Bomani Committee hiding the truth?

Ripoti ya Tume imewasilishwa bungeni. Therefore it is public. Please note that the summary I posted is the unofficial version of a popularised summary of the report. It is NOT the full report. The final popular version (with cartoons) will be posted on www.policyforum.or.tz some time next week.
 
Sheria mpya ya madini kuanza kutumika ramsi Aprili mwakani
broken-heart.jpg
Na Kizitto Noya

WAZIRI wa Nishati na Madini William Ngeleja amesema sheria mpya ya madini itakamilika na kuanza rasmi kutumika Aprili mwakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri Ngeleja alisema kwa sasa izara yake inakamilisha sera ya sheria hiyo kabla ya kutengeneza muswada na kuufikisha bungeni kwa ajili ya kutungwa sheria.

"Bado tuko katika mchakato wa kukamilisha sera, lakini ni mategemeo yetu kwamba zoezi hili tutalikamilisha mwishoni mwa mwaka huu na sheria nyenyewe iwe tayari ifikapo Aprili mwakani,"alisema.

Waziri Ngeleja alisema hayo alipokuwa akijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari aliowaita ofisini kwake kuzungumzia hatma ya mgodi wa almasi wa Williamson Limited (Mwadui).

Alisema katika sheria hiyo mpya, serikali inapitia vipengele mbalimbali kuhakikisha haiwabani kukindi cha watu na kuwapa unafuu wengine bali iwe ni sheria inayojali maslahi ya taifa kwa kuhakikisha matumizi ya rasilimali zake yanakuwa kwa faida ya wananchi.

Maandalizi ya sheria hiyo mpya ya madini yametokana na kazi ya kamati aliyoiunda Rais Jakaya Kikwete Novemba 12 mwaka jana kupitia mikataba yote ya madini na kupendekeza maboresho ili rasilimali hiyo ya taifa ivunwe kwa manufaa ya nchi.

Rais Kikwete aliiagiza kamati hiyo iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta ya madini na kupitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali.

Kamati hiyo ambayo awali ilitakiwa kukamilisha kazi hiyo ndani ya miezi mitatu, ilikuwa na jukumu la kukutana na taasisi zinazosimamia madini na wadau wengine, kupitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zitakazohusu migodi mikubwa nchini.

Mbali na Jaji Bomani, wajumbe wengine walioteuliwa katika kamati hiyo ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe na Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo.

Wajumbe wengine ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Rais pia alimteua Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWater Coopers, David Tarimo ambaye ni mtaalam wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo kushirikiana na wenzao hao katika kazi hiyo.

Kuundwa kwa Kamati hiyo kunafuatia hoja binafsi ya Zitto Kabwe aliyoitoa bungeni kutaka kuundwa kwa Kamati Teule yakuchunguza mazingira ya kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi huko Uingereza na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi Februari mwaka huu.

Baada ya kuwasilisha hoja hiyo, Kabwe alifungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi hapo Januari mwakani. Hatua hiyo ya Bunge iliibua mjadala mkubwa miongoni mwa makundi mbalimbali wakihoji sababu za kumfungia mbunge huyo kijana. Hivi karibuni wakati Rais Kikwete akihutubia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi katika Ukumbi wa Kizota , mjini Dodoma aliahidi kuunda kamati hiyo itakayojumuisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuangalia mikataba mipya ya madini.
Tuma maoni kwa Mhariri
Facebook
 
Yaani Waziri anaconfirm kabisa kwamba bunge la Tanzania ni rubber stamp, hivi wabunge wanajisikiaje wakisoma maneno kama haya.

WAZIRI wa Nishati na Madini William Ngeleja amesema sheria mpya ya madini itakamilika na kuanza rasmi kutumika Aprili mwakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri Ngeleja alisema kwa sasa izara yake inakamilisha sera ya sheria hiyo kabla ya kutengeneza muswada na kuufikisha bungeni kwa ajili ya kutungwa sheria.

Anaongea kama it is a foregone conclusion sio tu kwamba itapita bungeni, bali anayo mpaka timeframe kwamba itakuwa tayari kutumika by April.

