EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,356
KASHIFA nzito imeikumba Hospitali ya rufaa ya Bugando ya Jijini Mwanza baada ya kudaiwa kumtimua Mgonjwa wake ambaye ameozea Wodini hapo na sasa anaendelea kuoza akiwa nyumbani kwa mganga wa tiba za asili. Aliyetimuliwa Hospitalini hapo ni Joseph Luhogola (38),mkazi wa Kitongoji cha Nyabugera,Kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato katika Mkoa wa Geita.
Luhogola alipokelewa Hospitalini hapo Apr 22 mwaka huu akitokea katika Hospitali ya Wilaya ya Chato ikiwa ni saa chache baada ya kupata ajali. Ajali hiyo ilitokea Apr 22 katika Kijiji cha Lubambagwe Wilayani Chato,ambapo gari aliyokuwa ameipanda Luhogola aina ya Hiace akitokea Geita kwenda Mganza ilipofika eneo hilo na kupinduka baada ya kuchomoka gurudumu la mbele na baadaye la nyuma.
Kufuatia ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 7 mchana, Luhogola huku akiwa amepoteza fahamu alikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato ambako hata hivyo alipatiwa huduma ya kwanza kabla ya kuchukuliwa na gari la Hospitali hiyo hadi Bugando. Kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando alipokelewa na kulazwa wodi E namba 803 ambayo ni ya wanaume iliyoko katika ghorofa la 8 kwenye majengo ya Hospitali hiyo.
Hata hivyo imeelezwa kuwa,baada ya madaktari kuchunguza afya yake ilibainika kuwa alikuwa na tatizo la uti wa mgongo na alishauriwa kulala chali muda wote kama tiba ya tatizo alilokuwa nalo. Wakati wote akiwa Wodini hapo, mke wake Keflini Kafaransa(36) alikuwa akizuiwa kukaa wodini kwa mumewe kwa alichoelezwa sheria za Hospitali hiyo haziruhusu mwanamke kukaa kwenye wodi ya wanaume kwa muda mrefu.
Kutokana na hali hiyo, Kafaransa alilazimika kumtafuta shemeji yake Hatari Petro(21)ambaye ni mdogo wa Luhogola na ndiye aliyechukua jukumu la kumuuguza kaka yake huyo kuanzia Apr 28 hadi anatimliwa kwenye hospitali hiyo. Akisimulia mkasa huo,Luhogola ambaye kwa sasa yu mahututi nyumbani kwa mganga wa tiba za asili za mifupa katika Kitongoji cha Elimu,Kijiji cha Nyankumbu Wilayani Geita alisema hakutegemea kama Hospitali kubwa kama Bugando ingeweza kumuaga akiwa katika hali hiyo.
Luhogola ambaye kwa sasa amepooza kuanzia kifuani hadi miguuni anadai kuwa, iwapo angejua hayo yangetokea angewashauri ndugu zake wasimpeleke kwenye Hospitali hiyo kwa kuwa tatizo alilonalo la kuoza makalio yake lilisababishwa na wauguzi.
Joseph Luhogola (38),mkazi wa Kitongoji cha Nyabugera,Kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato katika Mkoa wa Geita akiwa amelala nyumbani kwa mganga wa tiba za asili Paul Chasama ambaye ni mtaalamu wa tiba za jadi kwa kuunga mifupa na kurudisha viungo vya mwili vilivyochengana ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Elimu,katika kijiji cha Nyankumbu Wilayani Geita amedai kuwa,kutokana na uzoefu kwenye kazi hiyo anao uhakika wa asilimia mia kwamba Luhogola atapona.
Baadhi ya watu wamedai iwapo mganga Chasama atafanikiwa kumponya kijana huyo aliyeoza makalio yake kama unavyoona pichani basi watalazimika kuwaondoa wagonjwa wao hospitali na kuwapeleka kwake.Picha zote na Victor Bariety-Geita
Kama umeguswa na habari hii ya kusikitisha wasiliana na mwandishi wa Malunde1 Blog mkoani Geita ndugu Victor Bariety kwa simu namba 0763 681 747 kwa ajili ya msaada kwa mgonjwa aliyeoza makalio ndugu Joseph Luhogola.
