Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

meningitis

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
8,464
Reaction score
4,828
Tunaposema huu upuuzi wa vyuo vya kata hautakiwi watu wanasema tuna dharau bora jamii inajionea yenyewe.
Ati mtu alifeli kidato cha nne leo hii anapewa cheti cha kuwa daktari...ukiuliza nini eti ooh tunapunguza uhaba wa madaktari...pambaff sana.



MY TAKE


  • SERIKALI INATAFUTA KURA
  • G.ABACHORI ANASAKA NOTI
  • MLALAHOI ANASAKA AJIRA YA URAHISI
Serikali ingewekeza katika vyuo vya utabibu kama vile KILOSA,KIBAHA,MVUMI na MACHAME tungeweza kuwa na vyuo bora sana kuliko IMTU lakini kwa kuwa serikali na jamii yetu inaamini mafanikio yanakuja kwa kukurupuka na bahati bahati haya ndio matokeo yake.

Roma haikujengwa kwa siku moja,vile vile taasisi kama MUHAS,UDSM,SUA,MUCCOBS hazikujengwa siku moja.

Leo hii unashuhudia chuo kama KAM MEDICS kinafundisha matabibu usishangae mwakani kinatoa degree ya udaktari,udaktari wa meno,pharmacy,na kozi nyingine lukuki bila kujipanga halafu unategemea ilinganishwe na MUHAS...huu ni uhuni.

Nasikia sikia kuwa UDSM ilianza kama kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha EAST AFRICA leo hii ni university yenye courses lukuki sasa linganisha na UDOM na mikozi yake lukuki iliyoanza juzi juzi halafu uniambie itakuwa sawa na UDSM...what a joke?go to ARUSHA UNIVERSITY,MAKUMIRA UNIVERSITY n.k ujionee idadi ya course zilizopo kulinganisha na resources.

Mbona taasisi kama DIT imebakia kuwa tech college na inatoa wahitimu wazuri tu bila hata kujipachika u-UNIVERSITY?

Tuache utani wa elimu hasa hasa elimu inayohusu afya.

Miaka takribani 15 tumeshuhudia wanafunzi wa sekondari wakifeli masomo ya sayansi vibaya sana PCB ikiwemo halafu linganisha na idadi ya wanafunzi wa udaktari katika kipindi hicho(waweza kuta zinalingana au hata kuwa kubwa kwa wahitimu wa elimu za afya) sasa utajiuliza wametokea wapi?

Muhimbili ilikuwa inadahili wanafunzi kati ya 70-150 kipindi kile cha watoto wakifaulu vizuri na nusu au robo tatu kati yao walikuwa wanadisco sasa leo hii Muhimbili anatoa 200,KCMC 100,Bugando 70,IMTU 90 n.k hii akili ya ukubwani au vyuoni imetokea wapi ghaflaghafla?....Tunaendekeza siasa ee?tunajidanganya wenyewe!

Siamini kama ni number ya watumishi wa afya waliopikwa nusu ndio imetuletea matokeo mazuri tunayoyaona kwenye afya kwa sasa bali ni juhudi za USA na wenzake.

Matokeo ya elimu hii ya kata ni uwepo wa semina nyiingi zinazoenda kwa jina la 'ON JOB TRAINING" hii inadhihirisha kuwa mabomu yaliyotegwa na vyuo vyetu inabidi yateguliwe..swali ni kwamba tutaweza kuyategua yote kwa wakati kabla hayajalipuka?...jibu ni hapana na mengine ndio hayoo yanalipuka!
by Jackbauer
 
Last edited by a moderator:
UDOM ndio usiseme,maana hata wakufunzi wao ni vituko!!unakuta lecturer anashindwa challenge kidogo tu toka kwa wanafunzi,maana anakua hanatofauti yoyote ya ufahamu wa mambo kulinganisha na wanafunzi wake.hili nalo ni bomu lingine kaka.
 
aliyekwambia walimu wote wa m/s watakuwa na shahada ninani? .
 
