Breeding season?

Tegelezeni

JF-Expert Member
Dec 31, 2009
268
124
Bila shaka mtakubaliana na mimi kuwa hali ya hewa kuanzia mwezi wa Mei hadi huu Julai ni muafaka kwa watu kujamiiana na hivyo kuifanya miezi hiyo kuwa kama ndio breading season, especially kwa wakazi wa ukanda huu wa Pwani ikiwemo Dar.
Ukipita mahospitalini hivi sasa utakuta idadi ya wanawake wanaohudhuria kliniki imeongezeka kwa kiwango cha kutisha tofauti na miaka ya nyuma. Hii inadhihirisha ni kwa kiasi gani Watanzania wamepania kuongeza uzao kwa ajili ya kujihakikishia nguvu kazi haiyumbi hapa nchini.
Kwa mfano hapa JF inakadiriwa wanachama wake wanatarajia kupata watoto 1000 kwa kipindi cha miezi sita ijayo, idadi hiyo si haba na inaonyesha ni kwa kiasi gani wana JF wana mchango mkubwa katika kuzalisha nguvu kazi ili taifa lisiyumbe kiuchumi.
Hongereni sana
Akina%2Bmama%2Bwajawazito%2Bwakiwa%2Bwanaendelea%2Bkusubiri%2Bhuduma%2Bya%2Bkliniki%2Bkatika%2Bkituo%2Bcha%2Bafya%2Bcha%2BMbambabay%2Bambapo%2Bwamekuwa%2Bwakitumia%2Bzaidi%2Bya%2Bsaa%2B7%2Bkusubiri%2Bhuduma%2Bza%2Bafya.JPG

 
Back
Top Bottom