Bora Kenya, Tanzania haipo salama kabisa

Bora Kenya, Tanzania haipo salama kabisa

Wa Tanzania tu wavivu wa kusoma na wakufikiri. Dhumuni la mwandiahi ni kutukumbusha kuwa tyna janga linali tupotezea maisha watu wengi hapa nchini na hatua stahiki haIja chukuliwa.
Wa tz huwa hatuoni athari ya jambo mpaka litufike physically. Hembu tiamke jamani haya magari yanatumaliza kwa kasi sana, unotoka nyumbani mzimaaa baadae familia inaletew taarifa ya kifo chako ama hauna miguu yote upo hospital. Hembu tuangalie tena na tena. Kila mmoja na jamii kwa ujumla tuchukue hatua. Kwanza kuepuka mwendo kasi, pili kuepuka kue.desha tukiwa tumelewa.
 
ugaidi na ajali za barabarani unaweza kuzicompare?
Hata mimi hii mada siielewi maana vita vya Al-Qaeda, Al-Shabab na wengineo wa IS wanahusianaje na ajali za barabarani amabazo zinatokana na uzuri wa barabara zetu
  • Hao madereva wala sio wasomali
  • hao madereva wanatoka Musama hadi Dar km1,000 au Songea - Arusha 1,000 masaa 16 utaacha kuchoka? utaacha kusinzia?
  • Barabara zetu si two traffic ways ni zile za kupishana ndani ya one way Traffic mtaacha kugongana uso kwa uso
ni heri tunayosikia Kenya juu ya mauaji yanayofanywa na Al shabab na serikali inafanya juhudi kubwa kudhibiti kuliko sisi ambapo
serikali imeshindwa kabisa kudhibiti AJALI ZA BARABARANI zinazotokea karibu kila siku sasa, na nyingi zikisababibishwa na uzembe wa madereva.

Si ajabu sasa kila ukiwasha TV, Kusikiliza redio au kusoma magazeti ukakumbana na habari ya ajali mbaya imetokea sehemu fulani na kuua watu kadhaa.
 
Al shabab imetumika kugusa hisia zetu. Angeandika ajali zinatumaliza labda wasomaji wangekuwa wachache kulinganisha na sasa, tusichepuke maada na kwenda kwenye mavita na ugaidi.
 
Wanabodi;

Nimekuwa nikifuatilia vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi.. Habari kubwa duniani kwa siku za hivi karibuni ni mauaji yanayofanywa na makundi mbalimbali ya kigaidi duniani (AL-QEDA, ISIS, BOKO HARAM, ALSHABAB etc) pamoja na ugonjwa wa Ebola.

Kwa sisi Tanzania tukio linalotugusa zaidi kwa ukaribu ni mauaji yanayofanywa na kundi la Al shabab katika nchi jirani ya Kenya. Sababu kuu ikiwa ni uwepo wa majeshi ya Kenya katika ardhi ya Somalia, pamoja na uvamizi unaofanywa na serikali ya Kenya misikitini katika kutafuta magaidi.

Wanabodi ukiona mwenzako ananyolewa wewe tia maji.. Ni muda tu unaweza sikia na sisi tumevamiwa (siombei) na hao maal shabab, just matter of time tu. So sio busara kuwasema wenzetu vibaya juu ya hilo.. Tujiangalie kwanza kama tupo salama.

Kiukweli hatupo salama hata kidogo, ni heri tunayosikia Kenya juu ya mauaji yanayofanywa na Al shabab na serikali inafanya juhudi kubwa kudhibiti kuliko sisi ambapo serikali imeshindwa kabisa kudhibiti AJALI ZA BARABARANI zinazotokea karibu kila siku sasa, na nyingi zikisababibishwa na uzembe wa madereva. Si ajabu sasa kila ukiwasha TV, Kusikiliza redio au kusoma magazeti ukakumbana na habari ya ajali mbaya imetokea sehemu fulani na kuua watu kadhaa. Serikali imeshindwa kabisa kuzinusuru roho zetu, heri Kenya inajitahidi kwenye al shabab.