This is another jewel in our supposedly checking and balancing high drama.

Hakuna hata kuwastahi wabunge kwa kusema "tunatarajia" or any of that sensitivity nonsense, the bunge is out b.i and it will pass this shy by April, full stop. And this is a direct quote, so no "lost in translation" excuse.

Circuses without bread!
 
Walikuwa wanasubiri wakubwa waipitie kwanza hiy sheria kuona kama inawafaa kwa matumizi yao
 
Yaani Waziri anaconfirm kabisa kwamba bunge la Tanzania ni rubber stamp, hivi wabunge wanajisikiaje wakisoma maneno kama haya.


Anaongea kama it is a foregone conclusion sio tu kwamba itapita bungeni, bali anayo mpaka timeframe kwamba itakuwa tayari kutumika by April...

Wabunge wanajisikia poa tu walichofuata bungeni ni posho na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. As long as bunge ni la chama kimoja litabaki kuwa mchezo wa kuigiza tu. Wanavuta vuta muda waendelee kula vi ten percent vyao, Ikifika mwaka wa uchaguzi ndio wa take action. Swali la kujiuliza ni Watanzania tunajisikiaje kudanganyika kila mwaka?


.
 
wabunge wanatakiwa kumtaka Waziri aombe msamaha kwa kauli yake hiyo iliyo presumptive, na angalau atoe statement kwamba hiyo ni projection inayotegemea kama bunge itaupitisha muswada kuwa sheria.

Otherwise watakuwa wamekubali kwamba wao ni rubber stamp, and this include the opposition.
 
Waziri wa Nishati na Madini, Mh. William Ngeleja alitamka hapo October 2009 mbele ya waandishi wa habari kuwa sheria mpya ya madini itakamilika na itaanza kutumika April mwaka huu, 2010. Kama ilivyokawaida ya viongozi wetu kutamka mambo wakiwa na uhakika (kwa mambo ambayo hayajapitishwa kisheria - hata kama); Mh. Ngeleja alitamka hayo akiwa na uhakika kwamba sheria itapitishwa na Bunge, jambo lililo jema kwa matarajio ya wengi wetu.

Sasa kwa vile mwezi Aprili hauko mbali, na ili kujaribu kuepuka 'korogo' jingine Bungeni kama ilivyotokea kwenye muswada wa Baraza la Usalama wa Taifa uliowakilishwa na Mh. Sophia Simba hivi karibuni; kwa walio karibu na mabadiliko tutarajiayo katika kulinufaisha Taifa letu, tafadhali tusaidieni kujibu swali moja la msingi - Je, ni asilimia ngapi Watanzania tutanufaika nayo kutoka kwenye uchimbaji wa madini unaofanywa na kampuni za kigeni?


Steve Dii
 
By Correspondent Gadiosa Lamtey
16-05-2008



Reports that the Mining Review Committee is yet to get a chance to present its findings to President Jakaya Mrisho Kikwete are incorrect, a lecturer with the University of Dar es Salaam has said.

It has been reported that the all inclusive committee formed to review mining contracts and recommend corrective measures is yet to submit its report to President Jakaya Kikwete, although the assignment was completed almost two months ago.

State House Communication Director Salva Rweyemamu told The Guardian yesterday the President had not yet received the report from the committee. Also, Committee Chairman Judge Mark Bomani said the report had been completed and was ready for submitting.

``The report is ready. We are only waiting for the President to give us a date when to submit it,`` Bomani said.

However, a Dar es Salaam-based political analyst Dr Laurean Ndumbaru said the appointed committee had not yet completed its task of preparing the final report before submitting it to the President.

``What they are supposed is to tell the truth that they have not yet finalized the report,`` said Dr. Ndumbaro, senior lecturer at the University of Dar es Salaam.

He said the Committee could submit its report to Chief Secretary Philemon Luhanjo who would take it to the President.

He urged the committee to speed up the process by submitting the findings to the responsible authority on time as the public seemed to be tired of unfulfilled promises.