Chanzo;malunde1.blogspot.
Luhogola alipokelewa Hospitalini hapo Apr 22 mwaka huu akitokea katika Hospitali ya Wilaya ya Chato ikiwa ni saa chache baada ya kupata ajali. Ajali hiyo ilitokea Apr 22 katika Kijiji cha Lubambagwe Wilayani Chato,ambapo gari aliyokuwa ameipanda Luhogola aina ya Hiace akitokea Geita kwenda Mganza ilipofika eneo hilo na kupinduka baada ya kuchomoka gurudumu la mbele na baadaye la nyuma.
Kufuatia ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 7 mchana, Luhogola huku akiwa amepoteza fahamu alikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato ambako hata hivyo alipatiwa huduma ya kwanza kabla ya kuchukuliwa na gari la Hospitali hiyo hadi Bugando. Kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando alipokelewa na kulazwa wodi E namba 803 ambayo ni ya wanaume iliyoko katika ghorofa la 8 kwenye majengo ya Hospitali hiyo.
Hata hivyo imeelezwa kuwa,baada ya madaktari kuchunguza afya yake ilibainika kuwa alikuwa na tatizo la uti wa mgongo na alishauriwa kulala chali muda wote kama tiba ya tatizo alilokuwa nalo. Wakati wote akiwa Wodini hapo, mke wake Keflini Kafaransa(36) alikuwa akizuiwa kukaa wodini kwa mumewe kwa alichoelezwa sheria za Hospitali hiyo haziruhusu mwanamke kukaa kwenye wodi ya wanaume kwa muda mrefu.
Kutokana na hali hiyo, Kafaransa alilazimika kumtafuta shemeji yake Hatari Petro(21)ambaye ni mdogo wa Luhogola na ndiye aliyechukua jukumu la kumuuguza kaka yake huyo kuanzia Apr 28 hadi anatimliwa kwenye hospitali hiyo. Akisimulia mkasa huo,Luhogola ambaye kwa sasa yu mahututi nyumbani kwa mganga wa tiba za asili za mifupa katika Kitongoji cha Elimu,Kijiji cha Nyankumbu Wilayani Geita alisema hakutegemea kama Hospitali kubwa kama Bugando ingeweza kumuaga akiwa katika hali hiyo.
Luhogola ambaye kwa sasa amepooza kuanzia kifuani hadi miguuni anadai kuwa, iwapo angejua hayo yangetokea angewashauri ndugu zake wasimpeleke kwenye Hospitali hiyo kwa kuwa tatizo alilonalo la kuoza makalio yake lilisababishwa na wauguzi.
Joseph Luhogola (38),mkazi wa Kitongoji cha Nyabugera,Kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato katika Mkoa wa Geita akiwa amelala nyumbani kwa mganga wa tiba za asili Paul Chasama ambaye ni mtaalamu wa tiba za jadi kwa kuunga mifupa na kurudisha viungo vya mwili vilivyochengana ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Elimu,katika kijiji cha Nyankumbu Wilayani Geita amedai kuwa,kutokana na uzoefu kwenye kazi hiyo anao uhakika wa asilimia mia kwamba Luhogola atapona.
Baadhi ya watu wamedai iwapo mganga Chasama atafanikiwa kumponya kijana huyo aliyeoza makalio yake kama unavyoona pichani basi watalazimika kuwaondoa wagonjwa wao hospitali na kuwapeleka kwake.Picha zote na Victor Bariety-Geita
Kama umeguswa na habari hii ya kusikitisha wasiliana na mwandishi wa Malunde1 Blog mkoani Geita ndugu Victor Bariety kwa simu namba 0763 681 747 kwa ajili ya msaada kwa mgonjwa aliyeoza makalio ndugu Joseph Luhogola.
Chanzo;malunde1.blogspot.