UDOM ndio usiseme,maana hata wakufunzi wao ni vituko!!unakuta lecturer anashindwa challenge kidogo tu toka kwa wanafunzi,maana anakua hanatofauti yoyote ya ufahamu wa mambo kulinganisha na wanafunzi wake.hili nalo ni sbomu linguine kaka.

wanaofundisha hapo wengi ni graduates wa miaka ya 2000 na kuendelea!
 
UDOM ndio usiseme,maana hata wakufunzi wao ni vituko!!unakuta lecturer anashindwa challenge kidogo tu toka kwa wanafunzi,maana anakua hanatofauti yoyote ya ufahamu wa mambo kulinganisha na wanafunzi wake.hili nalo ni bomu lingine kaka.

Huwezi kuwa unaongelea lecturer!!!!!
Na kwa premise yako unamaanisha lecturers wa hapo wote wamehitimu hapo na waliowafundisha walihitimu hapo??!!!!

Lecturers wengi pale walitoka UDSM, SUA na MZUMBE na sasa ndio wameanza kutoa Lecturers wao ambao pia
wengi First degrees na Masters zao hawakusoma pale au mtu akifika pale tu maarifa yanamuisha???!!!
 
haya bhana naona heri zenu mnaosoma vyuo vya taifa, mtuache na kata zetu maana tumeshaanza kuitana muhimbili na yule'wa Udom
 
Tunaposema huu upuuzi wa vyuo vya kata hautakiwi watu wanasema tuna dharau bora jamii inajionea yenyewe.
Ati mtu alifeli kidato cha nne leo hii anapewa cheti cha kuwa daktari...ukiuliza nini eti ooh tunapunguza uhaba wa madaktari...pambaff sana.
Sasa UDOM wameingiaje hapo? Maelezo yako hayaonyeshi bomu la UDOM.
 
Point yako ikiwa nini???!!!
Vyuo vyote vina graduates wa miaka hiyo kuanzia tutors mpaka madaktari!!!

Udaktari ni kama ufundi bomba,mtoto wa fundi bomba atafundishwa ufundi bomba na baba yake mpaka pale baba yake atakapofariki ndipo mtoto huyu kipindi hiki akiwa kijana ataanza kuifanya vizuri kiasi kazi ya ufundi bomba na hatimaye na yeye atamfundisha mwanawe.

huwezi ukamaliza MD5 halafu uende kufundisha madaktari halafu tutegemee madaktari hao wawe wazuri...never!!ukienda Muhimbili utawakuta mababu,mababa na makaka kwa ujumla wao ndio wanwafundisha madaktari...hii ni sawasawa na uingereza,marekani na maeneo mengine wanaojitambua na sio IMTU au UDOM au Agha khan ya bongo au kwa sasa IFAKARA.

Endelea kubisha ila mtaendelea kuumbuka
 
Kunajamaa angu ng'ombe kweli PCB alipata four kaenda chuo uchwara flani eti saiv ansfundisha madactari udim

Hivi unajua maprofesa na madaktari wengi tu walianzia diploma???!!!
Hebu weka vyuo alivyopita tuone kama kuna sehemu utaratibu haukufuatwa.
 
Kweli vichaa hawataisha dunia hii, Wale madaktari walio pasua mgonjwa kichwa badala ya goti wamesoma Udom? Hao mawaziri mizigo wamesoma Udom? Wewe unaeropoka humu Jf umelisaidia nini taifa hili kama sio kutwa kuropoka kwenye mitandao ya kijamii na vijiwe vya ghahawa?
 
Kweli vichaa hawataisha dunia hii, Wale madaktari walio pasua mgonjwa kichwa badala ya goti wamesoma Udom? Hao mawaziri mizigo wamesoma Udom? Wewe unaeropoka humu Jf umelisaidia nini taifa hili kama sio kutwa kuropoka kwenye mitandao ya kijamii na vijiwe vya ghahawa?

Unamjua daktari aliyefanya upasuaji huo alisoma wapi au unaropoka tu?
 
Back
Top Bottom