yetu. Aache "kwebona" ili tuondoe makundi ya uchama. Bukoba ni yetu sote. Nina imani manispaa itapga hatua kubwa kimaendeleo maana meya na mbunge ni kutoka Ukawa. Tusije kuleta vsngzio baada ya manispaa kudorora.

Tuanze na stendi ya Bukoba maana ni aibu.

Elimu imedorora xana.

Tuna imani mbunge atafanya kazi kubwa na kwa weledi na kushirikiana na wananchi kuleta maendeleo Bukoba.

Hili la stand na soko ni zaidi ya vyote. Na wajaribu kuanza kupanua barabara za mjini kwa 4ways na kutengeneza mitaro mikubwa ili kuziba surface ya ule udongo mwekundu. Huu udongo unachafua sana hata vumbi lake ni hatari.
 
Wapendwa Ndugu, Wadau na Wazawa wa Bukoba,Kagera..

Nichukue fursa hii kuwakaribisha katika Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO) Kongamano litakalowapa fursa ya kuijadili na kuijenga Bukoba Mjini Tuitakayo.
Kongamano hili limeandaliwa na Mbunge & Baraza la Madiwani kutegemea kufanyika 27 Disemba 2015 saa tisa Jioni. (tutawajulisha juu ya ukumbi hivi karibuni).

JUKWAA HILI LITAAMBATANA NA YAFUATAYO:

-Mbunge na Baraza la Madiwani kuwasilisha mpango kazi wetu wa miaka mitano 2016-2020.
-Mwakilishi wa Halmashauri kuwasilisha Fursa za uwekezaji zilizoko Bukoba Mjini.
-Kuzijadili changamoto za wananchi na wazawa wa Bukoba Mjini ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
-Kuona ni namna gani wazawa wa Bukoba, Kagera walioko mbali wanaweza kushiriki katika maendeleo ya Bukoba Mjini.

BUKOBA MPYA TUTAIJENGA KWA KUWA NA UONGOZI SHIRIKISHI UTAKAOWAPA WANANCHI, WAZAWA NA WADAU FURSA YA KUSHIRIKI.

Kongamano hili haliko katika misingi ya uvyama,udini wala ukabila. Yeyote mwenye kutaka kuiona Bukoba Mjini ikisonga mbele kwa kasi anakaribishwa sana.
Tuendelee kuwasiliana kupitia ukurasa wangu wa Facebook: Wilfred Lwakatare na email: mbungebukoba2016@gmail.com au wilfredlwakatare@gmail.com

kufika kwenu ndiyo mafanikio yetu.

Wenu katika ujenzi wa Bukoba Mpya;
Wilfred M. Lwakatare
Mbunge Bukoba Mjini 2015-2020.

Mh. mbunge nikupongeze kwa initiatives ulizoanza nazo, nakuhakikishia kam? unaenda na hii spidi nina uhakika ndani ya miaka 2 tu utakuwa umeleta mafanikio makubwa sana. Kushiriki na wadau wa maendeleo na kuwa kiongozi wa vyama vyote na dini zote itakusaidia sana, ile miradi ya nyuma ifatilie, ongea na wahusika taratiibu na kwa unyenyekevu naamini itarudi na mkienda kwenye vikao ipitisheni ili ianze kwa kasi, katika miradi ya maendeleo msiweke uvyama mbele naamini utaleta maendeleo ambayo yatakufanya urudi 2020 ukiwa na heshima kuu
 
Wapendwa Ndugu, Wadau na Wazawa wa Bukoba,Kagera..

Nichukue fursa hii kuwakaribisha katika Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO) Kongamano litakalowapa fursa ya kuijadili na kuijenga Bukoba Mjini Tuitakayo.
Kongamano hili limeandaliwa na Mbunge & Baraza la Madiwani kutegemea kufanyika 27 Disemba 2015 saa tisa Jioni. (tutawajulisha juu ya ukumbi hivi karibuni).

JUKWAA HILI LITAAMBATANA NA YAFUATAYO:

-Mbunge na Baraza la Madiwani kuwasilisha mpango kazi wetu wa miaka mitano 2016-2020.
-Mwakilishi wa Halmashauri kuwasilisha Fursa za uwekezaji zilizoko Bukoba Mjini.
-Kuzijadili changamoto za wananchi na wazawa wa Bukoba Mjini ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
-Kuona ni namna gani wazawa wa Bukoba, Kagera walioko mbali wanaweza kushiriki katika maendeleo ya Bukoba Mjini.

BUKOBA MPYA TUTAIJENGA KWA KUWA NA UONGOZI SHIRIKISHI UTAKAOWAPA WANANCHI, WAZAWA NA WADAU FURSA YA KUSHIRIKI.

Kongamano hili haliko katika misingi ya uvyama,udini wala ukabila. Yeyote mwenye kutaka kuiona Bukoba Mjini ikisonga mbele kwa kasi anakaribishwa sana.
Tuendelee kuwasiliana kupitia ukurasa wangu wa Facebook: Wilfred Lwakatare na email: mbungebukoba2016@gmail.com au wilfredlwakatare@gmail.com

kufika kwenu ndiyo mafanikio yetu.

Wenu katika ujenzi wa Bukoba Mpya;
Wilfred M. Lwakatare
Mbunge Bukoba Mjini 2015-2020.

HIZI PESA ; MBUNGE ZITAFUTWE NANI KAZIPEWA NA ANGELA MARKEL ZIMEFANYA KZI GANI ??????????



Jambo-Bukoba-Merkel.jpg


17. Juni 2015: Jambo Bukoba wird im Bundeskanzleramt f?r sein soziales und zivilgesellschaftliches Engagement mit einem von sieben Bundespreisen ausgezeichnet.
Im Vorfeld hatten sich ?ber 300 Initiativen aus Deutschland f?r den startsocial-Wettbewerb 2014/15 beworben. Als eine von lediglich 100 sozialen Organisationen erhielt Jambo Bukoba das begehrte startsocial-Beratungsstipendium um sich mit Experten-Know-how weiterzuentwickeln.
25 Initiativen, darunter auch wir, schafften es nach der viermonatigen, erfolgreichen Beratungsphase in die Bundesauswahl.
In die engere Wahl f?r die Endrunde in Berlin kamen nach Angaben von startsocial vor allem Konzepte, die durch ihre gesellschaftliche Relevanz und Wirksamkeit ?berzeugten und die w?hrend der Beratungsphase die gr??ten Fortschritte erzielten.
Jambo Bukoba unter den besten sieben in Deutschland Als eines von sieben herausragenden Projekten wurden wir mit einem Geldpreis ?ber 5.000 Euro ausgezeichnet. Es ist eine gro?e Ehre und eine tolle Auszeichnung f?r uns und unsere Arbeit f?r Kinder in Tansania.
Angela Merkel, Bundeskanzlerin und Schirmherrin der Veranstaltung, signierte sogar unseren Fu?ball im Jambo-Bukoba-Design.


 
Back
Top Bottom