Budgets za serikali zinakosa 'independent checks'

MovingForward

JF-Expert Member
Nov 10, 2009
489
49
Ninakumbuka vyema wakati wa Mwl Nyerere, rasimu za bajeti za Serikali zilikuwa zinapelekwa kwa wasomi na wataalamu, vikiwemo vyuo vikuu vyetu, hasa UDSM kupitiwa kabla ya kupelekwa bungeni. Lengo likiwa kupata independent inputs na ukosoaji kutoka kwa wataalamu walio nje ya wizara zinazoandaa bajeti. Utaratibu huu ulibadilika kipindi cha Mh Mwinyi. Hadi sasa. Nadhani haya ni matumizi mabaya ya wataalamu wetu ambao wapo tayari kujitolea kutoa maoni yao bureeeee pasipo kulipwa chochote, kwa maslahi ya taifa.

Kwa sababu ya bajeti hizi kukosa inputs za wataalamu, ndiyo maana kila wakati zinakuwa na ukosoaji mkubwa kutoka kwa wananchi. Wataalamu wetu, waliopo katika wizara husika wanaweza kuwa ni wazuri, lakini haiwazuii kufanya bajeti zenye mwelekeo wa wakubwa wao tu, hasa mawaziri. Kama bajeti hizi zingelikuwa zinapata inputs za wataalamu ambao ni independent, zingelikuwa zinabeba mahitaji na umuhimu halisi wa mahitaji ya nchi.

Tunapeleka bajeti Bungeni, sawa. Lakini je! ni wabunge wangapi ambao wanaouelewa wa kitaalamu kuchambua kwa kina bajeti hizi?? Kwa mfano; wakati wa kikao cha bajeti cha mwaka wa 2009/10; nilimwona kwenye TV moja, Mh Mbunge mmoja akitoa maoni akiifagilia bajeti, baada tu ya Mh Waziri wa fedha kuwasilisha hoja. Nilivutwa niingie kwenye tofuti ya Bunge la Jamhuri ya Muunganao wa Tz kuangalia CV ya Mh Mbunge huyo. Nilishangazwa kuona hakuna chochote wala lolote liliojazwa kuhusu taaluma yake. Kisha nikafuatilia, nikabaini inasemekana aliishia darasa la saba. Sasa kama ndani ya Bunge wataalamu wakuweza kuchambua bajeti zetu ni wachache, na wengi ndiyo kama hawa, na wakati huo huo kupita kwa bajeti ni kwa kura ya kutamka NDIYOOOOOOOOOOOO au SIYOOO, hapo tunategemea nini?.

Bajeti nyingi zitakuwa zinapitishwa tu kwa sababu wataalamu wetu watakuwa wakiziandaa kwa mazoea tu, na kukosa independent check ni ugonjwa!!. Lakini pia, tumeona BoT ambapo sehemu kubwa ya waajiriwa ni watoto wa vigogo!!! Nadhani huenda ikawa muundo wa ajira wa BoT unafanana na wizara zetu pia. Kwa hiyo, wataalamu wengi huenda wakawa ni watoto wa vigogo!! Hapo taaluma ni maswali, uzoefu ni maswali na independance ni maswali!!

Nadhani wakati umefika kwa serikali yetu kuwekeza katika wataalamu wetu badala ya wanasiasa tu!!! Wanasiasa wengi si wasomi waliobobea katika masuala ya kitaalamu. Hawawezi kutumulikia bajeti zetu ipasavyo!

Ni mawazo yangu hayo, ndugu watanzania wenzangu.
 
Wameshtuka wakiwa open sana watashtukiwa kwamba bajeti zenyewe ni za kuchonga tu na haziendani na mapato/matumizi halisi.

Hivi wewe unaamini huu mchezo wa kuigiza?
 
As far as I know budgetting means planning... but in Tanzania Budget means balancing expenditure game.
 
Mkuu

Wakati huo wa Nyerere hakukuwa na ubora wowote wa kuijadili budget, hafadhali sasahivi kidogo wasomi kiasi fulani niwengi bungeni, napia kunawataalam weng kwenye wizara kulinganisha wakati wa Nyerere, na pia sasahivi wataalam(independents) wetu wako free kuijadili na kuikosoa budget ya serikali.

Wakati wa Nyere niyeye mwenyewe kila kitu, haambiliki, wabunge wengi ni mbumbumbu, wasomi waliokua wanaijadili budget ilikuwa ni kiini macho.

Nakubali kabisa kuwa @more need to be done@ lakini usiturudishe wakati wa Nyerere ambao hakukuwa na mjadala bungeni wala kupinga mawazo yake, wasomi walikua waoga kumpinga mwalimu
Let us do it diferently but not to go back to medeivo Nyerere failure time.
 
Mkuu

Wakati huo wa Nyerere hakukuwa na ubora wowote wa kuijadili budget, hafadhali sasahivi kidogo wasomi kiasi fulani niwengi bungeni, napia kunawataalam weng kwenye wizara kulinganisha wakati wa Nyerere, na pia sasahivi wataalam(independents) wetu wako free kuijadili na kuikosoa budget ya serikali.

Wakati wa Nyere niyeye mwenyewe kila kitu, haambiliki, wabunge wengi ni mbumbumbu, wasomi waliokua wanaijadili budget ilikuwa ni kiini macho.

Nakubali kabisa kuwa @more need to be done@ lakini usiturudishe wakati wa Nyerere ambao hakukuwa na mjadala bungeni wala kupinga mawazo yake, wasomi walikua waoga kumpinga mwalimu
Let us do it diferently but not to go back to medeivo Nyerere failure time.

Haina maana kwamba turudi kwa Nyerere. Kwanza uelewe kwamba wakati ule focus ilikuwa ni Ujamaa na kujitegemea. Tunachohitaji hapa ni transparency na matumizi mazuri ya taaluma za wanazuoni wetu. Toa mfano wa wataalamu au institutions ambazo independently zimekuwa zikihusishwa katika ku-review budget!. Tunataka bajeti zilizokwenda shule, siyo kama hizi za akina Mramba za kubananishwa bungeni kwa sababu TZS 9 billion zote kazipeleka Rombo!!. Haya yote yanatokea kwa sababu mawaziri wanaoongoza wizara hizi wana- override budgeting process. Kuwa na uwazi zaidi wa budgeting process na kupata inputs kutoka kwa independent experts, kunaleta manufaa zaidi. Nchi kubwa kama Malekani, inatumia wataalamu, wasomi ambao ni independent na serikali, kuikosoa na kuishauri. Wewe unasema tunafanya vizuri kwa hili hapa TZ, MmmmmH.


Wataalamu ni wengi, ndiyo. Lakini ubora je!, independence ya kazi je!? let us think outside the box. Nani alikuambia au ni wapi uliko thibitisha kwamba nyerere alikuwa anapanga na kuamua bajeti ya nchi nzima, peke yake?!. Ndiyo, kulikuwa na mapungufu mengi katika utawala wake, lakini hili la kutumia independent checks & opinions ni jambo jema sana.

Usituambie watoto wa vigogo waliokuwa wamejazana BoT na qualifications hewa, kama haohao ndiyo wamejaa kwenye wizara zetu, wanaweza kutufanyia bajeti zinazokidhi mahitaji yetu ya nchi.

****************************************************
"The greatest loss on earth is failure to think appropriately".
"If you fail to plan you plan to fail"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom