Bugando hospital inatisha kwa PANYA na MENDE

Bugando hospital inatisha kwa PANYA na MENDE

Nyamwaga

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
454
Reaction score
118
Inasikitisha unapoingia katika kila ward unakutana na makundi ya panya na mende kila sehemu na hata wakati mwingine zinadhiriki kungata wagonjwa usiku hasa wale wanao kuwa wamezidiwa na hawajitambui.

Kwa kweli inasikitisha kuona hosp kubwa kama hii tena ya RUFAA inakuwa na hali kama hii na uongozi upo pamoja na serkali yake. Hii ni aibu kubwa hospital kugeuka kuwa kiwanda cha kuzalisha panya na mende.

Tunaomba uongozi wa hii hospital uwajibike ili kunusuru maisha ya wagonjwa.
 
Yaani maajabu ya hawa panya wanawinda sana wale wangonjwa wenye tatizo la mkojo na ambao sehemu zao za siri ziko nje nje na kuwangata bila huruma kana vile wamepata kitoweo. Na hata mchana hawaogopi watu wanaruka ruka juu ya vitanda.
 
Kichwa chako cha habari sio sahihi wapo ila sio kwa kiwango hicho unachosema cha kung'ata wagonjwa na kama ni hivyo basi kunamkono wa mtu hapo na wengine tunatoka nao nyumbani.
 
Usiwe mbishi kwa uhakika fika ujionee na sio kubisha. Hata manesi wanadai ni kero kwao kufanya huduma kwa wagonjwa na wakati mwingine wanawanyanganya dawa kwenye tololi.
 
Mjumbe unatafuta umaarufu hapa! Mm nimfanyakazi wa Hospitali Bugando sina takwimu zozote zibazosema kuna wagonjwa wameng'atwa na panya! Wagonjwa wote naututi wanalazwa ICU, wagonjwa wa Urology (wewe matatizo wa mikojo) huvaa nguo zao wanawekewa mipira tu sasa huyo panya wakuingia ndani ya nguo na kumng'ata mgonjwa huyo atakuwa sio panya! Sehemu kubwa kama Hospitali hii hawezi kukosekana panya ila sio wengi kama kama unavosema wewe umeongeza chumvi!!!!
 
Kwani hii Bugando si inapokea mabilioni ta Serikali? Sasa zinapelekwa wapi tena hata kushindwa kununua dawa ya kuangamiza hao dagaa pori?
 
Mjumbe unatafuta umaarufu hapa! Mm nimfanyakazi wa Hospitali Bugando sina takwimu zozote zibazosema kuna wagonjwa wameng'atwa na panya! Wagonjwa wote naututi wanalazwa ICU, wagonjwa wa Urology (wewe matatizo wa mikojo) huvaa nguo zao wanawekewa mipira tu sasa huyo panya wakuingia ndani ya nguo na kumng'ata mgonjwa huyo atakuwa sio panya! Sehemu kubwa kama Hospitali hii hawezi kukosekana panya ila sio wengi kama kama unavosema wewe umeongeza chumvi!!!!

Hilo la manesi kuporwa dawa na panya kwenye toroli unalizungumziaje?
 
Usiwe mbishi kwa uhakika fika ujionee na sio kubisha. Hata manesi wanadai ni kero kwao kufanya huduma kwa wagonjwa na wakati mwingine wanawanyanganya dawa kwenye tololi.

Weka picha mkuu,naona uongozi wa Bugando unakupinga
 
management hapo bugando imekaa kindugu,,wanachokitaka ndo wanakifanya kwa uchafu kweli ni chafu kuna matatizo chungu nzima pale.
 
Mpamba gozi hufutia kwake. Hakuna mgonjwa wa mkojo anayefaa suruali wala kabutula. Na hakuna kanuni inayosema hospital kubwa lazima iwe na panya. Kama we ni mfanyakazi kasome tena kanuni za afya.
 
Huna cha kuandika kwasababu huna data yoyote inasapoti unachokuandika!! Acha udaku kama hunachakuandika nakili hata mistari ya taarabu itakulipa!!
 
Usihangaike kutafuta ward ,ingia hodi hata no. 7 ujionee kwenye chumba cha wagonjwa wa uangalizi maalum na upande wa mashariki choo za wagonjwa hakuna taa giza la kufa mtu na manesi wanadai zina mwezi mzima haziwaki kuna short.
 
Huyu jamaa ni boga kweli hospital ya bugando isiwe na taa chooni??
Au umetumwa mkuu!!!
 
Mjumbe unatafuta umaarufu hapa! Mm nimfanyakazi wa Hospitali Bugando sina takwimu zozote zibazosema kuna wagonjwa wameng'atwa na panya! Wagonjwa wote naututi wanalazwa ICU, wagonjwa wa Urology (wewe matatizo wa mikojo) huvaa nguo zao wanawekewa mipira tu sasa huyo panya wakuingia ndani ya nguo na kumng'ata mgonjwa huyo atakuwa sio panya! Sehemu kubwa kama Hospitali hii hawezi kukosekana panya ila sio wengi kama kama unavosema wewe umeongeza chumvi!!!!

In kweli mkuu , hiyo ndiyo hali halisi niliishuhudia baada ya kulazwa kwa wiki tatu tena private ward. Jirekebisheni.
 
Hapa tunaongea kwa ushahidi! Kama unao weka kama huna wewe na mwenzako kaimbeni taarabu!!! MAJUNGU
 
Back
Top Bottom