Kwa wale madereva wenzangu mnajua tabia za askari wa usalama barabarani pale wanapokukamata na kosa, hicho kinachofanyika ambacho kimekuwa kama utaratibu wa kawaida ndio kinasababisha ajali za kila siku ambazo zinazozuilika. Trafiki anakukamata umezidisha abiria, badala ya kukwambia uwashushe, mkimalizana tu au akikupiga faini, safari inaendelea. Hivyo hivyo kwa spidi kubwa na ukaguzi wa matairi.

Serikali imeshindwa kudhibiti utoaji wa leseni kiholela.

Jiulize wakenya wangapi wanakufa kwa siku kutokana na Alshabab na Watanzania wangapi wanakufa kwa siku kutokana na ajali za kizembe za barabarani.. Mbaya zaidi naona wanatoaga takwimu feki za vifo au siku hizi habari hazitangazwi tena maana ajali ishakuwa kawaida.

TAFAKARI CHUKUA HATUA.



Ni kweli na wala hakuna unafuu wowote kwani serikali yetu kwa muda mrefu sasa iko likizoni kutatua matatizo ya nchi ila makada wao wako vijijini kuomba kura za urais mwakani.
 
Ni kweli na wala hakuna unafuu wowote kwani serikali yetu kwa muda mrefu sasa iko likizoni kutatua matatizo ya nchi ila makada wao wako vijijini kuomba kura za urais mwakani.

wewe jaribu uone kama serikali inatatua matatizo vijijini au kuomba kura, huwezi sema kwasababu mama anashinda kulea watoto nyumbani basi watakufa kwa njaa, jua baba anatafuta na watakula, ni mgawanyo tu wa madaraka, sasa jiongopee eti serikali inabishana jf, watu wako kazini 24/7 na ndio maana upo.
 
Hatuendi huko hata iweje,,, nchi yetu haina udini,,, hata upo si kwa level hiyo,,,, malengo ya vita ya kenya na somalia yangekuwa wazi tungewasaidia mbona congo tupo? hidden agenda zenu JK alisha zistukia na sisi tunamuunga mkono kwa hilo. kwanza ile coalition of the willing yenu imefikia wapi? si wawasaidie basi
 
hakuna kitu hatari kama kupambana na jitu joga lenye silaha na linalojua kuitumia (gaidi)!litawavizia wasio na silaha liwadhuru,uwanja wake wa vita ni makazi ya raia,lengo kuu ni kufanya kila njia raia wawe na hofu kama alivyo yeye!
 
Wa Tanzania tu wavivu wa kusoma na wakufikiri. Dhumuni la mwandiahi ni kutukumbusha kuwa tyna janga linali tupotezea maisha watu wengi hapa nchini na hatua stahiki haIja chukuliwa.
Wa tz huwa hatuoni athari ya jambo mpaka litufike physically. Hembu tiamke jamani haya magari yanatumaliza kwa kasi sana, unotoka nyumbani mzimaaa baadae familia inaletew taarifa ya kifo chako ama hauna miguu yote upo hospital. Hembu tuangalie tena na tena. Kila mmoja na jamii kwa ujumla tuchukue hatua. Kwanza kuepuka mwendo kasi, pili kuepuka kue.desha tukiwa tumelewa.

upo sawa kabisa mkuu...watanzania mpaka yawakute..ndo wanafumbuka
 
alshabab ni habari nyingine kabisa......
 
wewe jaribu uone kama serikali inatatua matatizo vijijini au kuomba kura, huwezi sema kwasababu mama anashinda kulea watoto nyumbani basi watakufa kwa njaa, jua baba anatafuta na watakula, ni mgawanyo tu wa madaraka, sasa jiongopee eti serikali inabishana jf, watu wako kazini 24/7 na ndio maana upo.


kweli wau wako kazini masaa 24/7 ila si serikali yetu hii.
 
Al shabab imetumika kugusa hisia zetu. Angeandika ajali zinatumaliza labda wasomaji wangekuwa wachache kulinganisha na sasa, tusichepuke maada na kwenda kwenye mavita na ugaidi.

Mkuu nashukuru kwa kuweza kuelewa lengo.. Nimejaribu kucheza na lugha na kugusa hisia za wachangiaji.. Bahati watanzania tu wavivu wa kusoma.. Wengi hawakusoma habari yote, baada ya kuona heading na neno Al shabab nililobold baaasi wakajikita hapo.. Ila 90% ya habari ni kuhusu ajali. Nway yote sawa lakini coz vyote ni threat.

Cool.
 
Back
Top Bottom