Mwanamwana
Platinum Member
- Aug 1, 2011
- 9,602
- 22,707
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imewataka watanzania wanaopeana zawadi kwa njia ya kutunzana pesa taslimu katika sherehe mbalimbali nchini, waelekeze utaratibu huo kwa njia mifumo ya malipo ya kidijitali.
Hayo yamesemwa leo, Agosti 4, 2026 na Ofisa Mwandamizi (BoT) Fredriki Mwakuu, alipokuwa akifanya mahojiano na NipasheDigital, mkoani Dodoma.
Mwakuu amesema kuwa kwa sasa serikali ipo katika malengo ya kupunguza matumizi ya pesa taslimu.
“Tunaona sasa hivi watu mbalimbali hususani akinamama wana tabia za kutunzana katika sherehe na kupelekea pesa kumwagika chini, ile haiko sawa BoT tumejipanga kuandaa mwongozo maalum kuhusiana na hilo,” amefafanua
Mchambuzi Mwandamizi Mifumo ya Malipo ya Taifa (BOT) Doto Namkaa, amesema mifumo ya malipo imegawanyika katika malipo makubwa na madogo bila kujali matumiaji awe na akaunti yoyote kutoka benki.
Nipashe
Hayo yamesemwa leo, Agosti 4, 2026 na Ofisa Mwandamizi (BoT) Fredriki Mwakuu, alipokuwa akifanya mahojiano na NipasheDigital, mkoani Dodoma.
Mwakuu amesema kuwa kwa sasa serikali ipo katika malengo ya kupunguza matumizi ya pesa taslimu.
“Tunaona sasa hivi watu mbalimbali hususani akinamama wana tabia za kutunzana katika sherehe na kupelekea pesa kumwagika chini, ile haiko sawa BoT tumejipanga kuandaa mwongozo maalum kuhusiana na hilo,” amefafanua
Mchambuzi Mwandamizi Mifumo ya Malipo ya Taifa (BOT) Doto Namkaa, amesema mifumo ya malipo imegawanyika katika malipo makubwa na madogo bila kujali matumiaji awe na akaunti yoyote kutoka benki.
Nipashe