Wilfred Lwakatare
Member
- Dec 10, 2015
- 22
- 70
Wapendwa Ndugu, Wadau na Wazawa wa Bukoba,Kagera..
Nichukue fursa hii kuwakaribisha katika Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO) Kongamano litakalowapa fursa ya kuijadili na kuijenga Bukoba Mjini Tuitakayo.
Kongamano hili limeandaliwa na Mbunge & Baraza la Madiwani kutegemea kufanyika 27 Disemba 2015 saa tisa Jioni. (tutawajulisha juu ya ukumbi hivi karibuni).
JUKWAA HILI LITAAMBATANA NA YAFUATAYO:
-Mbunge na Baraza la Madiwani kuwasilisha mpango kazi wetu wa miaka mitano 2016-2020.
-Mwakilishi wa Halmashauri kuwasilisha Fursa za uwekezaji zilizoko Bukoba Mjini.
-Kuzijadili changamoto za wananchi na wazawa wa Bukoba Mjini ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
-Kuona ni namna gani wazawa wa Bukoba, Kagera walioko mbali wanaweza kushiriki katika maendeleo ya Bukoba Mjini.
BUKOBA MPYA TUTAIJENGA KWA KUWA NA UONGOZI SHIRIKISHI UTAKAOWAPA WANANCHI, WAZAWA NA WADAU FURSA YA KUSHIRIKI.
Kongamano hili haliko katika misingi ya uvyama,udini wala ukabila. Yeyote mwenye kutaka kuiona Bukoba Mjini ikisonga mbele kwa kasi anakaribishwa sana.
Tuendelee kuwasiliana kupitia ukurasa wangu wa Facebook: Wilfred Lwakatare na email: mbungebukoba2016@gmail.com au wilfredlwakatare@gmail.com
kufika kwenu ndiyo mafanikio yetu.
Wenu katika ujenzi wa Bukoba Mpya;
Wilfred M. Lwakatare
Mbunge Bukoba Mjini 2015-2020.
Nichukue fursa hii kuwakaribisha katika Bukoba Municipal Developmental Conference (BUMUDECO) Kongamano litakalowapa fursa ya kuijadili na kuijenga Bukoba Mjini Tuitakayo.
Kongamano hili limeandaliwa na Mbunge & Baraza la Madiwani kutegemea kufanyika 27 Disemba 2015 saa tisa Jioni. (tutawajulisha juu ya ukumbi hivi karibuni).
JUKWAA HILI LITAAMBATANA NA YAFUATAYO:
-Mbunge na Baraza la Madiwani kuwasilisha mpango kazi wetu wa miaka mitano 2016-2020.
-Mwakilishi wa Halmashauri kuwasilisha Fursa za uwekezaji zilizoko Bukoba Mjini.
-Kuzijadili changamoto za wananchi na wazawa wa Bukoba Mjini ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
-Kuona ni namna gani wazawa wa Bukoba, Kagera walioko mbali wanaweza kushiriki katika maendeleo ya Bukoba Mjini.
BUKOBA MPYA TUTAIJENGA KWA KUWA NA UONGOZI SHIRIKISHI UTAKAOWAPA WANANCHI, WAZAWA NA WADAU FURSA YA KUSHIRIKI.
Kongamano hili haliko katika misingi ya uvyama,udini wala ukabila. Yeyote mwenye kutaka kuiona Bukoba Mjini ikisonga mbele kwa kasi anakaribishwa sana.
Tuendelee kuwasiliana kupitia ukurasa wangu wa Facebook: Wilfred Lwakatare na email: mbungebukoba2016@gmail.com au wilfredlwakatare@gmail.com
kufika kwenu ndiyo mafanikio yetu.
Wenu katika ujenzi wa Bukoba Mpya;
Wilfred M. Lwakatare
Mbunge Bukoba Mjini 2015-2020.