Asked to comment on allegations that his team was dillydallying because it was still finalizing its report, Judge Bomani said that the claims were untrue. ``We have completed our work. We are only waiting for the President to tell us when we can present him the findings.

We cannot present the recommendations to the Chief Secretary, because he is not the one who gave us the assignment. If you want, you can call the Chief Secretary if he is indeed the one who assigned us the task,`` Judge Bomani said and hung up.

The commission, which was formed by President Kikwete at the end of last year, was given until February this year to complete work and submit its recommendations.

It was tasked with reviewing commercial mining contracts and making recommendations that would enable the country to reach a win-win understanding with investors in the mining sector.

The committee was composed of opposition and ruling party legislators, mining experts and other government officials. It was also tasked to review laws governing the industry as well as analyse the taxation system in the mining industry.
Currently, mining companies pay three (3) per cent royalty, an amount seen as peanuts comparing to what they are reaping.

Commenting on the delay, Kahama MP-CCM, James Lembeli said the government decided to form the Mining Contracts Review Committee following the unfolding of the scandal on the Buzwagi mining contract.

``It was because of the on-going allegations on Buzwagi Mine, which is located in my constituency, that the committee was formed. I therefore wonder what has caused a delay in the presentation of the review team`s findings. The people are eager to know the recommendations,`` he said.

Lembeli said further delays could raise suspicion that the team`s report could be tampered with in the meantime. ``Let the document be presented to the President so that people`s faith in their government is preserved,`` the MP said.

Geita legislator-CCM, Ernest Mabina said MPs were eagerly waiting for the mining review team`s report so that they would discuss it. He said any delay in submitting the findings did not do justice to the wananchi.

`However, I understand that the terms of reference given to the committee covered a lot of areas, yet the time span for presenting the report had elapsed, there is a need to make the presidential probe team`s findings public,`` he said.

The MP called upon members of the public to remain patient until the time when the report would be presented.

On his part, Karatu Chadema MP Dr Wilbrod Slaa said lack of seriousness on national resources by the government was the main reason for its delay in making the report public.

Dr Slaa said the committee was supposed to submit its report in February this year although it is now May and nothing had been submitted yet. ``The government is not serious with its natural resources,`` Dr. Slaa said.

The opposition MP said the report should be made public for every Tanzanian to weigh whether they were getting a fair share from the mining industry or not.

The committee was made up of Judge Bomani, Kigoma North MP Zitto Kabwe, (Chadema), Kyela MP Dr Harrison Mwakyembe (CCM), Ezekiel Maige (Msalala, CCM), John Cheyo (Bariadi East, UDP) and Peter Machunde of the Dar es Salaam Stock Exchange.

Others were David Tarimo, a tax consultant with PricewaterhouseCoopers, Maria Kejo, director of civil and international law in the Ministry of Justice and Constitutional Affairs, Salome Makange, chief legal officer at the Ministry of Energy and Minerals, Mugisha Kamugisha, commissioner for policy in the Ministry of Finance and Edward Kihundwa, assistant director for human settlements in the Ministry of Lands, Housing and Human Settlements.

SOURCE: Guardian
Hii ripoti ya Jaji Bomani Haikufanyiwa kazi
 
Aliwahi kusema Rais Ali Hassan Mwinyi - Ruksa : Tanzania ni kichwa cha Mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa. That is what I said insanity is just doing the same thing over and over again expecting different results. Hiyo tume ingekuwa ya Bunge au ya Kimahakama ingekuwa na independence na ingepaswa kutoa findings hadharani! Kwa kuwa hiyo Kamati imetokana na utashi at he pleasure of the president it has to dance to his tunes. Who pays the piper chooses the music. Kwa uharaka wa kamati it is apparent hata hizo hadidu za rejea ni za Voda Fasta. Why are we always in hurry kwanini hatatitaki kushirikisha Ubongo? A very serious matter being done without a clear strategy? Kwani kamati ingeundwa taking on board cross cutting stakeholders kungekuwa na ubaya gani au ni kule kukurupuka which is a default approach by CCM?
 
