Habari wakuu,
Katika hali isiyo ya kawaida leo nimeenda tigo pesa kufanya muamala pesa niliokabidhiwa na mtu wangu wa karibu kama malipo ya jambo kwa mshangao mkubwa noti nilizotoa za elfu10 tatu dada wa tigo pesa akaniambia hizi fedha ni bandia na zipo nyingi kama hizi kwa Sasa nikajiuliza kweli ndugu yangu mimi naemjua anaweza kunipa ela bandia kwa hasira nikampigia simu nikihamaki ila mara mbili mbili nikinusa noti zina harufu ya fedha kwa hasira nikampigia mshkaji baada ya kumwambia kwa mshangao akaniambia skuizi na mimi ni mjinga ametoka ku draw pesa ATM mda sio mrefu kwahyo ATM sikuizi wanaweka fedha bandia. kiukweli sipo comfortable na hizi fedha kwa sasa mpaka nipate uhakika zaidi wa kuzitumia kwa usalama wangu.
Rai yangu kwa serikali kupitia wizara husika, Kama kweli hizi fedha ni halali nitoe wito na rai kwa serikali kupitia wizara husika naona ni vyema inabidi kabla ya kubadili kungekuwepo na utaratibu ili watumiaji wafahamu mabadiliko.
Na kama sio fedha halali basi serikali iwe makini kwenye hili maana huwezi kutofautisha kwa urahisi huu mfanano. Utofauti unaonekana kwa haraka kwenye utepe uliopita pembezoni kulia. N.B Angalia sign ya waziri&Gavana huenda there is changes.
View attachment 1408165
Sent using
Jamii Forums mobile app