Bora miaka 50 ya CCM kuliko miaka 5 ya UKAWA

Bora miaka 50 ya CCM kuliko miaka 5 ya UKAWA

vicdala55

kwasababu umekuja kama mtu mwenyeakili timamu naomba nikujibu point zako sita kama ifuatavyo.
1.kusudio la kuandika ni kuonyesha wasiwasi wangu juu ya hiki kikundi cha ukawa kama kweli ni watu watakaoweza kumeintain amani utulivu na mshikamano.
2.UKAWA kirefu chake ni umoja wa katiba ya wananchi sasa kwani umeambiwa ccm wanaunda katiba ya nani?
3.point ya usajili au katiba mimi hio point niliiweka ili kuondoa maswali ya kwamba wanajiita.
Mimi nawaona ni wahuni fulani kwasababu issue ilikuwa ni katiba sasa wamewaweka nyuma yao makundi au taasisi zingine na kutengeneza maslahi ya kisiasa kwa kumuanda mgombea mmoja.
Sasa je yale makundi mengine yatafaidikaje wakati kile kilichowapeleka kwenye bunge maalum kimegeuzwa.
4.nyumba3 kasri dubai bilioni uswiz ni hoja ambazo hazijibiki.
5.suala la amani ni la CCM peke yake kwasbb kama amani isingekuwepo bado tungewalaumu CCM kwavile ndie aliepewa dhamana ya kuziongozo ROHO na VIWILIWILI Milioni 45 vya binaadam.
6. Last,kuhusu kuigwa nenda Angola,Congo,Namibia,msumbii


Ndugu tofyo tuanze na hoja ya UKAWA.
Sote tunakubaliana kwamba si chama cha siasa hivyo ni ni sawa na kupiga Ramli unapokuja na mawazo ya kuwa na shaka nao endapo watadumisha amani ya Nchi. Hata hivyo, mpaka sasa hakuna matukio ya uvunjifu wa amani yaliyolopotiwa katika mikutano na harakati za UKAWA. UKAWA ni matokeo ya mchakato wa Bunge la Katiba na sio vinginevyo. Sijawahi kuonana popote kwamba hiki ni chama cha siasa hivyo uwe na mashaka nacho kwamba hakiwezi kuongoza Nchi, kiasi cha kuilinganisha na CCM, kwa hili kubali kwamba umechanganya hoja. Nitakubaliana na wewe kama utanitajia huyo mgombea mmoja wa UKAWA ni nani na uniambie. Hata hivyo si dhambi kwa wanasiasa kuungana na kuwa na mgombea mmoja katika uchaguzi. Kenya waliungana na akapatikana Mwai Kibaki, na hivi karibuni Uhuru Kenyata ingawa kabla aliwahi kuwa mgombea wa KANU, ujerumani Vyama vinaungana na majuzi muungano wa vyama vya upinzani vimechukua serikali huko India. Mifano ni mingi. Kuungana sio uhuni, vinginevyo utakuwa unajadili hoja kwa kuegemea upande mmoja hali ambayo huwezi kuwa na mawazo huru. Kuna watu ndani ya CCM wanakubaliana na fikra za UKAWA na wameonyesha msimamo wao hadharani hata kama hawakujiunga moja kwa moja na UKAWA....nina imani unawafahamu hata kwa majina. Tukubaliane kwamba UKAWA ni matokeo ya Bunge la Katiba. Hoja ya CCM wanaandika Katiba ya nani wala haihitaji muda mwingi wa kujiuliza,ipo wazi kwamba inahitaji Katiba itakayolinda maslahi yake, maneno na matendo yamejionyesha wazi. Ukiingia na msimamo wako katika uandishi wa Katiba,kamwe katiba utakayoipata haiwezi kuwa ya Wananchi. Rasmu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba (Imeundwa kisheria) ni matokeo ya ukusanyaji wa maoni ya Wananchi, niambie CCM imetoa wapi maoni inayoyasimamia? Hoja ya AMANI, naomba nirudie kukwambia kwamba amani yetu ni matokeo ya Watanzania wote kufuata sheria na taratibu za Nchi. Nchi hii ina umri wa zaidi ya miaka 50 tangu tulipojitawala wenyewe wakati Umri wa CCM hauzidi miaka 37 mpaka sasa. Kama amani yetu utaihusianisha na CCM pekee eti kwa sababu ndo inaongoza Nchi, basi tukubaliane kwamba na maovu yote ikiwa ni pamoja na huduma duni za Afya, Elimu, Miundombinu, rushwa, Madawa ya kulevya, wizi wa Mabilioni ya fedha za serikali mambo kama hayo vyote ni matendo ya CCM.
 
Sam sitta na wenzie waliwahi kuandamana wakisema ,,,,,,,,,,,,heri mkoloni kuliko nyerere!wewe mleta mada hatukushangai, akili zako na matope ya sokoni tandale ni sawa, kwa kutumia neno la kistaarabu!
 
Back
Top Bottom