Sheria mpya ya madini kuanza kutumika ramsi Aprili mwakani
broken-heart.jpg
Na Kizitto Noya

WAZIRI wa Nishati na Madini William Ngeleja amesema sheria mpya ya madini itakamilika na kuanza rasmi kutumika Aprili mwakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri Ngeleja alisema kwa sasa izara yake inakamilisha sera ya sheria hiyo kabla ya kutengeneza muswada na kuufikisha bungeni kwa ajili ya kutungwa sheria.

"Bado tuko katika mchakato wa kukamilisha sera, lakini ni mategemeo yetu kwamba zoezi hili tutalikamilisha mwishoni mwa mwaka huu na sheria nyenyewe iwe tayari ifikapo Aprili mwakani,"alisema.

Waziri Ngeleja alisema hayo alipokuwa akijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari aliowaita ofisini kwake kuzungumzia hatma ya mgodi wa almasi wa Williamson Limited (Mwadui).

Alisema katika sheria hiyo mpya, serikali inapitia vipengele mbalimbali kuhakikisha haiwabani kukindi cha watu na kuwapa unafuu wengine bali iwe ni sheria inayojali maslahi ya taifa kwa kuhakikisha matumizi ya rasilimali zake yanakuwa kwa faida ya wananchi.

Maandalizi ya sheria hiyo mpya ya madini yametokana na kazi ya kamati aliyoiunda Rais Jakaya Kikwete Novemba 12 mwaka jana kupitia mikataba yote ya madini na kupendekeza maboresho ili rasilimali hiyo ya taifa ivunwe kwa manufaa ya nchi.

Rais Kikwete aliiagiza kamati hiyo iliyoongozwa na Jaji Mark Bomani kuchambua mfumo wa kodi unaotumika katika sekta ya madini na kupitia mfumo wa usimamizi wa shughuli za uchimbaji mkubwa unaofanywa na serikali.

Kamati hiyo ambayo awali ilitakiwa kukamilisha kazi hiyo ndani ya miezi mitatu, ilikuwa na jukumu la kukutana na taasisi zinazosimamia madini na wadau wengine, kupitia mikataba ya madini na nyaraka nyingine zitakazohusu migodi mikubwa nchini.

Mbali na Jaji Bomani, wajumbe wengine walioteuliwa katika kamati hiyo ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe na Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo.

Wajumbe wengine ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Rais pia alimteua Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWater Coopers, David Tarimo ambaye ni mtaalam wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo kushirikiana na wenzao hao katika kazi hiyo.

Kuundwa kwa Kamati hiyo kunafuatia hoja binafsi ya Zitto Kabwe aliyoitoa bungeni kutaka kuundwa kwa Kamati Teule yakuchunguza mazingira ya kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi huko Uingereza na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi Februari mwaka huu.

Baada ya kuwasilisha hoja hiyo, Kabwe alifungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi hapo Januari mwakani. Hatua hiyo ya Bunge iliibua mjadala mkubwa miongoni mwa makundi mbalimbali wakihoji sababu za kumfungia mbunge huyo kijana. Hivi karibuni wakati Rais Kikwete akihutubia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi katika Ukumbi wa Kizota , mjini Dodoma aliahidi kuunda kamati hiyo itakayojumuisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuangalia mikataba mipya ya madini.
Tuma maoni kwa Mhariri
Facebook
Hii sheria ya madini bado night mbaya kwa kuwa ilishindwa kufuata maadhimio mengi ya kamati ya Bomani. Kwa mfano, haiondoi usiri wa mikataba ya maďini pamoja na malipo kwa serikali.
 
Hii sheria ya madini bado night mbaya kwa kuwa ilishindwa kufuata maadhimio mengi ya kamati ya Bomani. Kwa mfano, haiondoi usiri wa mikataba ya maďini pamoja na malipo kwa serikali.

Sheria inasemaje kuhusu uchenjuaji na usafishaji madini nje ya nchi?
 
Back
Top Bottom