GODZILLA
JF-Expert Member
- Dec 26, 2014
- 5,902
- 10,503
Huko Tanganyika kila mtu mjuzi. Kwenye uandishi wa habari wamo, kwenye udaktari wamo, kwenye sheria wamo. Mradi tu kujitia ujuvi.
Kipindi cha Covid-19 Kila mtu aligeuka kuwa mwanasayansi na mchambuzi mahiri wa conspiracy theories na international propaganda!
Juzi kuna makanjanja wamekamatwa muhimbili pale wakijifanya madaktari. Kasoma soma tu videsa vya Google kajitunuku na cheti cha udaktari yeye mwenyewe!
Ndio sampuli ya watu waliomo mitandaoni wakipotosha na kutoa ushauri batili watu wakiwaamini kuwa ni madaktari. Ndio hawa wa "Kunywa juisi ya mchaichai, meza karafuu, fanya vile na vile...." tafrani tu.
Kipindi fulani palizuka vishoka mahakamani lakini wakadhibitiwa ipasavyo. Kukopi kopi tu gugo na yeye kashakuwa wakili.
Ndio sampuli ya watu humu wanatoa ushauri batili wa kisheria mitandaoni kisha watu wakaamini ni ushauri sahihi.
Majukwaa ya sheria na majukwaa ya madaktari yadhibitiwe, na ushauri wowote unaotolewa humo uchukuliwe kwa tahadhari kubwa.
Kama una shida ya kitabibu ama kisheria tembelea hospitali na ofisi za mawakili.
BE SO WARNED!
Kipindi cha Covid-19 Kila mtu aligeuka kuwa mwanasayansi na mchambuzi mahiri wa conspiracy theories na international propaganda!
Juzi kuna makanjanja wamekamatwa muhimbili pale wakijifanya madaktari. Kasoma soma tu videsa vya Google kajitunuku na cheti cha udaktari yeye mwenyewe!
Ndio sampuli ya watu waliomo mitandaoni wakipotosha na kutoa ushauri batili watu wakiwaamini kuwa ni madaktari. Ndio hawa wa "Kunywa juisi ya mchaichai, meza karafuu, fanya vile na vile...." tafrani tu.
Kipindi fulani palizuka vishoka mahakamani lakini wakadhibitiwa ipasavyo. Kukopi kopi tu gugo na yeye kashakuwa wakili.
Ndio sampuli ya watu humu wanatoa ushauri batili wa kisheria mitandaoni kisha watu wakaamini ni ushauri sahihi.
Majukwaa ya sheria na majukwaa ya madaktari yadhibitiwe, na ushauri wowote unaotolewa humo uchukuliwe kwa tahadhari kubwa.
Kama una shida ya kitabibu ama kisheria tembelea hospitali na ofisi za mawakili.
BE SO WARNED!