English Learner
JF-Expert Member
- Jan 1, 2012
- 366
- 453
....Na hapo ndo nampa heko JK kwa kucgeza karata na kulamba dume, kwa kuwaleta madingi hawa.
Ukarimu ulioje Wachina na Wamerekani watafanya kazi usiku na mchana, wakatwe kodi ili misaada itolewe kuleta maendeleo kwa Watanzania?! Kabla ya kutoa pongezi, kama unashughulisha akili yako hata kwa kiwango kidogo tu lazima ujiulize; Kati ya hawa wageni, Je kuna hata mmoja ambaye ujio wake kweli ilikuwa ziara ya matembezi au mapumziko ya kuja kukwea bembea kama wafanyavyo viongozi wetu? Kama kuna mikataba ya miradi ya kiuchumi imefanyika, je ni rasilimali za nani zimefunganishwa kwenye hiyo mikataba, Je, kuna rasilimali hata moja ambayo ni mali binafsi ya Ndugu Kikwete, Salma na wanawe; ambayo si ya wananchi wa Tanzania? Au je, rasilimali hiyo haikuwepo kabla katika ardhi ya Tanganyika kaileta Rais Kikwete? Ni vema kujua kwa nini watangulizi wake, akiwemo wa zama za hivi karibuni ambaye naye alikuwa mlafi hakufikia kiwewe cha sasa katika kuzifungua na kuziwekea fungani rasilimali zetu kwa pupa kubwa kama hii. Huwezi kupata neno bora zaidi ya uwendawazimu kwa mtu anayeshika hili na kabla hajakamilisha anaanzisha lile na kuacha hili likiwa bado halijapata muelekeo. Serikali ya Kikwete imekuwa kama vile imeambiwa baada ya 2015, vizazi vijavyo vitaletewa Tanzania nyingine yenye rasilimali tele, na kama haiwezi kuzimaliza sasa basi zitachacha! Kwa hiyo jukumu la serikali ya awamu yao ni kutapanya na kugawa kila kilichopo sasa. Kiwewe hiki ndicho kinafanya swali la nini kipaumbele cha maendeleo kwa uchumi wa Tanzania kuwa gumu kwa watunga sera wetu. Wakilala leo na MADINI, kesho wataamka na KILIMO KWANZA, keshokutwa watakuja na ELIMU KWANZA na mtondo watasahau watakuambia NISHATI KWANZA kabla hawajaota mchana na kusema AFYA KWANZA na mtondogoo wakakueleza MIUNDOMBINU KWANZA! Kwanza inatumika katika kila jambo jipya mpaka mwishowe kimantiki inasimama kumaanisha MWISHO-KWANZA.
I liked that part highlighted in purple!
Source: Nitatoa pongezi kwa Rais Kikwete nikijua undani wa Mikataba ya Marais Xi na Obama - wavuti.com