Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,481
- 14,858
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa ina mpango wa kuuza sehemu ya hifadhi yake ya dhahabu kwa ajili ya kufadhili miradi ya kimkakati ya serikali.
Akizungumza mkoani Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Masoko ya Fedha wa BoT, Emmanuel Akaro, amesema madai hayo si ya kweli.
Ameeleza kuwa kinachotekelezwa ni mpango wa kuuza dhahabu iliyozidi kiwango kilichoidhinishwa, kwa lengo la kusawazisha mizania ya hifadhi ya dhahabu ya benki hiyo.
Kwa mujibu wa Akaro, bodi ya BoT imeidhinisha benki hiyo kuwa na hifadhi ya dhahabu isiyozidi dola za Marekani bilioni mbili, wakati thamani ya sasa imefikia dola bilioni 3.24, hivyo kutokana na tofauti hiyo, benki inapanga kuuza kiasi kilichozidi kiwango kilichowekwa.
Amefafanua kuwa fedha zitakazopatikana kutokana na mauzo hayo zitawekezwa katika masoko ya fedha ya kimataifa kwa lengo la kuongeza mapato ya uwekezaji, na si kwa ajili ya kufadhili miradi ya serikali.
Akaro amesisitiza kuwa BoT ni chombo huru, na uamuzi wowote wa kutumia uwekezaji wake kufadhili miradi ya serikali unahitaji idhini ya Bunge.
Hadi jana Januari 29, 2026, BoT ilikuwa na akiba ya fedha za kigeni yenye thamani ya dola bilioni 6.52, na kati ya hizo, dhahabu inakadiriwa kuwa dola bilioni 1.2, dola za Marekani bilioni 3.8, na sarafu ya China (yuan) dola milioni 735.
Pia Soma
Akizungumza mkoani Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Masoko ya Fedha wa BoT, Emmanuel Akaro, amesema madai hayo si ya kweli.
Kwa mujibu wa Akaro, bodi ya BoT imeidhinisha benki hiyo kuwa na hifadhi ya dhahabu isiyozidi dola za Marekani bilioni mbili, wakati thamani ya sasa imefikia dola bilioni 3.24, hivyo kutokana na tofauti hiyo, benki inapanga kuuza kiasi kilichozidi kiwango kilichowekwa.
Amefafanua kuwa fedha zitakazopatikana kutokana na mauzo hayo zitawekezwa katika masoko ya fedha ya kimataifa kwa lengo la kuongeza mapato ya uwekezaji, na si kwa ajili ya kufadhili miradi ya serikali.
Akaro amesisitiza kuwa BoT ni chombo huru, na uamuzi wowote wa kutumia uwekezaji wake kufadhili miradi ya serikali unahitaji idhini ya Bunge.
Hadi jana Januari 29, 2026, BoT ilikuwa na akiba ya fedha za kigeni yenye thamani ya dola bilioni 6.52, na kati ya hizo, dhahabu inakadiriwa kuwa dola bilioni 1.2, dola za Marekani bilioni 3.8, na sarafu ya China (yuan) dola milioni 735.