Budget ya harusi...

Budget ya harusi...

Mr.Duttu

Member
Joined
Nov 7, 2015
Posts
91
Reaction score
57
Habari za majukumu ndugu zangu,

Leo nimekuja hapa kwenu kwaajiri ya kuweza kupata ujuzi [structure]na mwenendo mzima wa harusi sana sana ikiwa ni kwenye ku set budget ya harusi kwa kadri ya wa tu 300 mpka 450, naitaji kujua naweza kuwa na budget ya kiasi gani kuweza ku kidhi harusi na sherehe kwa idadi ya watu hao kwa makadilio, kwamtu mwenye experience na jambo hili naona maelezo kidogo.

Asanteni.
 
Hapo inategemea na mazingira kuanzia gharama za msosi kwenye mazingira hayo
 
Idadi ya watu pekee sio kigezo cha kujua bajeti halisi.
Kitu cha msingi ni aina ya sherehe harusi, mazingira ya sherehe na uwezo wa watu kiuchumi unaotaka kuwaalika.

Kwa harusi hizi za kimjini mjini kwa zama hizi, kwa idadi hiyo ya watu, wastani wa bajeti ya 10-15milioni inatosha. Ukitaka mbwembwe nyingi basi andaa 20+ milioni. Na ukiwa unataka sherehe ya harusi kufanyika kinyumbani, kijijini au kijamii, basi 5milioni au pungufu ya hapo inatosha sana
 
Idadi ya watu pekee sio kigezo cha kujua bajeti halisi.
Kitu cha msingi ni aina ya sherehe harusi, mazingira ya sherehe na uwezo wa watu kiuchumi unaotaka kuwaalika.

Kwa harusi hizi za kimjini mjini kwa zama hizi, kwa idadi hiyo ya watu, wastani wa bajeti ya 10-15milioni inatosha. Ukitaka mbwembwe nyingi basi andaa 20+ milioni. Na ukiwa unataka sherehe ya harusi kufanyika kinyumbani, kijijini au kijamii, basi 5milioni au pungufu ya hapo inatosha sana
Duh yani nichome million 20 kisa harusi? Ujinga huo sifanyi.

Bora niwachangishe ikifika hela nzuri nasepa kusikojulikana.
 
Unataka wale na kunywa nini? Na utatumia ukumbi gani? Wa kanisa au wa kukodi? Usafiri unataka wa aina gani, wa kukodi au ndugu na marafiki watajitolea?

Kwa watu zaidi ya 300 lazima wawe wamekuchangia na kuna kamati inahusika. Hivyo hakuna sababu ya wewe kuhangaika na maswala ya bajeti kamati itashughulikia.

Jambo la msingi wanakamati watakuambia kianzio cha mezani na ambacho kinaweza kuwa 2M. Halafu kwa watu hao 300 huenda watakaochangia ni 200 na 100 wataingia bure.
Na kwa watu 200 kwa hesabu ya haraka unaweza kukusanya mchango wa kati ya 20M na 30M. Na hii inategemea wewe unazungukwa na watu wenye uwezo kiasi gani, yaani marafiki na ndugu. Na hapo mavazi na gauni la harusi ni juu yako

Lakini kama pesa inatoka mfukoni mwako basi watu hata 60 wanatosha kwa bajeti ya 2M.

Ghalama za harusi inategemea wewe unataka iweje. Inawezakana hata kwa 1M
 
Nenda stationary kawaulize huwa wanaprint vitu kama hivyo na kuandika mambo hayo...chukua hata sampo moja upate muongozo

ila kuna mambo mengi mfano ukumbi uliokamilika, mavazi, chakula/Vinywaji, usafiri, gharama za MC, Muziki n.k

kutaja figure ya pesa kabisa inategemea na ulivyojipanga kwa kuzingatia vipengele nilivyotaja hapo juu
 
Oa kawaida tu Mwamba
Hawa akina Aisha na Mwajuma
Chukua tu kisela tia ndani
Uharibu 20M zote hizo

Unaonekana hata huna hela Mpk uje kuomba Ushauri huku Mitandaoni acha na hayo Maharusi ya Mbwembwe.
 
Back
Top Bottom